Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA (K.n.y MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:- Kituo cha Afya Ujiji kinahudumia zaidi ya wakazi 20,000 lakini kituo hicho hakina mashine ya ultrasound. Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya ultrasound katika kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nipate kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa suala la ultrasound katika vituo vya afya au Hospitali za Wilaya na Halmashauri, ni suala kubwa sana na halipatikani maeneo mengi nchini Tanzania na hii inaathiri kina mama na wanaokwenda katika Hospitali hizo kuangalia hali zao za kiafya hasa katika suala la tumbo.

Je, ni lini sasa Serikali itaweka mkakati kupeleka ultrasound kwenye vituo vyote vya afya nchini Tanzania na Hospitali za Wilaya ili wanawake wapate huduma hizo katika hospitali nchini?

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Mlimba, Kituo cha Afya cha Mlimba kina ultrasound na mfuko wa Jimbo nilichukua nafasi mimi kumpeleka kwa kuomba na DMO kwenda kumsomesha mtaalam ambaye amesharudi na huduma hii inapatikana Kituo cha Afya cha Mlimba, lakini kuna Kituo cha Afya cha Mchombe, hakina ultrasound.

Je, nini kauli ya Serikali kupeleka ultrasound katika Kituo cha Afya cha Mchombe, ndani ya Jimbo la Mlimba?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, nakubaliana kabisa na Serikali inatambua umuhimu wa uwepo wa kifaa cha ultrasound na ndiyo maana katika vituo vyote vya afya ambavyo tunavijenga, tayari fedha tulishapeleka MSD kwa ajili ya kuhakikisha kwamba kituo cha afya vinavyokamilika vinakuwa na vifaa ikiwa pamoja na ultrasound.

Mheshimiwa Spika, na kwa mfano, katika swali la msingi la Kituo cha Afya cha Ujiji, tayari fedha imepelekwa na fedha hiyo imepelekwa tarehe 29 Aprili uliopita na baada ya wiki tatu, katikati ya mwezi Juni, tayari ultrasound itakuwa imefika.

Mheshimiwa Spika, lakini katika swali lake la pili, hicho kituo cha afya ambacho anakisema cha Mchome, naamini ni miongoni mwa vituo vya afya ambavyo tayari tumeshapeleka fedha MSD, kwa hiyo, tukishamaliza kipindi cha maswali na majibu, ni vizuri tukakutana na Mheshimiwa Mbunge ili tutazame wao lini wanatarajia kupata ultrasound.

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA (K.n.y MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:- Kituo cha Afya Ujiji kinahudumia zaidi ya wakazi 20,000 lakini kituo hicho hakina mashine ya ultrasound. Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya ultrasound katika kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi, Kituo cha Afya cha Pasua kilichopo Manispaa ya Moshi nacho kina tatizo la ultrasound, lakini pamoja na mortuary. Je, ni lini Serikali itapeleka ultrasound na kujenga hicho chumba cha kuhifadhindugu zetu waliotangulia mbele ya haki?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetoa majibu katika swali la msingi, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo vituo vya afya vinajengwa, vinakuwa ni vituo vya afya ambavyo vinakamilika kwa maana ya kuwa na watalaamu lakini pia kuwa na vifaa vya kutosha.

Mheshimiwa Spika, sasa katika swali lake anaongelea Kituo cha Afya ambacho kinaitwa Pasua kiko Moshi na anasema kuna haja ya kuwepo mortuary lakini pia na uwepo wa ultrasound. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hakuna kituo cha afya hata kimoja ambacho tungependa kikawa kituo cha afya nusu, tungependa vituo vya afya vyote vikamilike, ni vizuri tukaelezana tatizo ni nini na hasa ukizingatia kwamba, hata kwa Halmashauri ya Moshi, mapato yake ya ndani yapo ya kutosha kabisa. Kwa hiyo, ni suala tu la mipango tujue nini kifanyike kwa haraka ili wananchi waweze kupata huduma hizo.