Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza Madaktari Bingwa nchini?

Supplementary Question 1

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, asilimia kubwa ya wananchi wetu kipato chao ni cha chini na wamekuwa wakitegemea hpspitali zetu za Serikali kama msaada mkubwa pindi wanapopata changamoto za afya. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba, hawa madktari bingwa wachache ambao tunao hawapati vishawishi vya kwenda kufanya kazi nje ya nchi ama kwenye private hospitals?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ukiangalia idadi ya madaktari bingwa ambao tunao bado ni chache sana, lakini hospitali nyingi za mikoa hazina madaktari bingwa. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha madaktari hawa wanagawiwa kwa uwiano mzuri, ili kuepusha usumbufu wa Wananchi wengi kutoka mikoani na kufuata huduma Hospitali ya Muhimbili? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, naomba nilitaarifu Bunge lako kwamba, katika nchi ambazo tumejaliwa kidogo kwamba, madaktari wetu hawatoki sana kwenda nje ya nchi kulinganisha na nchi nyingine katika Bara la Afrika, Tanzania ni mojawapo.

Mheshimiwa Spika, na moja ya mkakati ambao tumeuweka wa kuhamasisha madaktari wetu na wataalam wetu wa afya kuendelea kukaa nchini ni maboresho ambayo tunaendelea kuyafanya katika sekta ya afya; vituo zaidi ya 352 tumeviboresha, hospitali za wilaya 67 tumejenga, sasa hivi tunaendelea na ujenzi wa hospitali za rufaa tano za mikoa na maboresho mengine makubwa ya kimiundombinu, ya vifaa, ambayo sasa hivi yamesababisha kwamba, hata huduma zile kubwa za kibingwa ambazo zilikuwa zinafanyika nje ya nchi sasa hivi zimeweza kufanyika nchini. Kwa hiyo, hili nalo limesaidia sana kuwafanya wataalam wetu wazalendo kubaki, pamoja na motisha nyingine za ndani ambazo tumeendelea kuwapatia watalaam wetu katika sekta yetu ya afya.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Sonia Magogo ameulizia suala la uwiano; ni kweli tunakiri tumekuwa na changamoto kubwa sana ya uwiano wa upatikanaji wa Madaktari Bingwa katika baadhi ya mikoa. Na hili sisi kama Wizara tumeshaliona na moja ya mkakati ambao tumeufanya sisi kama Wizara ni kuhakikisha kwamba, wataalam ambao tunaenda kuwasomesha kwa fedha ya Serikali tunachukua katika maeneo ambayo yamekuwa na uhaba mkubwa wa wataalam kwa lengo kwamba akimaliza na tumewasainisha kitu kinaitwa bonding kwamba, ukimaliza na iwapo kama umesoma na fedha za Serikali basi tutakurudisha kulekule katika maeneo ambayo ulikuwa umetoka, ili uweze kupata utaalam huo.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi hiki cha mpito ambapo huduma hizi hazijaweza kupatikana katika baadhi ya mikoa ndio tumekuwa tunaendesha kambi; Madaktari Bingwa hawa wachache tulio nao tumekuwa tunawazungusha ndani ya nchi kwa kambi maalum katika baadhi ya mikoa, ili waweze kutoa hizo huduma kwa wale Wananchi, ili angalau katika ile mikoa basi huduma zile ziweze kupatikana.