Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali za barabarani za kutisha katika Milima ya Sukamahela eneo la Mbwasa, Manyoni na Sekenke Shelui:- (a) Je kwa kipindi cha miaka miwili yaani 2016 na 2017, ni ajali ngapi zimetokea katika milima tajwa? (b) Je, ni watu wangapi wamepoteza maisha na wangapi walijeruhiwa katika kipindi hicho? (c) Je, Serikali inatoa tamko gani ili kupunguza au kukomesha kabisa ajali katika maeneo haya ndani ya Mkoa wa Singida?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, uzembe na uchovu wa madereva, ubovu wa barabara, hii ni kampeni ya kila siku ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuzuia ajali lakini katika eneo hili bado ajali zinaendelea kutokea. Nilidhani labda Wizara ya Ujenzi itoe jibu la kiufundi zaidi kwa maana ya kurekebisha eneo hilo. Je, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi iko tayari kufanya usanifu upya katika eneo hilo na kufanya marekebisho ili kupunguza ajali?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa ajali zimekuwa nyingi sana katika eneo hilo, kwa mfano magari ya mafuta yamekuwa yakidondoka pale na moto unalipuka, majeruhi ni wengi lakini tumekuwa na tatizo la magari ya zimamoto pamoja na ambulance.

Je, Serikali iko tayari kutuletea magari ya zimamoto pamoja ambulance katika Wilaya ya Manyoni? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA) Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kujibu swali la nyongeza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba kabla ya ujenzi wa barabara katika eneo ambalo analitaja, ajali zilikuwa nyingi sana kuliko ilivyo sasa. Pamoja na ajali kuendelea kutokea, sisi Wizara ya Ujenzi baada ya ujenzi mara zote huwa tunaendelea kufanya tafiti ili kuona changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge eneo ambalo analitaja tutaweka msukumo mkubwa tuone kwa nini hizi ajali zinaendelea kutokea kutokana na hali ilivyo pale ili tuweze kuchukua hatua muafaka. Ni muhimu tu niendelee kusisitiza kama ilivyo kwenye jibu la msingi watumiaji wa barabara maeneo yote wazingatie alama za barabarani zinazowekwa kwa sababu maeneo ambayo ni hatari, sisi Wizara ya Ujenzi tumejitahidi kuweka alama kutoa tahadhali kwa watumiaji wa barabara ili muda wote tuwe salama tukiwa barabani.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumwambia Mheshimiwa Mtuka kwamba eneo hilo tutaliangalia kwa macho mawili ili tuone nini la kufanya. Hata hivyo, jambo hili lazima tushirikiane na watumiaji wengine wa barabara. Ahsante sana.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:- Kumekuwa na ajali za barabarani za kutisha katika Milima ya Sukamahela eneo la Mbwasa, Manyoni na Sekenke Shelui:- (a) Je kwa kipindi cha miaka miwili yaani 2016 na 2017, ni ajali ngapi zimetokea katika milima tajwa? (b) Je, ni watu wangapi wamepoteza maisha na wangapi walijeruhiwa katika kipindi hicho? (c) Je, Serikali inatoa tamko gani ili kupunguza au kukomesha kabisa ajali katika maeneo haya ndani ya Mkoa wa Singida?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo taarifa kuwa vituo vikubwa vinapima ulevi lakini kuna baadhi ya madereva wa magari makubwa wenye kuendesha masafa marefu wanavyopata muda wa kupumzika vituo vya njiani wanakesha wakinywa pombe na kusababisha ajali.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwadhibiti madereva hawa ili kupunguza ajali za barabarani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ambazo tunachukua katika kudhibiti madereva walevi, likiwemo kusimamisha magari hasa haya ambayo amezungumza yanayobeba abiria na mizigo na kuwapima vilevi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tukifanya kazi hiyo maeneo mbalimbali nchini na kwa kiwango kikubwa tumefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa aina ya madereva ambao wanaendesha magari hali wakiwa wamelewa. Pale ambapo tunawabaini basi hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yao.