Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, Serikali inatumia Sheria ipi kutowapa wafanyakazi stahiki zao zinazohusu kupandishwa madaraja na ongezeko la mwaka (Annual Increment) kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Suala la kupandishwa madaraja linaambatana na ongezeko la mishahara. Serikali hii ya Awamu ya Tano imekuwa haipandishi watu madaraja kwa wakati, mtu anakaa mpaka miaka sita, saba, hajapandishwa madaraja. Nataka tu kujua Serikali iko tayari kuwalipa wale watu arrears zao kwa ile miaka ambayo hawakupandishwa madaraja kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Mheshimiwa Waziri amesema wafanyakazi wafanye kazi kwa bidii. Hivi kweli anafikiri unaweza kumkamua ng’ombe maziwa kama humpi chakula cha kutosha? Nakushukuru.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza Malapo, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba kipekee nimpongeze sana kwa jinsi ambavyo anafuatilia masuala yote ya watumishi wa umma nchini. Hata hivyo, naomba niseme kwamba, katika upandishwaji wa madaraja tuna madaraja ya aina tatu, kuna kupandishwa kwa madaraja kwa maana ya salary increase, kuna annual increment na kuna salary promotion, lakini katika suala la upandishwaji wa madaraja Serikali ilitoa tamko hapa wiki tatu zilizopita kwamba, kuanzia Mei Mosi mwaka huu (2019) Serikali inatarajia kupandisha madaraja, vyeo, watumishi zaidi ya 193,000. Hilo zoezi limeshaanza, lakini vilevile mwaka 2017/ 2018 Serikali ilishalipa annual increment zaidi ya bilioni 72.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile naomba niseme kabisa kwamba, Walimu walishalipwa zaidi ya bilioni 37, lakini kada nyingine za utumishi wa umma walishalipwa zaidi ya bilioni 35, lakini malimbikizo ya mishahara zaidi ya bilioni 75 zimelipwa. Isitoshe tu, lakini zaidi ya wastaafu waliokuwa wanaidai Serikali wameshalipwa zaidi ya bilioni tisa na hawa wastaafu ni zaidi ya 1,800.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili ni kwamba, Serikali inawajali sana watumishi. Sio lazima iwe katika nyongeza tu ya mshahara, lakini vilevile tukumbuke kwamba, Serikali ndio guarantor, watumishi wanapotaka kujenga nyumba, watumishi wanapotaka kufanya mikopo, kuna bima za afya zote hizo ni sehemu ya motisha. Kwa hiyo, naomba niseme kabisa Serikali inawajali watumishi katika njia mbalimbali na hata katika kupanda madaraja hiyo imeshaanza kutekelezwa. Ahsante.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, Serikali inatumia Sheria ipi kutowapa wafanyakazi stahiki zao zinazohusu kupandishwa madaraja na ongezeko la mwaka (Annual Increment) kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nampongeza dada yangu Mheshimiwa Mary Mwanjelwa kwa majibu mazuri yaliyokwenda shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali la nyongeza. Kwa kuwa, Serikali iliwafukuza watumishi ambao walighushi vyeti au hawakuwa na vyeti vya kidato cha nne na kati ya hao watumishi ambao walifukuzwa ni kwamba, walikopa katika benki zetu na mpaka sasa hawajui hatima yao na wengine wamekufa na wengine wamekimbia nyumbani kwa sababu, benki zinawafuata mpaka nyumbani. Nataka kujua kwa sababu, wakati wanachukua Serikali ndio ilikuwa guarantor wao. Sasa je, nini Kauli ya Serikali kwa benki ambazo zinawasumbua hawa watumishi na hawana jinsi ya kuweza kurudisha hizo fedha? Ahsante.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la mdogo wangu, Mheshimiwa Amina Mollel, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Serikali Mei, 2016 ilienda kwenye zoezi la kusitisha upandishwaji wa madaraja na vilevile kusimamia hilo zoezi zima la vyeti feki, lakini sio vyeti feki tu hata watumishi hewa. Tukumbuke kabisa kwamba, wakati najibu hapa swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Tunza Malapo nimesema Serikali inakwenda mbali zaidi katika kuwajali watumishi kwenye motisha hata katika kuwapatia guarantor mbalimbali ikiwemo na mikopo ya benki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tukumbuke watumishi hawa walikuwa ni halali, walikuwa ni watumishi halali na ndio maana Serikali inakuwa ni guarantor. Sasa kama wewe tayari umeshafukuzwa na hiyo tunasema ni crime kwa maana hiyo, sisi tunazingatia tu kwa yule mtumishi ambaye ni halali, Serikali itamjali, Serikali itakuwa ni guarantor pamoja na mambo mengine ya motisha. Ahsante.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, Serikali inatumia Sheria ipi kutowapa wafanyakazi stahiki zao zinazohusu kupandishwa madaraja na ongezeko la mwaka (Annual Increment) kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nina swali moja dogo la nyongeza. Annual increment ipo kisheria, kutowapatia wafanyakazi annual increment kunasababisha wakati atakapostaafu kupungua, kupunjwa kwa mafao yao sambamba na kupungua kwa pension zao za uzeeni na wanasema kwamba, hii awamu ya kuwasaidia wanyonge na maskini.

Je, hawaoni sasa kuendelea kutowapatia annual increment wafanyakazi hawa wanaendelea kuwapunja, kuwadhulumu wanyonge hawa na lini Serikali wataacha tabia hii?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Masoud, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudie tena kujibu kile nilichojibu kwamba, suala la annual increment mwaka 2017/2018, Serikali imeshalipa annual increment kwa watumishi wote wa umma bila kujali kada zozote. Pia nimesema imelipa zaidi ya bilioni 72, lakini sio kwamba, Serikali inawapunja ni sehemu ya mtumishi wa umma kupata motisha; tena nilitegemea kaka yangu hata angeshukuru kwamba, Serikali inawajali watumishi na ndio maana imeweza kuongeza hiyo mishahara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme jibu langu nilishalijibu, Serikali inawajali watumishi na ndio maana mwaka 2017/2018 imelipa zaidi ya bilioni 72. Ahsante.