Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itatekeleza kwa ukamilifu Sera ya Afya ya kutoa huduma za afya bure kwa wanawake wajawazito, watoto chini ya miaka mitano pamoja na wazee wenye umri zaidi ya miaka 60? (b) Mwaka 2014 Serikali ilianza utaratibu wa kuwapatia wazee vitambulisho kwa ajili ya matibabu bure kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali. Je, ni Wilaya ngapi zimekamilisha zoezi hilo muhimu ili kuokoa maisha ya wazee yanayopotea kwa kukosa huduma za afya?

Supplementary Question 1

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekiri changamoto kubwaya utekelezaji wa Sera hii ya kutoa huduma bure kwa makundi haya maalum ikiwemo wajawazito, watoto chini ya miaka mitano, wazee wanaozidi umri wa miaka 60 ambao hawana uwezo lakini pia makundi ya watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hii makundi haya yanateseka sana kupata huduma maeneo mbalimbali na wengi kiukweli wanapoteza maisha. Leo maeneo ya vijijini, Wilayani huko wanaandikiwa barua kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya watembee mitaani wanaomba misaada ili waweze kutibiwa kwahiyo Serikali ione changamoto kubwa hii iliyopo.

Mheshimiwa Spika, napenda kujua, Serikali imekuja na mkakati wa kuweza kuwepo hii huduma ya kuweza kutoa bima kwa wote sasa hawajasema specific ni lini itakamilika. Wanasema mpaka mchakato wa Serikali kutoa maamuzi. Hebu muone umuhimu ni lini sasa, naomba commitment hapa Bungeni ni lini mchakato huu utakamilika ili mfuko huu uweze kuwa na fedha ya kutosha makundi haya yatibiwe yaweze kupona kwa kuwa wengi wanapoteza maisha?

Mheshimiwa Spika, lakini tangu Serikali imetoa agizo kwenye Halmashauri zetu ni miaka zita sasa na Mheshimiwa Waziri kwenye majibu yake ni asilimia 40 tu wametekeleza, kwa hiyo bado wazee wengi hawajapewa vitambulisho, hawapati huduma za fya kwenye madirisha maalum.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali, siyo kutoa tu rai, Serikali sasa naiomba leo iweze kutoa tamko hapa Bungeni, itoe deadline ni lini ambapo vitambulisho hivi vikamilike na wale Halmashauri ambazo hazijakamilika kwa wakati waweze kupewa adhabu ili wazee hawa ambao wametumikia Taifa hili wapate huduma za afya bure waweze kuishi. Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Magdalena Sakaya alitaka commitment ya Serikali kwamba ni lini utaratibu au mchakato huu wa Bima ya Afya kwa wananchi wote utakamilika; nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ifikapo Bunge la Septemba Serikali tutaleta Muswada wa Bima ya Afya kwa wananchi wote ndani ya Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Spika, lakini ameuliza swlai la pili kuhusiana na wazee na lini mchakato huu tuweze kutoa tamko; mimi naomba niseme tu kama ifuatavyo; nchi yetu sasa hivi inaendelea kupata neema na wastani wa Matanzania sasa hivi kuishi ni iaka 64 kwamba tunategemea kwamba na tunatarajia kama kila mtu atatunza afya yake vizuri tunatarajia tu kwamba atafika miaka 64, kwa hiyo umri huu unazidi kuongezeka na iddai ya watu hawa wanazidi kuongezeka ambao wanazidi miaka 60. Kwa hiyo, hatuwezi tukasema wkamba tutatoa ukomo kwamba ifikapo kesho wazee wote wa miaka 60 wawe wamepata vitambulisho.

Kwa hiyo mimi niendelee kusisitiza tu kwamba Serikali imeshatoa maagizo kwa Halmashauri zote na hili ni agizo la Serikali wanatakiwa waendelee kuwatambua wazee na waendelee kuwapatia vitambulisho wale wazee ambao hawana uwezo wa kugharamia matibabu.

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itatekeleza kwa ukamilifu Sera ya Afya ya kutoa huduma za afya bure kwa wanawake wajawazito, watoto chini ya miaka mitano pamoja na wazee wenye umri zaidi ya miaka 60? (b) Mwaka 2014 Serikali ilianza utaratibu wa kuwapatia wazee vitambulisho kwa ajili ya matibabu bure kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali. Je, ni Wilaya ngapi zimekamilisha zoezi hilo muhimu ili kuokoa maisha ya wazee yanayopotea kwa kukosa huduma za afya?

Supplementary Question 2

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli suala hili la matibabu bure limekuwa na changamoto kubwa sana mpaka kuna baadhi ya vituo na hospitali wakina Mama wajawazito wanambiwa waende na mabeseni, pamba na hata mikasi.

