Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kata hizi alizozitaja Mheshimiwa Dkt. David Mathayo ni Kata ambazo ziko kwenye milima mirefu. Naomba nimkumbushe Mheshimiwa Waziri kwamba alikuja Same Mheshimiwa Dkt. Mathayo akaingia kwenye gari yake na mimi nikaingia kwenye gari yake tukazizungukia kata hizi zote ambazo zimetajwa hapa na Kata ya Vuje, kata ya Bombo, Kata ya Mtina kata ya Lugulu.

Mheshimiwa Waziri uliona hali halisi ya kata hizi kwamba ni korofi mno hazina mawasiliano ya uhakika pamoja na mawasiliano ya Barabara, Mheshimiwa Waziri unakuja na mikakati gani sasa ya kuhakikisha hizi kata ambazo ziko milimani zinaondoka na matatizo haya ahsante Mheshimiwa.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza uniruhusu tu nitoe shukrani kwamba nilivyofanya ziara katika maeneo haya nilipata ushirikiano wa hali ya juu sana kwa Mheshimiwa Mbunge lakini pia kwa viongozi wa wilaya, kwa hiyo nakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na niseme tu yapo maeneo mbalimbali ambayo yanakuwa na changamoto kutokana na hali ya jiografia, eneo la Same hili linamilima lakini yapo maeneo mengine ambayo yana misitu ambayo hii ni vikwazo kwa mawasiliano kwa hiyo utaona changamoto ya mawasiliano imekuwa kubwa katika eneo hili kwa sababu ya hali ya jiografia kwa maana hiyo milima na misitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tumejipanga kama Serikali ndiyo maana utaona katika awamu ya nne tuko kwenye hatua ya manunuzi, tutaendelea kuweka hiyo minara ambayo imetajwa na katika eneo hili tutakuwa na kata tano vijiji kumi na tatu na baada kusimika hiyo minara tutafanya tadhimini kuona maeneo yapi kutokana na geografia ambayo yatakuwa hayajapata tena mawasiliano kwahiyo hizi changamoto tunaendelea kuziondoa tunavyokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge mkakati mkumbwa uliokuwepo ni kuhakikisha kwamba tunaweka maeneo haya katika mipango yetu kupitia mfuko wa mawasiliano kwa wote. Lakini pia tunaweka bajeti ya kutosha tunavyokwenda ili sasa tuhakikishe kwamba baadaye tunamaliza changamoto ya mawasiliano katika eneo hili lakini unafahamu pia tunaendelea kufanya usanifu mkubwa katika barabara kutoka Same kwenda Mkomazi lakini tutakwenda mkinga kule tumejipanga ili tuondolee shida wananchi wa maeneo haya ambayo hali ya geografia inawaathiri sana kwa maana ya usafiri wa barabara hali ni mbaya lakini pia upande wa mawasiliano ahsante sana.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza, Mheshimiwa Waziri nimekuwa nikiuliza mara nyingi katika Bunge hili vijiji vya Imbilili, Imiti na Chemchem kwamba havina mawasiliano na nimekuwa nikipatiwa majibu ya Serikali kwamba dawa ya tatizo hili ni kuongezea nguvu minara ya Voda na Airtel, lakini kazi hii haifanyiki naomba nifahamu ni lini sasa kazi hii itafanyika ili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata mawasiliano.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, nampongeza sana Mbunge kwa sababu tumeongea mara nyingi sana kuhusu changamoto za jimbo lake Mheshimiwa Mbunge na sisi tumejipanga. Kama nilivyozungumza juzi kwamba katika mradi huu wa Awamu ya IV ya kupunguza changamoto ya mawasiliano tunazo kata mia tano 21 na vijiji 1222 ambavyo viko kwenye mpango. Nimuombe tu Mheshimiwa Gekul kwa sababu kile kijitabu ninacho hapo baadaye tuwasiliane ili tupitie kwa pamoja uweze kuona namna tulivyojipanga kutatua changamoto za mawasiliano katika eneo la kwako na tutaendelea kufanya hivyo mpaka wananchi waweze kuwasiliana vizuri katika maeneo yao ahsante.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 3

