Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza mpango kabambe wa kusambaza umeme vijijini chini ya mpango wa REA:- (a) Je, ni lini vijiji vyote 70 vya Wilaya ya Mkalama vitapata umeme wa REA II? (b) Je, Serikali ipo tayari kuweka umeme katika vitongoji vinavyopitiwa na njia ya umeme wa REA?

Supplementary Question 1

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa tena nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Namshukuru Naibu Waziri alishafika maeneo hayo na kesho Mheshimiwa Waziri atakuwa yuko Mkalama kwa suala hili hili.

Maswali mawili ya nyongeza; katika suala zima la mradi wa ujazilizi hasa katika vijiji vya Iguguno, Kinyangiri, Nduguti, Gumanga, Iyambi, Nkalakala, wananchi wameshaelimishwa? Kwa sababu wananchi wanalalamika. Sasa REA wamechukua hatua gani kuwaelimisha wananchi kwamba ujazilizi unakuja?

Swali la pili. Ziko sehemu ambazo umeme umeshawaka, lakini kumekuwa na maeneo ambayo yamerukwa na Naibu Waziri anafahamu na alifika. Ni lini umeme utawaka kwenye Kanisa la TAG Ibaga, Mkalama Kituo cha Afya, Matongo, Kijiji cha Kidi na Kitongoji kimoja cha Gumanga?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana kwa kazi nzuri anayoifanya. Ni kweli tuliambatana pamoja katika maeneo ya Nkito kama ambavyo nimeyataja katika swali langu la msingi, Ibaga na tukawasha umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maswali yake mawili, ameulizia mradi wa ujazilizi. Kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, ni kwamba Mradi wa Ujasilizi awamu ya pili unaanza Julai, 2019 kwa gharama za shilingi bilioni 197 kwa mikoa tisa ikiwemo Singida Tabora, Shinyanga, Dodoma, Kilimanjaro, Tanga, Pwani na maeneo mengine.

Kwa hiyo nataka nimthibitishie katika huu ujazilizi ya awamu ya pili katika Vijiji alivyovitaja ikiwemo cha Iguguno na Ibagala vitapatiwa umeme na nataka niielekeze REA pamoja na TANESCO ifanye uhamasishaji katika maeneo haya na kwamba TANESCO Mkoa wa Singida ijipange sasa kwa ajili ya vitongoji vyote ambavyo vinatakiwa viingie katika mradi wa ujazilizi, awamu ya pili, mzunguko wa kwanza na mikoa mingine 16 itapatiwa mradi wa ujazilizi, awamu ya pili, mzunguko wa pili, ambao utagharimu zaidi ya bilioni 460 na mazungumzo yanaendelea na Serikali ya Ufarasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ameuliza katika maeneo Mbaga na Mkalama kikiwemo na kituo cha afya, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa katika Wilaya ya Mkalama kwa mradi wa REA awamu ya tatu imegusa vijiji 30 na mradi wa REA awamu ya kwanza vilikuwa vijiji 14 na kwa kuwa wilaya yake ina vijiji takribani 70, ni wazi vijiji 26 vitaingia katika rea awamu ya tatu, mzunguko wa pili ambao pia unaanza sambamba mwezi Julai, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi inayoendelea sasa hivi katika Wakala wa Nishati Vijijini ni kuandaa makabrasha kwa ajili ya kutangaza zabuni na kuwapata wakandarasi wa kuanza mradi huu ili iwezeshe nchi yetu ifikapo 2020/2021 Juni, tuwe tumemaliza vijiji vyote nchini ambavyo havikuwa na umeme. Ahsante sana.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza mpango kabambe wa kusambaza umeme vijijini chini ya mpango wa REA:- (a) Je, ni lini vijiji vyote 70 vya Wilaya ya Mkalama vitapata umeme wa REA II? (b) Je, Serikali ipo tayari kuweka umeme katika vitongoji vinavyopitiwa na njia ya umeme wa REA?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Lumuma inayotoka Wilaya ya Kilosa ni mashuhuri sana kwa kilimo cha vitunguu, lakini kata hii haina umeme na inategemea umeme kutoka Wilaya ya Mpwapwa ambayo ipo kwenye mkoa mwingine wa Dodoma. Je, kata hii ni lini itapatiwa huduma ya umeme ili iweze kupata huduma ya umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mama yangu Dkt. Christine Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naye pia naomba nimpongeze kwa kufanya kazi nzuri kama Wabunge wengine wa Viti Maalum kufuatilia sekta mbalimbali. Katika swali lake hili la nyongeza ameuliza hii Kata ya Lumuma ambayo ipo jirani kabisa na Wilaya ya Mpwapwa nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge hata Diwani wa Kata ile mwanamama amekuwa akifuatilia na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kilosa naye nataka nimtaarifu Mheshimiwa na wananchi wote wa Kata ya Lumuma kwamba, tunatambua changamoto hii na kwa kuwa wapo karibu na Wilaya ya Mpwapwa tumeiagiza TANESCO, yapo maeneo tumeamua kuwapa TANESCO ili wasambaze umeme vijijini na mpaka sasa zaidi ya maeneo 200 yametwaliwa na TANESCO ili isaidie REA katika kusambaza umeme vijiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi mama Mheshimiwa Dkt. Ishengoma tutaambatana katika ziara kwenye kata hii ya Lumuma kuelezea ujumbe huu pamoja na TANESCO na REA na kwamba watapatiwa umeme katika nyakati za kuanzia mwezi Julai, 2019 na kuendelea. Ahsante sana.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza mpango kabambe wa kusambaza umeme vijijini chini ya mpango wa REA:- (a) Je, ni lini vijiji vyote 70 vya Wilaya ya Mkalama vitapata umeme wa REA II? (b) Je, Serikali ipo tayari kuweka umeme katika vitongoji vinavyopitiwa na njia ya umeme wa REA?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Nimeongea na Waziri mara nyingi na akaniahidi kwamba kwenye mradi wa REA ambao sasa hivi upo field kwenye Kata ya Idete, Shule ya Sekondari Matundu Hill na Shule ya Sekondari Kamwene ambapo mradi unapita pembeni kidogo anasema maeneo haya ni muhimu kupeleka, lakini mpaka leo hakuna jitihada za Serikali.

