Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Wananchi wa Tarafa ya Mombo wamekuwa na hitaji la kuwa na skimu kubwa ya umwagiliaji katika Bonde la Mto Mkomazi na mara kadhaa viongozi wa Serikali wamekuwa wakitoa ahadi ya kukamilisha jambo hilo. Je, ni lini Serikali itatekeleza mradi wa umwagiliaji katika Bonde la Mto Mkomazi?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri alifanya ziara kwenye hili na anazungumza eneo ambalo analifahamu. Pamoja na majibu yake mazuri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza mradi huu ulibuniwa muda mrefu sana na ni mradi ambao una uwezo wa kuhudumia eneo kwa maana hekta karibu zaidi ya hekta 5000 na tathmini ambayo unasema ilifanyika ya usanifu uliofanyika ulifanyika muda mrefu.

Je, Serikali iko tayari sasa kuharakisha mapitio ya usanifu upya ili kujua gharama halisi kwa mazingira tuliyokuwanayo sasa na kwa namna ya kutekeleza mradi huu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili tunayo Skimu ya Songea na Makalala kule Magoma, lakini pia skimu ya Kwamkumbo pale Mombo ambapo wananchi wamekuwa wakiathirika wakati mvua maji yakiwa mengi yanaenda kwenye mashamba ya wakulima na kuharibu mazao na kusababisha hasara kubwa.

Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari, kuwatuma wataalam wa umwagiliaji waende kwenye maeneo haya na kuona namna ya kutatua changamoto hizi za wananchi?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anataka kufahamu Serikali kuharakisha mchakato wa kuweza kupitia upya tathmini ya mradii huu. Kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tangu siku zile nilivyofika mimi katika bonde hili na kufika bwawa lile tayari tushawaelekeza viongozi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Kanda ya Kilimanjaro wanalifanyia tathmini upya bwawa lile ili kujua gharama halisi na kuanza utekelezaji kwa mipango ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu athari ya mafuriko katika skimu hizi tatu alizozitaja za Skimu ya Songea na Makalala, kwamba nitumie nafasi hii kwanza kuwaelekeza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Kanda ya Kilimanjaro kwenda haraka katika mabwawa haya kufanya tathmini na kuona namna gani tunaweza kujenga miundombinu ile yamatuta kwa ajili ya kukinga mafuriko ya athari ya mabwawa haya.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Wananchi wa Tarafa ya Mombo wamekuwa na hitaji la kuwa na skimu kubwa ya umwagiliaji katika Bonde la Mto Mkomazi na mara kadhaa viongozi wa Serikali wamekuwa wakitoa ahadi ya kukamilisha jambo hilo. Je, ni lini Serikali itatekeleza mradi wa umwagiliaji katika Bonde la Mto Mkomazi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Spika, ahsante, bonde la Mto Manonga kama lilivyo bonde la mto Mkomazi kuna Skimu ya Umwagiliaji ya Igurubi, ambayo ilijengwa miaka ya 1980 lakini sasa hivi ilibebwa na maji wakati wa msimu wa mvua uliopita. Naiomba Serikali basi kama inaweza kwenda kuifufua hiyo skimu ili wananchi wa eneo hilo waendelee na kilimo cha mpunga, lakini pia skimu zingine ambazo za namna hiyo zilizoachwa kama kule Kibaha Vijijini na sehemu zingine ziangaliwe zote ili ziweze kufufuliwa, ahsante sana.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, nashukuru, kwanza ombi lake la kwenda kufanya ukarabati mkubwa kwenye skimu hii ya Igurubi kwanza tunalipokea, lakini nichukue nafasi hii kuwaeleza Wabunge wote skimu ziko nyingi sana katika Taifa hili, tuna eneo zaidi la hekta milioni 29 zinafaa kwa umwagiliaji na mpaka sasa miaka 58 tumeendeleza hekta 4,75,000 tu. Kwa hiyo, tukitumia au tukitegemea skimu hizi zote kuendeleza kwa kupata pesa za kibajeti tutachelewa sana, sisi kama Serikali na ndiyo maana tulianzisha benki ya mkakati ya Maendeleo Benki ya Kilimo kwa ajili ya kuendeleza miradi mikubwa hii.

Kwa hiyo sasa hivi Benki ya Maendeleo ya Kilimo itapita kila Halmashauri ambayo iliyokuwa na eneo hili la umwagiliaji kwa ajili ya skimu zingine tuziendeleze kwenye kilimo cha kibiashara kwa ajili ya kupata mikopo yenye riba nafuu ili badala ya kusubiri hela za kibajeti ili tuweze kuendeleze skimu hizi kwa muda mfupi Tanzania nzima.