Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Uwekezaji vya Nkwenda na Murongo? (b) Je, ni lini ujenzi wa Vituo hivyo utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba niseme, taarifa za soko kukamilika kwa asilimia 50 siyo kweli, labda tuambiwe 20 mpaka 30, lakini pia soko hilo limesimama kuendelezwa tangu mwaka 2013. Swali la hivyo lilijitokeza Bungeni mwaka 2016 na taarifa iliyotoka ni kwamba, Nkwenda ilitengewa shilingi milioni 385….

MWENYEKITI: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja, lakini pointi yangu ni kwamba, kumekuwepo na taarifa za kutenga fedha tangu mwaka 2016/2017 ambazo hazijaenda. Sasa swali, hizo bilioni 2.5 kama tumeahidiwa muda mrefu na hazijaenda, zitakwenda kweli?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wilaya ya Kyerwa iko mpakani, inapata faida ya kuwa na Rwanda na Uganda, hakukuwa na juhudi zozote za kujenga viwanda na kuifanya wilaya kuwa damping place ya bidhaa kutoka Uganda. Nini mkakati wa Wizara kujenga viwanda katika wilaya hii ili kuifungua?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kama alivyokiri kwamba swali hili lilishawahi pia kuulizwa na Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Jimbo hilo na msisitizo wetu ni uleule, kwamba Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Kilimo na Serikali kwa ujumla, pamoja na Waheshimiwa Wabunge, ni kwamba tunayo dhamira ya dhati, kuhakikisha kwamba, masoko haya ya mpakani yanaimarishwa, ikizingatiwa kwamba hiyo ni sehemu ya kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakumbuka kwamba tarehe 6 Septemba, 2019 Marais wetu, kutoka Uganda pamoja na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, walifanya mkutano kupitia Baraza la Biashara wa kuimarisha biashara za mipakani. Kwa hiyo, suala hilo ni la kipaumbele na litafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusiana na kujenda viwanda, hiyo ni moja ya fursa ambazo ziliibuliwa katika kongamano hilo la wafanyabiashara na nimhakikishie tu kwamba, kadri muda unavyoenda, hayo yote yatashughulikiwa kwa nia ya kuongeza tija ya bidhaa zetu na kuhakikisha kwamba wananchi wetu wa Afrika Mashariki na Tanzania wanafaidika kwa pamoja.