Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR aliuliza:- Walimu wote nchini wameingia katika Mkataba na Mwajiri ambao pamoja na mambo mengine unaonesha uwepo wa increment kila ifikapo mwezi Julai; tangu iingie madarakani Serikali ya Awamu ya Tano Walimu hawajapewa stahiki hiyo. Je, ni lini Walimu watalipwa stahiki hiyo kama malimbikizo au haki hiyo imeshapotea?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB MUSSA BAKARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Sijaridhika na majibu ya Serikali. Swali la kwanza, ni takribani miaka sita au saba huko nyuma, kwamba hizo nyongeza hazitolewi na Serikali. Je, hatuoni kwamba Serikali inafanya makusudi kufinya bajeti ili kuwakosesha Walimu hao nyongeza hizo za mishahara?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kama hii ipo kisheria, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa hiyo nyongeza ya mishahara na mara ya mwisho imetoa lini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge maswali yake ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma hapa kwenye jibu la msingi kwamba kulingana na kanuni za kiutumishi ambazo watumishi wote Tanzania sio Walimu tu watumishi wote wanajua, kwamba Serikali inapanga kuamka, kwa mfano kwaka huu wa fedha 2019/2020 kwenye bajeti yetu, kama hatukuuingiza kipengele cha nyongeza ya mishahara ambapo najua kuna tamko pale litatolewa kwenye Sherehe za Mei Mosi, maana yake ni kwamba mwaka huu kama hawataongeza mishahara halipaswi kuwa deni. Hili kwa mujibu wa kanunu za kiutumishi watumishi wote wanajua.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya Serikali kutathimini, tumesema mara ya mwisho nyongeza ya mishahara imetolewa mwaka 2017/2018, kwa hiyo hili kimsingi sio deni. Serikali inapanga kuinua mapato yake kama kuna uwezo wa kuongeza inaongeza na haya hayapaswi kuwa malalamiko.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR aliuliza:- Walimu wote nchini wameingia katika Mkataba na Mwajiri ambao pamoja na mambo mengine unaonesha uwepo wa increment kila ifikapo mwezi Julai; tangu iingie madarakani Serikali ya Awamu ya Tano Walimu hawajapewa stahiki hiyo. Je, ni lini Walimu watalipwa stahiki hiyo kama malimbikizo au haki hiyo imeshapotea?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, moja ya tatizo linalopoteza morality ya utendaji kazi katika watumishi wetu wa umma ni pamoja na kutokuweka wazi namna ambavyo Serikali italipa madeni ya huko nyuma ya watumishi wetu; na kwa kuwa kwa jambo hili watumishi wanakosa moyo wa kufanya kazi, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kukaa na vyama vya wafanyakazi ili waweze kuona namna gani ya kutatua tatizo hili la madeni ya huko nyuma ili watumishi wetu wote waweze kufahamu namna ambavyo Serikali kama mlezi wao na mwajiri wao itawatendea katika jukumu hili la kulipa madeni?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshafanyia kazi madai ya Walimu na watumishi wengine na ilishakutana na viongozi wa vyama vya wafanyakazi na utaratibu upo wa kuweza kulipa fedha hizi. Kwa sasa hakuna mgogoro kati Serikali na wafanyakazi, madeni yanajulikana. Tunatafuta fedha na uwezo wa Serikali kuanza kulipa madeni haya. Hata hivyo tunalipa kila muda, sio kwamba bajeti ni kubwa kiasi hicho, kwa hiyo madeni yanalipwa, lakini pia tumeshakubaliana namna ya kwenda, deni halisi linajulikana kwamba kila mtu anadai kiasi gani na hilo linafanyiwa kazi.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR aliuliza:- Walimu wote nchini wameingia katika Mkataba na Mwajiri ambao pamoja na mambo mengine unaonesha uwepo wa increment kila ifikapo mwezi Julai; tangu iingie madarakani Serikali ya Awamu ya Tano Walimu hawajapewa stahiki hiyo. Je, ni lini Walimu watalipwa stahiki hiyo kama malimbikizo au haki hiyo imeshapotea?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kukosekana kwa nyongeza ya mwaka kwa Walimu na wafanyakazi wengine (annual increment) kunapelekea wakati wakistaafu wanakosa haki yao ya msingi ya mafao ya kijumla, sambamba na pension yao wakati watakapostaafu.

Je, Serikali inawaambia nini Walimu ambao tayari wamestaafu mwaka jana na mwaka juzi ndani ya awamu hii ambao sasa wamekosa hiyo increment ambapo inaenda kuathiri mafao yao ya kustaafu na pension yao ya kila mwezi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masoud kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe maelezo kwa ufupi sana. Jambo la kwanza kuna tofauti kati ya madai na nyongeza ya mishahara. Tumesema kwenye nyongeza ya mshahara Serikali inapanga bajeti kulinga na mwaka husika wa bajeti. Kama hujaongezewa hilo sio deni la hupaswi kudai na nimejibu kwenye jibu la msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, madeni, haya ndio haki ya watumishi kudai na utaratibu wake ni kama nilivyoeleza namna ya kuweza kuyafidia. Walimu hata juzi Waziri wa Nchi ametoa tamko hapa, hata kupandisha madaraja imeelekezwa vizuri kwenye Waraka wa Waziri kwamba ni muhimu izingatiwe kama kuna watu wanakaribia kustaafu na hawajapandishwa daraja na wamekidhi vigezo, tuanze na hao.

Kwa hiyo hilo jambo la kuwa karibu na kustaafu limezingatiwa na hakuna mtu atakayenyimwa haki yake, deni ni deni hata kama mtu atakuwa amestaafu, atapewa na tutakapoanza kulipa madeni kimsingi tunaangalia wale wenye shida, wale waliostaafu ndiyo tunaanza kuwalipa na wengine wanaendelea. Ahsante.