Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa barabara ambayo inatoa Makao ya Wilaya kwenda Utegi inasumbua kwa muda mrefu na kwa muda mrefu imekuwa ni ahadi ambayo bado haijafanyiwa kazi. Je, Serikali sasa itakuwa tayari kuiangalia wakati inasubiri hiyo ahadi ya Rais ya muda mrefu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa ahadi za Rais ziko nchi nzima na Wilaya ya Kilolo pia tulikuwa na ahadi kama hiyo ambapo Rais alikuwa amesema barabara ya kutoka Kilolo - Iringa ingeanza kujengwa mara moja. Sasa tayari tunaelekea kwenye uchaguzi na ilikuwa ahadi ya kabla ya uchaguzi. Je, Serikali inasemaje ili wananchi wa Kilolo wajue umuhimu wa Serikali ya Awamu ya Tano? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme Serikali inatekeleza maagizo na ahadi zote za Ilani ya Chama cha Mapinduzi na pia itaendelea kutekeleza maagizo yote ya Viongozi wetu Wakuu wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Utegi itajengwa kutokana na upatikanaji wa fedha ndiyo maana usanifu umeendelea. Kwa hiyo, tukishamaliza usanifu, tukapata fedha itajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini barabara yako Mheshimiwa kama ambavyo tumeshaongea hata nje ya hapa kwamba barabara ile tayari imeingizwa kwenye Mpango wa Benki ya Dunia. Ni taratibu zinaendelea baadaye itajengwa kwa kiwango cha lami.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza niipongeze Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujenga daraja la muda la Nderema ambalo linaunganisha Wilaya ya Kilindi na Handeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuipongeza Serikali, naomba niulize swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mvua hizi hazikutegemewa na zimeharibu sana barabara kuanzia Handeni – Kibirashi - Songe – Gairo. Je, Serikali iko tayari kutuma wataalamu kwenda kuangalia hali ya uharibifu ili kuweza kurejesha mawasiliano katika eneo hili? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja dogo la Mheshimiwa Kigua, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nitoe taarifa kwamba kwa mujibu wa usanifu wa barabara mvua zina return period tatu; kuna ya miaka kumi, hamsini na miaka mia moja. Mvua iliyonyesha juzi Tanga inaonekana ina return period ya miaka mia moja na ambayo design huwa haijumuishi returned period hizo lakini kwa mujibu wa swali lako Mheshimiwa Mbunge tuko tayari.

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri swali moja dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeahidi kujenga barabara ya Kaliua - Chagu (km 48) na walituambia kwamba tayari walishapata mfadhili wa kuijenga barabara hiyo. Ni lini sasa ujenzi wa barabara wa hiyo km 48 tu utaanza? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja dogo la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza barabara hiyo siyo kilometa 48 ni kilometa 36, tenda tumeshatangaza wakati wowote tunasaini mikataba. Baada ya kusaini mikataba kuanzia tarehe ile tuliyosaini tutakwambia sasa tunaanza lini na tunakamilisha lini.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Barabara ya kutoka Mangamba - Kilambo - Msimbati itajengwa lini kwa kiwango cha lami kwa sababu ni Sera ya Serikali barabara zinazounganisha nchi kuzijenga kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba usanifu wa barabara hiyo ya kutoka Mtwara Mjini - Kilambo tumeshakamilisha. Ni nia ya Serikali kuhakikisha tumeijenga kwa kiwango cha lami pamoja na daraja ili tuweze kuungana kwa daraja la pili kwa ajili ya kwenda Mozambique.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba niulize swali langu la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa ziarani Wilayani Ruangwa alitoa maelekezo kwamba barabara kutoka Ruangwa - Nachingwea - Masasi na Ruangwa -Nachingwea - Nanganga zijengwe kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Rais akitoa kauli inakuwa ni maagizo. Je, lini upembuzi yakinifu utaanza kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja dogo la Mheshimiwa Salma Kikwete, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Salma Kikwete ni kwamba upembuzi yakinifu na usanifu wa kina tumeshakamilisha. Ujenzi tumeshaanza na tayari tumeshajenga km 5. Kwa hiyo, maagizo ya Mheshimiwa Rais kama alivyosema ni sheria lazima tutayatekeleza.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais Jimboni Ukerewe mwaka jana tarehe 5 Septemba, 2018, alitoa maelekezo ya ujenzi wa km 14 za lami kutoka Lugeze - Nansio mjini. Nataka kujua ni hatua ipi imefikiwa ili ujenzi huo uweze kuanza? Nashukuru sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu barabara hii ameifuatilia muda mrefu na matokeo yake niseme kwamba usanifu wa barabara hii umeshaanza ukikamilika tutajenga barabara hii kwa kiwango cha lami.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 7