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana mwaka 2016 Serikali ilituambia sisi Wabunge tuweze kuorodhesha maeneo yote ambayo hayana mawasiliano Wabunge tulifanya hivyo na tena mwaka huu Serikali ikatuambia tuweze kufanya hivyo tena, na mimi baadhi ya maeneo yangu kwa mfano kata ya Halungu, Kata Nambizo, Bara Magamba, Itaka na maeneo mengine hayana mawasiliano ya simu. Je, ni lini Serikali sasa itapeleka mawasiliano ya simu katika maeneo hayo ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Jimbo la Mbozi?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, niseme tu kama nilivyozungumza, tumekuwa tukiwasiliana na Waheshimiwa Wabunge vizuri ili kutatua tatizo la changamoto ya mawasiliano katika maeneo mbalimbali. Na kupitia huu utaratibu ambao tunaufanya kupata maoni na ushauri wa Wabunge ndiyo maana katika Awamu ya IV tumekuja na orodha kubwa sana ambayo tunaendelea kutatua matatizo yaliyokuwa maeneo yetu, vijiji 1222, ni vijiji vingi sana lakini kupitia kwenye awamu zilizopita tumeendelea kufanya hivi ninavyozungumza iko miradi mingine ambayo inaendelea wakati tutakuja na awamu nyingine ya nne. Kwa hiyo, Mheshimiwa Haonga nikutoe hofu tu kwamba ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba suala la mawasiliano litakuwa kwa wote kama tulivyoanzisha mfuko na nishukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru Bunge lako kuanzisha Mfuko wa mawasiliano kwa wote umekuwepo kwa miaka kumi na kazi kubwa sana imefanyika ili kuhakikisha mawasiliano yanakuwa bora katika maeneo ya nchi yetu.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 4

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi napongeza sana Serikali kwa hatua zake za kusambaza na kusimamia mawasiliano pamoja na kujenga minara sehemu zote. Pamoja na hayo nataka niulize Serikali ina mikakati gani na ya haraka kwa kiasi gani katika kudhibiti au kuimarisha kikosi kazi cha kupambana na hawa wahuni kila siku wanaosumbua wananchi katika kuwaibia pesa zao kupitia mtandaoni kwa kuwaambia tuma hela hii kwa namba hi, tuma hela hii kwa namba hii, Serikali inafanya nini kuwadhibiti wahuni hawa?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, ipo mikakati mingi ya kupambana na hali hii ambayo inajitokeza kwa sababu ya ukuwaji wa teknolojia pia changamoto nazo zinakuwa zipo nyingi, tunao mkakati kwanza wa kuelimisha wananchi ili kuwaokoa na hii hali ambayo inajitokeza lakini pia mara kwa mara mnaona tunaendelea kuboresha Sheria na Kanuni hata hili zoezi la uandikishaji wananchi kwa kupitia alama za vidole kufanya usajili wa simu ni hatua hizo madhubuti za kuhakikisha tutaendelea kumbambana nah ii changamoto ambayo ipo. Kwa hiyo, ni kuahakikishie tu kwamba kila wakati changamoto inapojitokeza kama sisi Serikali tunachukuwa hatua hii kuwafanya wananchi wetu kuwa salama.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 5

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, changamoto ya mawasiliano iliyopo Same Magharibi inafanana kabisa na changamoto iliyopo Singida Magharibi. Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano katika maeneo ya Iyumbu, Ingombwe, Mtunduru, Sepuka, Mwaru, Ingriasoni, na Irisia ili kuhakikisha kwamba wananchi wa maeneo hayo hawaachwi nyuma na mawasiliano ya simu za mkononi? Nakushukuru sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kama nilivyozungumza kwamba maeneo nchi nzima tunafanya juhudi za kuhakikisha kwamba tunaboresha mawasiliano na iko orodha ndefu tu katika Mkoa wa Singida. Nimsihi tu Mheshimiwa Aysharose Matembe na nimpongeze sana kwa kweli hata nilivyofanya ziara Singida nilipokea orodha ndefu sana kwa ajili ya kuboresha mawasiliano katika mkoa huu. Kwa hiyo, nikuombe tuonane tu ili tuweze kupitia hii orodha ili ufanye kazi ya kuwaelimisha wananchi kwamba Serikali inajipanga mwaka huu wa fedha kuna kazi kubwa itafanyika kwa ajili ya kuendeleza kuboresha…

MWENYEKITI: Ahsante

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 6

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza Kijiji cha Misiaje kilichopo katika Kata ya Malumba na Kijiji cha Imani na Kaza moyo kilichopo Kata ya Lukumbule havina mawasiliano. Je, ni lini Serikali itajenga minara katika vijiji hivyo ili kuwapa mawasiliano wananchi hao?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naompongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu nilivyofanya ziara Mkoani Ruvuma tulikuwa na mawasiliano mazuri sana kulikuwa na changamoto nyingi sana na hasa hasa maeneo haya ambayo yapo mpakani. Kwa hiyo, nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge avute subira kama nilivyosema tunaorodha ndefu sana, aje tu tupitie kwa pamoja halafu tutakapoweka minara hii katika maeneo ambayo yameainishwa tutaangalia tena tuone kama kuna maeneo bado yanachangamoto Serikali itakuwa ipo tayari kuendelea kupunguza tatizo ambalo lipo katika maeneo yetu.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 7

