Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Kondoa imewasilisha andiko la Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Kijiji cha Mongoroma, Kata ya Serya takribani miaka mitatu sasa, eneo la ekari 3,000 limetengwa kwa ajili ya mradi huo utakaonufaisha takribani wananchi 12,000. Je, ni lini Serikali italeta fedha hizo ili mradi huo uanze?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nitumie fursa hii kushukuru majibu ya Serikali sambamba na hayo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, namba moja, ni miaka tisa sasa toka tumeingiza zaidi ya milioni 143 kwenye mradi huu na hakuna ambacho kimeweza kuwa realized mpaka leo. Ukichukua faida ambazo tungezipata kwa mradi ule watu 12,000 kunufaika tungekuwa tu kwa mwaka tunapata zaidi ya bilioni 50; mpaka leo tunazungumzia miaka tisa tungekuwa tumetengeneza zaidi ya bilioni 500, ukiangalia hii opportunity cost peke yake acha multiplier effect kipindi cha uchumi wa viwanda na mazao ambayo yangetokana na matokeo yale ya pale kwenye mradi ule tungekuwa tumepiga hatua kubwa sana kwa wananchi wa Kondoa.

Je, ni lini sasa Serikali itafikia hatua ya kuweza kufanya hii tathmini ya kina na hatimaye kufanya hii tathmini ya kina na hatimaye kukamilisha mchakato mradi huu utekelezwe? la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili ili Mheshimiwa Naibu Waziri uweze kujiridhisha na fursa iliyoko kule fursa kubwa sana.

Ni lini sasa mimi na wewe na pamoja na wataalam wako tutaongozana tuende pale Mongoroma tukaone nini kinaweza kikafanyika kwa haraka zaidi? Ahsante sana.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anataka kujua kwamba huu mradi umechukua muda mrefu zaidi ya miaka tisa na hela pale tumeshawekeza ni lini sasa kwamba tumeanza kuuharakisha huu mchakato.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kwanza kumhakikisha Mheshimiwa Mbunge pamoja na kwamba sijafika katika mradi huu, lakini viongozi wetu, Wahandisi wetu wa Kanda ya Umwagiliaji Kanda ya Dodoma tayari wako kwenye mchakato wa kuufanyia tathmini ya kina ili kubaini gharama halisi za sasa badala hizi za miaka kumi iliyopita ili kuingiza katika mpango kabambe wa umwagiliaji ambao tumeuhaulisha ile Sera ya mwaka 2013 kwa hii ambayo Sera Mpya ya mwaka 2018 mradi huu pia tunaenda kuutekeleza na tathmini itafanyika haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, pili kama nilivyojibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kafumu kwamba mradi mbadala au njia mbadala ya kutekeleza miradi hii mikubwa ni kutumia Benki ya Maendeleo ya Kilimo kwa sasa hivi kwa sababu tunaondoka kwenye kilimo kile cha kujikimu tuko kwenye kilimo cha kibiashara. Kwa hiyo, lazima sasa tuwekeze ndiyo maana tumewaletea benki hii yenye riba rafiki kwa wakulima ili kuenda kuendeleza miradi mikubwa kama hii kwa sababu ile ni benki ya kimkakati.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili niko tayari baada ya bajeti yetu inayoanza kesho tarehe 17 Mei na kumalizika tarehe 20 Mei tuonane tupange ikiwezekana tarehe 21 na 22 Mei mimi na wataalam wangu tuko tayari kufika Kondoa ili kuliangalia.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Kondoa imewasilisha andiko la Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Kijiji cha Mongoroma, Kata ya Serya takribani miaka mitatu sasa, eneo la ekari 3,000 limetengwa kwa ajili ya mradi huo utakaonufaisha takribani wananchi 12,000. Je, ni lini Serikali italeta fedha hizo ili mradi huo uanze?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na yenye kuleta matumaini kuhusiana na miradi hii ya umwagiliaji. Lakini pamoja na pongezi hizo mimi naomba niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, iko miradi ya kilimo cha umwagiliaji ambayo ilikuwa inaendelea katika Mkoa wetu wa Ruvuma ikiwemo mradi wa kilimo cha umwagiliaji uliopo Legezamwendo, Misyaje na baadhi ya vijiji vingine. Miradi hii imesimama kwa ajili ya kukosa pesa na nina uhakika tayari miradi hii ilishaanza. Kuendelea kuchelewa kupeleka pesa maana yake ni kuongeza gharama za mradi.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha tunapeleka pesa katika miradi hii ili kukamilisha? Ahsante.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, nashukuru, ni kweli kwamba kuna miradi mingi ambayo imeanza kujengwa na haijamalizika mpaka sasa na labda nilitaarifu Bunge lako rasmi; baada ya Tume hii ya Taifa ya Umwagiliaji kurudi Wizara ya Kilimo tuliweza kupita katika scheme karibuni zote nchini ili kuzingalia na namna gani na wataalam wetu na hiyo pia ndani ya Serikali kama mnakumbuka siku tatu zilizopita Mheshimiwa Waziri Mkuu amewasimamisha zaidi ya Wakurugenzi saba kwa ajili ya kupisha uchunguzi tufanye tathmini ya kina kuangalia matumizi ya fedha kwa sababu pesa zilikwenda nyingi, lakini matumizi yalikuwa ni mabovu sana.

Kwa hiyo siyo kila mradi ukikwama kumalizika ni kwa sababu kwamba pesa zilikosekana, lakini baada ya hiki chombo tulichounda sasa hivi, Tume tuliyounda sasa hivi kwenda kuchunguza mapungufu hayo ya ubora wa miradi, thamani ya miradi baadae tutakuja na taarifa rasmi na kujipanga namna gani tutakwenda kumaliza mradi huu.