Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER A. BULAYA aliuliza:- Jimbo la Bunda Mjini limekuwa likikumbwa na adha ya ukosefu wa maji safi na salama na Serikali imekuwa ikikwamisha mradi wa maji safi na salama Bunda kwa muda sasa kushindwa kutoa fedha za utekelezaji:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha, ili mkandarasi aweze kukamilisha mradi huo?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba niulize maswali yangu mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri na Mheshimiwa Spika wewe ni shahidi, huu mradi ni wa muda mrefu sana zaidi ya miaka 11. Miaka mitatu mizima tunazungumzia suala la chujio, si sawa kwa wananchi wa Bunda na Mkoa wa Mara. Naomba niulize maswali yangu mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, mbali na changamoto za wakandarasi kutokulipwa, mbali na changamoto za wakandarasi kuondoka site, Mamlaka ya Maji ya Mji wa Bunda kupitia vyanzo vyake vya ndani vimeanza kusambaza mitandao ya maji. Sasa nilitaka kujua Serikali mna mkakati gani wa kusaidia jitihada hizi za mamlaka ya maji Mji wa Bunda mbali na kwamba, haipati ruzuku Serikalini, kuendelea na zoezi la usambazaji wa miundombinu ya maji katika maeneo mbalimbali ikiwepo Manyamanyama, Bunda Store, Gerezani, Olimpas, Sazila; Serikali lini mtahakikisha hii mitandao ya maji yanafika kwenye maeneo hayo ambayo hakuna kabisa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri unajua Mamlaka ya Mji wa Bunda, Halmashauri yetu ya Mji wa Bunda ni Mpya. Tumekuta kuna madeni ya umeme ambayo mwisho wa siku takribani milioni 603 hayo tumerithi. Mamlaka yangu ya Mji wa Bunda inalipa bili current bili inalipwa, lakini haya madeni yamerithiwa kupitia halmashauri iliyopita tangu Mzee wangu Wassira. Wizara mna mkakati gani kuhakikisha hli deni linalipwa, ili umeme usikatwe wananchi waweze kupata huduma ya maji maana wao ndio wanaoathirika na bili inalipwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, cha kwanza nataka nikiri kwamba, moja ya changamoto kweli tuliyokuwanayo ilikuwa wakandarasi wababaishaji, lakini uanzishwaji wa RUWASA mmekwishatupa rungu sisi viongozi wa Wizara ya Maji, hatuna sababu hata moja ya kulalamika. Tutachukua hatua kwa mkandarasi yeyote ambaye atataka kutuchelewesha katika kukamilisha miradi yetu ya maji.

Mheshimiwa Spika, kikubwa kutokana na mradi ule Mheshimiwa Waziri amekwishatoa agizo kwamba, mradi ule sasa tutatekeleza kupitia wataalam wetu wa ndani katika kuhakikisha tunawapa uwezo Mamlaka ile ya Bunda kwamba, tutatoa milioni 375 na wataalam wetu wa ndani wataukamilisha mradi ule kwa haraka. Na kazi iliyobaki ni wataalam wetu wa mamlaka sasa kuwaunganishia wateja wao, ili waweze kupata huduma hii ya maji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala zima la ukatikaji wa umeme na madeni yaliyopo, hii ni Grade C mamlaka yao. Sisi kama Wizara yetu ya maji tumeona haja sasa ya wao kulipa kidogo na sisi tuweze kuwaongezea ili katika kuhakikisha tunakamilisha deni lile na wananchi wa Bunda waendelee kupata huduma ya maji. Pia natambua kwa Mheshimiwa Kangi Lugola kukamilika kwa mradi huu maeneo ya vijiji jirani kwa maana ya Buzingwe, Bulamba na Kabainja nao watapata huduma ya maji. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Esther Bulaya kukamilika kwa mradi huu utafanya maamuzi sahihi sasa ya kurudi nyumbani, ahsante sana.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ESTHER A. BULAYA aliuliza:- Jimbo la Bunda Mjini limekuwa likikumbwa na adha ya ukosefu wa maji safi na salama na Serikali imekuwa ikikwamisha mradi wa maji safi na salama Bunda kwa muda sasa kushindwa kutoa fedha za utekelezaji:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha, ili mkandarasi aweze kukamilisha mradi huo?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa niwashukuru Wizara ya Maji kwa sasa kwa kweli tuseme ukweli kwamba, viongozi wote Mawaziri, Makatibu na watendaji wote sasa wako kazini, wanafanya kazi vizuri, niwashukuru sana. Katika Jimbo la Bunda wataalam walifanya tathmini ya kuchimba visima vya maji ikaonekana kwamba, visima vinakauka, Wizara ikaja na mkakati wa kuchimba malambo zaidi ya malambo 16 ambayo ni matumizi ya maji, sasa kwa mwaka huu wamechagua kuchimba malambo matano. Nilitaka kuuliza tu Waziri, ni lini sasa haya malambo matano yatafanyiwa kazi? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kiukweli anafanya kazi kubwa sana. Jana tu tulikuwepo nae katika Wizara yetu ya maji na Katibu Mkuu na moja ya makubaliano ni katika kuhakikisha tunatia fedha kwa ajili ya uchimbaji wa mabwawa zaidi ya matano. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nataka nikuhakikishie sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo kwa Wananchi wako wa Bunda Vijijini kuweza kuchimbiwa mabwawa haya na waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, pia, nitumie nafasi hii kuwapongeza Wabunge wa Mkoa wa Mara wanaotokana na Chama cha Mapinduzi kwa mshikamano wao na kuweza kupigana. Zaidi ya miradi Mgango, Kyabakari tumekwishasaini, lakini tunakwenda kutatua tatizo la maji Mugumu pamoja na Tarime. Ahsante sana.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ESTHER A. BULAYA aliuliza:- Jimbo la Bunda Mjini limekuwa likikumbwa na adha ya ukosefu wa maji safi na salama na Serikali imekuwa ikikwamisha mradi wa maji safi na salama Bunda kwa muda sasa kushindwa kutoa fedha za utekelezaji:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha, ili mkandarasi aweze kukamilisha mradi huo?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, ahsante ningependa kuuliza swali moja la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Vijijini tumechimbiwa visima 11 na kati ya visima hivyo, visima vitatu tayari Serikali imeridhia mchakato wa kutafuta mkandarasi uanze.

Je, ni lini Serikali itaridhia na visima vinane vilivyobaki navyo mchakato wa kutafuta mkandarasi uanze, ili huduma ya upatikanaji wa maji Jimbo la Mtwara Vijijini iboreke?

SPIKA: Majibu ya swali hilo Mheshimiwa Naibu Waziri Maji, tafadhali.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, lakini la kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, mama yangu Hawa, kwa kazi kubwa anayofanya katika jimbo lake, lakini kikubwa nimuagize Mhandisi wa Mkoa kwa maana ya Meneja wa RUWASA katika kuhakikisha analifuatilia hili jambo na ahakikishe lianze kwa haraka. Na sisi kama Wizara ya Maji tupo tayari kuwapa msaada, ili mradi huu uanze kuwaka kwa wakati.