Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE (MHE. AMINA S. MOLLEL) aliuliza:- Shule ya Viziwi Mwanga hutoa Elimu ya Msingi kwa Watoto wasiosikia na wasioongea kwa Mikoa ya Kilimanjaro, Tanga na Arusha; wanapohitimu Elimu ya Msingi, Wanafunzi hao hujiunga na Shule za Sekondari za kawaida ambazo hazina Walimu wenye Taaluma Maalum, vifaa na mazingira rafiki kwa Watoto wenye ulemavu:- Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari Maalum kwa Watoto Viziwi (wasiosikia na wasioongea)?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza kabla ya kuuliza swali la nyongeza ninaomba kutoa ufafanuzi kwamba hawaitwi wasiosikia au wasioongea kwa ujumla wao wanaitwa viziwi kwa hiyo, ni vizuri zaidi kuwa makini na haya majina ili kuepuka wakati mwingine kuonekana kwamba kwasababu neno asiyesikia ina maana ni mtu mtukutu. Asante naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwasababu tatizo hili ni kubwa maeneo mengi na kwa namna moja au nyingine wanaochagua hawazingatii kwa kujua kwamba huyu mtoto ana mahitaji pengine maalum au asiye na mahitaji maalum. Sasa je, ni lini Serikali itaweka mchakato maalum kwa kuzingatia kwamba katika kila mkoa angalau kuwepo na shule zitakazosaidia watoto wenye mahitaji maalum wakiwemo viziwi?

Swali la pili uhaba wa waalimu ambao hawana ujuzi wa kufundisha wanafunzi kwa maana kwamba wanafunzi wote wanachanganywa pamoja hata wale viziwi.

Je, sasa upi mkakati maalum wa Serikali katika kuhakikisha kwamba walimu wenye mahitaji maalum wanasambazwa katika shule zetu za msingi ili basi waweze kusaidia wanafunzi wetu hasa wenye mahitaji maalum? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunao upungufu wa shule hizi katika maeneo mbalimbali ya nchi na kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi tumeanza na hizo na kuna baadhi ya maeneo kuna shule zingine uwezo wa Serikali ukiruhusu basi tutajenga karibu kila mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungependa hao watoto wapate huduma ya taaluma katika yao ya karibu bila kupata usumbufu ili kwasababu pia kuna kuwa na shida hata kuwatoa nyumbani na kuwapeleka hata kwenda kuwaangalia wanapata matatizo ya magonjwa na mambo mengine hiyo ndiyo shida. Lakini tunatoa wito pia kwenye jibu letu kwamba hata wale wadau ambao wanaweza wakajenga shule kama hizi tumeshuhudia shule nyingi zipo Tanzania hapa za private na za watu binafsi na wadau mbalimbali lakini nyingi zinalenga watoto hawa ambao wanauelewa wa kawaida na hawana aina yoyote ya ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tukipata mdau mwingine pia ambaye anaweza akajenga shule za aina hii za mahitaji maalum tutampa support kama Serikali ili shule iweze kufunguliwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia swali lake la msingi anaulizia kama kuna namna ya kuweza kupeleka walimu katika kila mahali. Ni kweli kwamba kuna upungufu lakini kila tunapokuwa na ajira ya walimu tunazingatia pia walimu wa mahitaji maalum. Na swali lake anapozungumza hapa kwamba tusaidiane pia namna ya kutambua watoto katika kila eneo ilitokea pia kwamba tunatoa taarifa kuwatambua watoto hao katika maeneo yao lakini pia maeneo mengine wanafichwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitumie fursa kuwaomba pia Waheshimiwa Wabunge na watanzania wote inapotokea kuna mwanafunzi wenye ulemavu katika eneo hilo lakini pia tukasema hawa watoto ukiwatenga wenyewe wenyewe pia imekuja hoja inaitwa elimu jumuishi ili watoto hawa waanze kuzoeana wanasaidiana ili hata mtoto akizaliwa katika jamii yetu kwenye familia ni mlemavu asitengwe hiyo ni nia ya Serikali tuwe na elimu jumuishi lakini wanapokuwa na ulemavu mkubwa zaidi wanapata mahitaji mahsusi na usimamizi mahsusi ili waweze kupata huduma vizuri sana. Ahsante!

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE (MHE. AMINA S. MOLLEL) aliuliza:- Shule ya Viziwi Mwanga hutoa Elimu ya Msingi kwa Watoto wasiosikia na wasioongea kwa Mikoa ya Kilimanjaro, Tanga na Arusha; wanapohitimu Elimu ya Msingi, Wanafunzi hao hujiunga na Shule za Sekondari za kawaida ambazo hazina Walimu wenye Taaluma Maalum, vifaa na mazingira rafiki kwa Watoto wenye ulemavu:- Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari Maalum kwa Watoto Viziwi (wasiosikia na wasioongea)?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kuniona sambamba na majibu mazuri yaliyotolewa na Serikali wilayani Moshi Vijijini kuna shule ya viziwi ya Vona wamejitahidi kwa muda mrefu sana kupata ushirikiano na Serikali lakini imeshindikana. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kufuatana na mimi mpaka Vona ili aone ni jinsi gani Serikali itaisaidia shule hiyo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo tayari sana kuambatana na mwalimu tukatembelee watoto wetu hao wazuri tukaone mazingira hayo na ni kuhakikishie Mheshimiwa Mbunge huo ushirikiano uliokosekana sasa utapatikana. Ahsante sana.