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ahadi hizi za Rais ziko maeneo mengi na Vunjo maeneo ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Himo iliahidiwa kujengewa barabara kwa lami km 7 na sasa kuna mafuriko eneo la lower area Kahe kuanzia Fungagate, Kahe, Kiomu mpaka maeneo ya Chekereni na Kilema Hospital. Barabara zote hizi ziliahidiwa na Mheshimiwa Rais kujengwa kwa kiwango cha lami na Serikali inajua. Ni lini watatekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja dogo la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme ni kweli ziko ahadi nyingi za Mheshimiwa Rais lakini katika barabara zimewekewa utaratibu wake. Tunaanza kwanza kukamilisha barabara kuu na zile zinazounga mipaka ya majirani zetu baadaye tutakwenda kwenye barabara za mikoa na tunarudi tena chini kwenye barabara hizo za vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge wewe tulia tu ni kwamba Ilani ya Chama cha Mapinduzi na ahadi za viongozi lazima zitekelezwe.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 8

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Nangurukuru - Liwale ni ya vumbi na kokoto lakini naishukuru Serikali mwaka huu tumetengewa fedha shilingi milioni 300 kuanza usanifu wa kina. Hata hivyo, mvua zilizonyesha mwezi uliopita zimelaza watu siku tatu barabarani. Ni nini mkakati wa Serikali kuifanya barabara hii ipitike majira yote? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Mbunge Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema mwenyewe tumetenga fedha kwa ajili ya kuifanyia usanifu wa awali na usanifu wa kina, malengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami ili haya matatizo ya mvua yanapojitokeza yasije yakaleta athari kwa wananchi. Hata hivyo kwa vile umetuambia tutaifanyia kazi, hela ya emergency ipo ili tuweze kurudisha hiyo miundombinu wananchi waendelee kutumia barabara hiyo.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 9

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Ruaha National Park Iringa ni ahadi ambayo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne na Awamu ya Tano na mpaka sasa ni upembuzi yakinifu tu unaendelea kwa miaka yote hiyo kumi na tano. Ni lini sasa barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami ili kusaidia wale watalii wanaokwenda kule waweze kwenda kwa ufasaha? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara anayoizungumza inaitwa jina Iringa - Msembe (km 104). Barabara hiyo ilikuwa imewekwa kwenye mafungu mawili; moja ni la ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Nduli ambao tumeshatangaza tenda na mkandarasi amepatikana wakati wowote tutasaini mkataba. Hizi km 104 tayari tumeshamaliza mpaka usanifu wa kina na tumeomba fedha kutoka Benki ya Dunia. Kwa hiyo, wananchi wa Iringa, tena ndiyo nimeoa kule, shemeji zangu wale, wala asiwe na wasiwasi barabara ile inajengwa.

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 10

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Serikali ina mpango gani wa kutenga pesa kwa ajili ya upembuzi yakinifu kwa barabara ya kutoka Njia Nne - Kipatimu (km 50)? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la rafiki yangu Mheshimiwa Ngombale ,kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungumza mara nyingi juu ya barabara hii. Niombe tu tuwasiliane ili tuone kwa sababu kwenye Mipango Mikakati yetu katika Wizara tumeiweka katika Mpango ili tuweze kuendelea na hatua ya ujenzi wa lami. Kwa hiyo, tuonane na Mheshimiwa Mbunge ili nimpe taarifa za kukutosha ili aweze kutoa maelezo mengi kwa wananchi wake. Ahsante.