Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Vyuo Vikuu

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri yenye matumaini hasa kwa mwaka huu kutengewa hizo shilingi milioni 34, lakini hii barabara ya Kidiwa - Tandali imeshafanyiwa upembuzi yakinifu, ingawa sasa hizo fedha zitatafutwa mpaka lini? Hapo sasa napenda kufahamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Tarafa ya Mgeta kama alivyotembelea miaka ya nyuma, landscape yake bado ni ile ile ya milimani na watu wanaishi milimani. Kwa sasa tunategemea barabara hii kubwa moja toka Sangasanga kwenda mpaka Nyandila - Kikeo. Barabara hii ni mbovu sana hasa wakati wa masika; na tulishaahidiwa. Nakumbuka miaka ya 1970s alipokuja Mheshimiwa Abdu Jumbe aliahidi kwamba tutatengenezewa kwa kiwango cha lami. Ni kweli naweza nikalia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alipokuja aliahidi kwamba barabara hii itatengenezwa kwa kiwango cha lami kulingana na ubovu wake na nauli inakuwa kubwa: Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga barabara hii ya Sangasanga mpaka Nyandila kwa kiwango cha lami?

Swali la pili. Katika kutatua changamoto za usafiri katika Tarafa hii ya Mgeta, wananchi wamejitolea kutengeneza barabara nyembamba za kupita pikipiki, lakini wanakutana na changamoto ya utaalamu; wakati mwingine hawajui barabara iende hivi, kwa hiyo, wanakutana na changamoto hizo, lakini pia wanakutana na changamoto sehemu nyingine inabidi ijengwe madaraja au karavati.

Je, Serikali sasa iko tayari kuungana na wananchi hawa wa Tarafa ya Mgeta ili kupeleka wataalam pamoja na kuwajengea madaraja ili tuweze pia kutumia usafiri wa pikipiki kuunganisha vijiji na Kata? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, machozi tuliyoshuhudia yakitoka kwa Mheshimiwa Mbunge wa Mlimba pale, yanatosha kwa Mkoa wa Morogoro. Kwa hiyo, isingependeza tukapata machozi mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Dkt. Tisekwa akubaliane nami kwamba ahadi zote zinazotolewa na Viongozi Wakuu kwa maana ya Marais, hata kama Rais aliyetangulia ndio aliyetoa ahadi, sisi kama Serikali, ahadi hizo tunazitunza na ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba ahadi za viongozi wetu tunazitekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni Mheshimiwa Mbunge atakuwa shuhuda, katika ahadi ambazo zimetolewa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, katika bajeti ambayo tumepitisha, tumeanza kutekeleza katika maeneo yote ambayo ahadi zimetolewa. Tumeanza kujenga lami kwa kilometa moja moja. Kwa muungwana ahadi ni deni, naomba nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge, tutatekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili suala la pili ambapo wananchi wameanza kutengeneza barabara kwa ajili ya kupita angalau kwa pikipiki, lakini kinachokosekana ni utaalam, naomba nichukue fursa hii kumwagiza coordinator wa Mkoa wa Morogoro ahakikishe kwamba anamwagiza Meneja wa Wilaya husika ili kwenda kutoa utaalam ili wananchi pale ambapo wanatoa nguvu yao isije ikapotea na aone namna ambavyo na Serikali tunaweza tuka- complement ili kazi nzuri iweze kuonekana.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kama ilivyo kwenye swali la msingi, kule Moshi Vijijini katika Kata ya Mabogini iko barabara inayotoka Mabogini inakwenda Chekereni mpaka Kahe. Ile barabara huwa inakarabatiwa na wananchi na wakati mwingine na TARURA lakini kwa fedha kidogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliwahi kuuliza swali la msingi hapa, nikaahidiwa kwamba TARURA inao mpango mkubwa wa kuifanyia kazi hiyo barabara ili iweze kupitika katika kipindi chote cha mwaka. Sasa hivi tunavyoongea, ile barabara haipitiki kabisa kwa sababu imebadilika kuwa mfereji. Naomba …

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Komu, uliza swali tafadhali.

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumwuliza Naibu Waziri, ni lini hiyo kazi ya kuitengeneza hiyo barabara itaanza?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni jana tu Mheshimiwa Komu aliuliza swali kuhusiana na barabara ya Jimboni kwake na tukakubaliana kwamba ni vizuri tukaenda kwenye uhalisia. Naamini na hili anaongezea ili wakati tutakavyokuwa tunaenda Moshi tukashughulikie barabara zote mbili, tukitizama tujue suluhu ipi ambayo inatakiwa? Tujue tukiwa site. Mheshimiwa Komu, naomba niipokee katika lile la jana na la leo, kwa hiyo, tunakuwa na barabara mbili.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililopo kwenye Tarafa ya Mgeta linafanana kabisa na tatizo lililopo kwenye katika Tarafa ya Namasakata, katika Jimbo la Tunduru Kusini. Barabara ya Chemchem - Ligoma inazaidi ya miaka 10 tangu 2007 haijawahi kutengenezwa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara ile ili wananchi waweze kufaidika na Uongozi wa Awamu ya Tano?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge ni mashuhuda kwamba tangu tulivyoanzisha chombo chetu kwa maana ya TARURA, wengi wamekuwa wakipongeza ufanisi ambao umetokana na chombo hiki. Kwa hiyo, ni vizuri sasa tusiishi kwa historia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwmaba ni vizuri tukawasiliana na Meneja wa TARURA ili atupe uhalisia katika barabara hii ambayo anaongelea na hiyo miaka 10 ambayo iliahidiwa, hakika kwa Serikali ya Awamu ya Tano tunaahidi na kutekeleza.