Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Mlima Nyoka - Songwe yenye urefu wa kilometa 48.9 utaanza baada ya ya usanifu na upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika kutokana na jibu la msingi la Wizara nataka kujua kwanza, je, Serikali haioni kwamba inapoteza muda katika utekelezaji wa miradi mbalimbali hususan miradi ya barabara kwa kufanya upembuzi yakinifu, usanifu kwa muda mrefu?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, barabara hii ni barabara muhimu sana katika uchumi wa Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Songwe. Je, hawaoni kuna umuhimu wa kuongeza muda wa kufanya kazi kwa haraka ili hii barabara iweze kukamilika na wananchi wa mikoa hii miwili waweze kufaidika katika ujenzi wa kiuchumi katika Taifa hili la Tanzania?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwakagenda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu, usanifu wa kina utaratibu wa manunuzi na ujenzi ni utaratibu wa kimataifa na maana yake ni kuhakikisha kwamba hiyo kitu inaitwa value for money inapatikana vizuri kwa sababu msipofanya taratibu mkaainisha mahitaji yote, matokeo yake ndio kufanya upembuzi ambao ni pungufu na mkiingia tenda mnaweza msipate value for money.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, hoja yake ya kwenda haraka Serikali inaenda haraka ili kuhakikisha na sehemu kubwa ni msongamano wa pale Mbeya Mjini, ndio maana tunataka kuchepusha ili tutajenga mchepuo kwa ajili ya malori, lakini pale katikati kwa ajili ya kupanua ili msongamano usiwe mkubwa pale mjini Mbeya.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Mlima Nyoka - Songwe yenye urefu wa kilometa 48.9 utaanza baada ya ya usanifu na upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu na mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alikuwepo Mbeya kwenye ziara na Mheshimiwa Rais Mkoani Mbeya na aliona mwenyewe msongamano ulivyo kwa barabara hiyo ya TANZAM, ambayo kwa kweli inahudumia sio Mikoa ya Mbeya na Songwe tu, ni nchi nzima pamoja na nchi ya DRC, Zambia, Malawi pamoja na nchi zingine.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa fedha yake yenyewe ikisubiri fedha za Benki ya Dunia?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mwambalaswa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kuanza kabla ya kukamilisha usanifu, lakini suala la msongamano wa magari lina solution nyingi pia ukisimamia taratibu za kiusalama na ndio maana tuna Jeshi la Polisi bado wanameneji vizuri ili msongamano ule usiwe mkubwa na ndio maana msongamano upo kwa muda fulani fulani tu, lakini muda mwingine panakuwa pamekaa vizuri.

Mheshimiwa Mwambalaswa, hili tunalifanyia kazi, Serikali inatambua hiyo changamoto, kwa hiyo asiwe na wasiwasi, baada ya muda mambo yote yatakwenda vizuri.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Mlima Nyoka - Songwe yenye urefu wa kilometa 48.9 utaanza baada ya ya usanifu na upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa daraja Sibiti sasa limekamika kwa maana magari yanapita pale juu na Mheshimiwa Rais alitoa ahadi ya ile lami, sasa tungependa kujua kwamba ujenzi wa hizo kilomita 25 za lami umefikia wapi?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kiula kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Daraja la Sibiti limekamilika na tayari tumesaini mkataba na mkandarasi yule yule ili aweze kujenga zile kilomita 25 za lami. Kwa hiyo, fedha ipo na mkandarasi yupo na mkataba umesainiwa, anaendelea kujenga kwa kiwango cha lami hizo kilomita 25.