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nimekuwa nayataja maeneo kadhaa ambayo yapo jimbo la Mtwara mjini kwa muda mrefu ndani ya Bunge hili na maeneo hayo, Naulongo, Mkunjanguo, Namayanga, na Mbawala Chini ambapo hakuna mawasiliano ya simu kabisa. Nilikuwa naomba commitment ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba ni lini atafanya ziara ya Mtwara Mjini kuja kukagua mguu kwa mguu maeneo haya ili aweze kudhibitisha kwamba maeneo haya yanahitaji mawasiliano kwa simu?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anaomba nifanye ziara katika Mkoa wa Mtwara na sisi unafahamu Mheshimiwa Mbunge tuna miradi mingi sana ambayo Wizara yangu inasimamia, nitafanya ziara mapema baada ya Bunge hili katika Mkoa huu wa Mtwara.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 8

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza Kijiji cha Yaeda Chini, Masieda, Endamilay na Mbullu Vijijini wamesaini mikataba ya kujenga minara TTCL na Holotel wameondoka. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri watarudi hawa TTCL kujenga minara Mbullu Vijijini?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu TTCL wamepewa kandarasi ya kujenga minara maeneo mbalimbali. Tatizo au changamoto ambayo ilikuwepo kidogo ni kwamba TTCL wanavyopewa kazi sambamba na wakandarasi wengine kwa maana hawa Tigo, Airtel, Vodacom kidogo tumekwenda kusuasua, siyo kusuasua kwa sababu wenyewe sasa kama taasisi ya Serikali lazima wafuate Sheria ya Manunuzi ambayo imetuchelewesha kwenda kusimika minara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, hatua za manunuzi ziko vizuri kwa maana TTCL watakuja katika eneo lake na kusimika ile minara ambayo wamepewa fedha na Mfuko wa Mawasiliano. Kwa hiyo, avute tu subira wanakuja na tutaweka hiyo minara kuongeza mawasiliano katika eneo lake.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 9

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo ya usikivu wa simu yaliyopo Same Magharibi ni sawa na matatizo yaliyopo katika Wilaya ya Ngara, Kata za Keza, Mganza, Mrusagamba, Mgoma, Kabanga na Rusumo, ambapo yanaingiliana na nchi jirani za Rwanda na Burundi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha usikivu wa mawasiliano katika kata hizi?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia maendeleo katika eneo lake. Niseme tu maeneo ya mipakani yanazo changamoto za kuingiliana kwa mawasiliano. Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote jambo hili tumeshalitambua na tuna mkakati wa kuwasiliana na wenzetu nchi za jirani kwa sababu upo utaratibu ambao tunajiwekea kwamba ile minara iwekwe umbali fulani ili ipunguze changamoto hii ya kuingiliana kwenye mawasiliano. Pia, tunaendelea kusimika minara katika maeneo haya ya mipakani ili kuhakikisha wananchi wetu wa maeneo hayo hawapati changamoto hii ya kuingiliana kwa mawasiliano.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 10

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Yapo mawasiliano hafifu katika Kijiji cha Kamnyazia, Kata ya Lusaka, Vitongiji vya Mpande. Halotel walishajenga foundation toka mwaka jana mwezi Agosti hawajaonekana. Ni lini sasa watakwenda kumalizia kazi ile ili wananchi waweze kupata huduma?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Malocha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wameuliza maswali mengi sana kuonesha kwamba tunazo changamoto kubwa za minara katika maeneo yetu. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge swali hili alilouliza kuhusu mnara wa Halotel nilichukue tu kama suala mahsusi ili tuweze kujua nini kilichotokea ili tuweze kuliondoa tatizo hilo na hatimaye mnara huu uweze kukamilishwa. Ahsante sana.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA (K.n.y. MHE. DAVID M. DAVID) aliuliza:- Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Simu itawapelekea huduma ya simu wananchi wa Kata za Msindo Mshewa, Mhezi, Vumari, Vudee, Tae, Suji, Gavao, Saweni na Ruvu Jiungeni?

Supplementary Question 11

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Katika Jimbo langu la Nkasi Kusini kuna Vijiji sita vya Kisambala, Ng’undwe, Mlalambo, Kasapa na Izinga, mara nyingi nimepeleka orodha Wizarani ili vipatiwe mawasiliano. Je, ni lini Serikali itavipatia mawasiliano vijiji hivi? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu changamoto zilizoko katika maeneo haya sababu ya jiografia yake, naona ndiyo maana amekaa na jirani yake pale Mheshimiwa Malocha. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba eneo hili ambalo analizungumzia tutaweka msukumo wa kipekee ili tuone changamoto hizi zinakaa vizuri kwa sababu nafahamu kwamba kuna changamoto nyingi sana kwenye eneo lake, kwa hiyo, avute subira. Pia, naomba tuonane na Mheshimiwa Mbunge ili aweze kuona kwenye orodha namna ambavyo tumejipanga ili aweze kwenda kusema kwa wananchi kwamba Serikali hii imejipanga kuhakikisha kweli mawasiliano yanakuwa mawasiliano kwa wote.