Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA Aliuliza:- Serikali ilikopa fedha za mkopo nafuu kutoka Serikali ya India kwa ajili ya miradi 26 ya maji ikiwemo Mji wa Makambako. Je, ni lini mradi huo wa maji utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 11 Aprili, 2019 kwa kuwa Waziri aliapa mbele ya wananchi wangu na mbele ya Rais alipokuja tarehe hiyo. Je, ni lini mradi huu utaanza na ni mwezi gani utaanza ili wananchi wangu waendelee kuwa na imani kutokana na kiapo alichokifanya siku ile?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, siku ile kulikuwa na changamoto ya Mradi wa Ngamanga, kwa kuwa siku ile ilionekana ni lazima wataalam wabaki pale ili waweze kutatua tatizo hili; ni lini sasa hatua zilizochukuliwa ili kutatua mradi huu wa Ngamanga?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Sanga kwa kazi kubwa sana anayoifanya katika Jimbo lake la Makambako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kabisa Mheshimiwa Rais alivyofanya ziara na Mheshimiwa Waziri wetu alitoa commitment ya kuhakikisha mradi huu utatekelezeka haraka. Nataka nimtoe hofu kabisa sisi kama Wizara tumejipanga na tunatambua kabisa agizo la Mheshimiwa Rais kwamba tukishindwa kutekeleza mradi huu, tutatumbuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara ya Maji hatupo tayari kutumbuliwa, tutafanya kuusaini mkataba ule haraka ili utekelezaji wa miradi ya maji miji hii 28 utekelezwe kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa katika mradi ule wa Ngamanga, tulishatuma wataalam wetu na tumeshaangiza mabomba, kuna kazi inaendelea naamini ndani ya muda mfupi utakamilika na wananchi wake watapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA Aliuliza:- Serikali ilikopa fedha za mkopo nafuu kutoka Serikali ya India kwa ajili ya miradi 26 ya maji ikiwemo Mji wa Makambako. Je, ni lini mradi huo wa maji utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mji wa Muheza ni mojawapo ya sehemu ambazo zitafaidika na mradi huu kutoka India. Vile vile wakati wananchi wa Muheza wanasubiri mradi huu ambao ni mkubwa, upo mradi mwingine wa kutoa maji katika Mji wa Pongwe na kuleta Muheza Mjini. Mradi huu umefikia asilimia 70 na tumebakiza asilimia 30 tu ili wananchi wa Muheza waanze kupata maji ya uhakika. Tatizo ni uchakavu wa mabomba ambayo yako pale Mjini Muheza. Nataka kujua, ni lini Serikali itaruhusu mabomba yale yaanze kufumuliwa na kazi hiyo ianze kufanyika ili maji hayo yaweze kuunganishwa kuja Mjini Muheza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa
Mbunge, amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana, hususan katika suala zima la utatuzi wa maji katika Jimbo lake la Muheza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Balozi Adadi ameshakutana na Mheshimiwa Waziri na tumeshakubaliana kwamba sasa ile kazi ya kuhakikisha tunaondoa yale mabomba inafanyika mara moja. Nami kama Naibu Waziri tutalisimamia katika kuhakikisha ile kazi inaanza na wananchi wake waweze kupata maji safi.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA Aliuliza:- Serikali ilikopa fedha za mkopo nafuu kutoka Serikali ya India kwa ajili ya miradi 26 ya maji ikiwemo Mji wa Makambako. Je, ni lini mradi huo wa maji utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuuliza, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa kuboresha upatikanaji wa maji katika Jimbo la Rombo kadiri ya mpango ambao tumeupeleka Wizarani?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza Mheshimiwa Mbunge, amekuwa akiuliza swali la Rombo mara kwa mara na tumeshakubaliana tutakwenda Rombo, lakini kikubwa tunashukuru kwanza Bunge lako Tukufu limetuidhinishia kiasi cha shilingi bilioni 610 katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo kwa wananchi wa Rombo kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.