Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Chilonwa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambayo kwa sasa imefikia kwenye linta?

Supplementary Question 1

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu mazuri sana ya Serikali ambayo ameyatoa hapa Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini kwa umuhimu wa eneo lile niombe tu Mheshimiwa Naibu Waziri tupate nafasi twende sote kwa pamoja tutembee katika kijiji kile tuone jiografia ya pale na umuhimu wake ili Serikali iweze kuona inaisaidia vipi Halmashauri ya Chamwino katika kukamilisha zahanati ile.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Mbunge wa Chamwino Makao Makuu ya Ikulu ya Nchi kwa kukubali na kutupongeza, lakini mimi nipo tayari sana wakati wowote mwezi huu wa Tano twende katika Jimbo lake tukatembee. Ahsante.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Chilonwa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambayo kwa sasa imefikia kwenye linta?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kijiji cha Kitifu kipo Kata ya Mgombezi kimejenga zahanati na kimekamilisha, isipokuwa tu tunaomba mtusaidie majengo ya daktari pamoja na majengo mengine ambayo hayajakamilika. Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana, je, mtakuwa tayari kutusaidia angalau tuweze kupata fedha kwa ajili ya jengo la mganga?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge mwanamke wa Jimbo ambaye anafanya kazi kubwa sana pale Korogwe. Naomba nimhakikishie kwamba mimi, Wizara na Serikali tupo tayari kuwasaidia Wabunge wanawake ili waendelee ku-maintain Majimbo yao. Tutafanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Chilonwa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambayo kwa sasa imefikia kwenye linta?

Supplementary Question 3

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Wiki tatu zilizopita niliuliza swali kuhusu Zahanati ya Kigarama ambayo wananchi wamejenga kwa nguvu zao, miaka miwili wamekamilisha OPD, lakini kuna upungufu wa choo na nyumba ya Mganga na haiwezi kufunguliwa kabla ya hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali itaweza kukamilisha majengo hayo yanayopungua ili Kituo hiki kiweze kutoa huduma kwa wananchi ambao wanahangaika muda mrefu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Jambo hili tunalifahamu na kama nilivyojibu tangu wiki iliyopita ni kwamba tupo kwenye mchakato wa kupeleka fedha za kumalizia maboma ya Zahanati na Vituo vya Afya na naomba jambo hili tulichukue kwa uzito, tutalifanyia kazi, Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi. Ahsante.