Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Jimbo la Tunduru Kusini lina jumla ya vijiji 65, kati ya hivyo ni vijiji vinne tu ndiyo vimefikiwa na umeme wa REA Awamu ya I na ya II:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika vijiji 61 vilivyobaki?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Katika Vijiji alivyovitaja kuwa vilipata umeme awamu ya kwanza na ya pili vya Azimio, Chiwana, Mkandu na Mbesa umeme ulipita barabarani ndani ya mita 100 kutoka barabara kuu ilikopita nguzo kubwa. Je, ni lini mradi wa kujazilizia mitaa iliyobaki katika Vijiji hivyo vya Azimio, Chwana, Mkandu na Kijiji cha Airport itaanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, mwaka 2017 nilipeleka maombi maalum kuongeza vijiji katika Mradi wa REA katika Vijiji vya Tuwemacho, Chemchem, Ligoma, Makoteni, Nasia, Semeni, Mtina, Angalia, Nalasi, Mchoteka, Kitani, Mkolola pamoja na Masakata. Nini kauli ya Serikali kuhusu uwekaji wa awamu ya tatu ya umeme katika Vijiji hivyo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya swali la msingi la Mheshimiwa Mpakate, lakini vilevile nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mpakate jinsi anavyofuatilia umeme katika Jimbo lake.

Mheshimiwa Spika, ni kweli vijiji vingi tuliviweka kwenye round II ya awamu ya tatu inayoendelea, lakini baada ya kuona changamoto kubwa sana katika Jimbo la Tunduru Kusini tulifanya mapitio mapya na vijiji 13 tuliviingiza kwenye round inayoendelea. Kwa hiyo katika utaratibu tunaojenga line kwa sasa kutoka Tunduru Mjini mpaka Msingi umbali wa kilometa 20 tumechukua vijiji vingine 13 vikiwemo vijiji ambavyo anavisema vya Angalia, Semeni ambako Mheshimiwa Mbunge anatoka lakini mpaka Tuwemacho, Chemchem mpaka Chilundundu kwa vijiji vyote hivyo viko kwenye mpango. Pia Wakandarasi kupitia TANESCO sasa wanavifanyia kazi, kwa hiyo nimpe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge pamoja na kumpongeza, vijiji 13 vya nyongeza tayari vimeshaanza kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu nyongeza ya vijiji vya ujazilizi; mradi umeshaanza na utekelezaji wa maeneo ya kujaziliza, maeneo ya vitongoji unaanza mwezi huu utachukua miezi 12, lakini maeneo ya Azimio pamoja na Mbesa ambako tayari umeme upo kwenye Vitongoji 17, tayari pia TANESCO wameanza kuvifanyia kazi.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Jimbo la Tunduru Kusini lina jumla ya vijiji 65, kati ya hivyo ni vijiji vinne tu ndiyo vimefikiwa na umeme wa REA Awamu ya I na ya II:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika vijiji 61 vilivyobaki?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Singida Kaskazini lina miradi ya REA II, REA III, phase I pamoja na umeme wa backborne kwenye vijiji 54. Hadi sasa ni vijiji 13 tu ndiyo ambavyo vimekwishakufikiwa na umeme na vingine mpaka sasa bado. Je, Mheshimiwa Waziri wa Nishati yuko tayari kuambatana nami kutembelea Jimbo la Singida Kaskazini kujionea changamoto zilizopo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monko kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Monko amerejea Mradi wa REA awamu ya pili ambapo kwa kweli kama Serikali tuliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Singida na Kilimanjaro baada ya makosa ambayo yalitendeka katika Mradi wa REA awamu ya pili na tukafanya kazi na kumweka Mkandarasi mpya ambaye anaendelea na kazi kwa kushirikiana na REA.

Mheshimiwa Spika, swali lake ameulizia utayari wetu wa kuambatana naye; nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge nipo tayari mimi pamoja na Waziri kwa wakati tofuati kutembelea Jimbo lake kama ambavyo tulishafanya mwezi wa Nane tulitemebelea Jimbo lake ikiwemo Kijiji cha Iddi Simba na tuliwasha umeme pia aliwakilishwa na Mheshimiwa Mbunge Aisharose Matembe. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge niko tayari muda wowote kutembelea eneo lake na kuendelea kuwasha umeme na kukagua kazi inavyoendelea. Ahsante sana.