Je, ni lini sasa Shule ya Sekondari Matundu Hill Idete na Shule ya Sekondari Kamwene watapatiwa umeme ili wanafunzi wa sekondari waweze kujisomea na kupata ufaulu mzuri?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nijibu swali la Mheshimiwa Kiwanga Susan kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru kwa swali lake zuri, nami nimewahi kufika Idete; katika Idete pale ikiwemo Gereza la Idete limeunganishiwa umeme kwa kutumia ile umeme wa low cost design. Kwa hiyo nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ahadi ya Mheshimiwa Waziri na hapa nitoe malekezo kwa Shule za Sekondari Kamwene na Matundu Hill Idete nimwagize mkandarasi State Grid wa Mkoa wa Morogoro atekeleze maagizo ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, agizo hili sio kwa mkandarasi wa Morogoro peke yake na wakandarasi wote nchi nzima, watekeleze agizo la Serikali la kuhakikisha wanapofikisha umeme katika maeneo mbalimbali kama pana taasisi za umma iwe kituo cha afya, iwe mradi wa maji, iwe sekondari waunganishe. Tuliwaeleza variation ya namna hiyo inakubalika na Serikali hii ya Awamu ya Tano haiwezi kushindwa kulipa gharama kama inagharimu mradi mzima wa REA awamu ya tatu zaidi ya takribani trioni moja na bilioni mia moja. Kwa hiyo, nawaomba wakandarasi watii maelekezo ya Serikali. Ahsante sana.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza mpango kabambe wa kusambaza umeme vijijini chini ya mpango wa REA:- (a) Je, ni lini vijiji vyote 70 vya Wilaya ya Mkalama vitapata umeme wa REA II? (b) Je, Serikali ipo tayari kuweka umeme katika vitongoji vinavyopitiwa na njia ya umeme wa REA?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tarehe 10 Agosti, 2018, Waziri wa Nishati alizindua mradi wa REA III katika Mkoa wa Kigoma katika Kijiji cha Lusesa, Kata ya Lusesa na akaahidi kwamba baada ya mwezi mmoja umeme utawaka katika kata hiyo na viunga vyake vinavyozunguka kata hiyo, lakini mpaka leo umeme haujawaka. Nataka nijue ni lini Serikali itaagiza wanaohusika na umeme waweze kuwasha umeme katika kata hiyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Josephine Genzabuke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze kwa kweli kwa kazi kama Mbunge wa Viti Maalum kufuatilia masuala ya sekta ya nishati mkoani kwake. lakini kama ambavyo amesema uzinduzi katika Kata ya Lusesa ulifanyika mwaka 2018 mwezi Agosti, ni wazi kabisa kulikuwa na changamoto ya mkandarasi katika Mikoa ya Kigoma na Katavi na niwashukuru Wabunge wa mikoa hiyo pamoja na wananchi kwa subira yao namna ambavyo waliliridhia. Hata hivyo, nataka niseme mkandarasi huyu wa CCCE Etern anaendelea na kazi. Hata hivi karibu Mheshimiwa Waziri amewasha vijiji kama vitatu katika Wilaya ya kibondo.

Kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge amesema katika Kata ya Lusesa ambapo imezinduliwa na ahadi ilitolewa na kwamba mpaka sasa hivi bado vijiji vya Kata hiyo ya Lusesa havijawashwa, naomba nilichukue ili niwasiliane na Meneja wa TANESCO wa Mkoa wa Kigoma pamoja na mkandarasi, kwa vile uzinduzi ulifanyika kwa kata hii na ni wazi lazima ilikuwa kazi ifanyike kwa haraka na umeme uwake, pamoja na kwamba mkandarasi hana muda mrefu.

Kwa hiyo nitoe maelekezo kwamba agizo la Mheshimiwa Waziri litekelezwe katika Kata hii ya Lusesa, vijiji hivyo ambavyo vimeanishwa viwashwe na nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, baada ya hili Bunge la Bajeti, tutafanya naye ziara katika Mkoa wa Kigoma. Ahsante sana.