Je, ni lini Serikali sasa itaona umuhimu wa kuweka angalau fedha kidogo za kuchangia akina mama wajawazito ili waweze kupata huduma bora? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sera ya Afya ya mwaka 2007, huduma kwa ajili ya akina mama wajawazito ni bure na sisi kama Seriakli tumekuwa tunaendelea kuwekeza sasa hivi takribani akina mama milioni mbili wanajifugua kwa mwaka ndani ya nchi yetu na sisi kama Serikali kupitia Bajeti hii ya dawa, vifaatiba na vitendanishi tumejaribu sana kuhakikisha vifaa vya kujifungulia vinakuwepo, tumehakikisha kwamba chanjo kwa ajili ya watoto tunakuwa nazo, dawa zote za muhimu kwa maana dawa za kupunguza upungufu wa damu kwa akina mama yale madini ya iron pamoja na phera sulfate pamoja na folic acid tunakuwa nazo, dawa za kuongeza uchungu oxytocin tunakuwa nazo na dawa za kupunguza kifafa cha mimba tunakuwa nazo. Kwa hiyo, ni sehemu chache sana ambazo tunapata malalamiko kama hayo na mimi kama Naibu Waziri nimetembelea sehemu mengi sana basi ni sehemu nyingi vifaa vya kujifungulia tunavyo na sisi kama Serikali tunavyo kupitia Bohari yetu ya madawa.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itatekeleza kwa ukamilifu Sera ya Afya ya kutoa huduma za afya bure kwa wanawake wajawazito, watoto chini ya miaka mitano pamoja na wazee wenye umri zaidi ya miaka 60? (b) Mwaka 2014 Serikali ilianza utaratibu wa kuwapatia wazee vitambulisho kwa ajili ya matibabu bure kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali. Je, ni Wilaya ngapi zimekamilisha zoezi hilo muhimu ili kuokoa maisha ya wazee yanayopotea kwa kukosa huduma za afya?

Supplementary Question 3

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Same Mashariki lina tatizo kubwa sana la huduma za afya. Kituo kilichokuwa kimeitwa Kituo cha Afya Vunta kwenye Tarafa ya Mamba Vunta ilikuwa ni ghala la mazao kikapandishwa hadhi lakini hakina hadhi hata ya kuwa dispensary, Tarafa ya Gonja haina hata zahanati wala kituo cha afya cha serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka kuiomba Serikali kwamba kwa muda mrefu nimeenda kuongea na Serikali kuhusu kuboresha angalau basi Hospitali ya Gonja Bombo ambayo Serikali kupitia KKKT wanasaidia watu wa Tarafa hii ya Gonja na ya Mamba Vunta kupata huduma katika hospitali hii.

Je, ni lini Serikali itapeleka angalau Madaktari basi wakasaidie kuboresha huduma hii ili akina mama wajawazito wasife wakitembea umbali mkubwa zaidi ya kilometa 15 mpaka 30 kufuata huduma katika Tarafa ya Ndungu ambayo kituo kipo bondeni na Tarafa hizi zote kubwa ziko milimani ambapo hata barabara zetu ni mbaya sana?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha sekta ya afya ikiwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za wananchi pale ambapo wanaanzisha ujenzi wa maboma ya zahanati Serikali kupitia Halmashauri imekuwa ikichangia kukamilisha yale maboma lakini sambamba na hilo tumefanya maboresho makubwa sana ya vituo vya afya takribani kati ya vituo zaidi ya 500 ndani ya nchi yetu, zaidi ya 300 na tumeweza kuvifanyia maboresho kuweza kutoa huduma za dharura za kumtoa mtoto tumboni.

Mheshimiwa Spika, lakini sambamba na hilo, Serikali katika mwaka huu wa fedha mabao unakwisha tumejielekeza nguvu katika kujenga hospitali za Wilaya 67 na lengo ni kusogeza hizi huduma za fya karibu zaidi na wananchi.

Mheshimiwa Spika, lakini sambamba na hilo, katika maeneo ambapo hatuna Hospitali za Wilaya tumekuwa tunafanyakazi kwa karibu sana na hizi hospitali ambazo ziko katika taasisi za kidini ambazo kwa jina zimekuwa zinaitwa DDH na tumekuwa tunawapatia rasilimali fedha kwa ajili ya dawa pamoja na watumishi. Kwa hiyo, sisi tuko tayari kama Serikali tukipata maombi mahususi kuhusiana na hii Hospitali ya DDH ambayo nimekuwa nimeiongelea kama kuha hitaji la rasilimali watu tuko tayari kuweza kushirikiana nao kwa ajili ya lengo la kutoa huduma kwa wananchi wa Same Mashairiki.