Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Changamoto kubwa inayowafanya wanawake wa Tanzania wasishiriki kwenye Sekta ya Kilimo na ufinyu wa Bajeti na mitaji kutoka kwenye Taasisi za Kifedha:- Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya ushiriki wa wanawake kwenye Sekta ya Kilimo ukizingatia changamoto hizo?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nimeyapokea.

Swali la kwanza; kwa kuwa Benki ya Kilimo mpaka sasa haijaweza kuwa katika Mikoa yote na hizo benki nyingine alizozizungumzia kama NMB na alitaja benki mbili zote hizo ni Commercial na zinahitaji wewe unayekwenda kukopa lazima uwe na dhamana na wanawake wengi hawana nyumba wala hawana dhamana ambazo zinatambulika kibenki: Je, Serikali iko tayari ku-guarantee mikopo hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Tatizo katika kilimo ni pamoja na mbegu bora na mara nyingi unakuta kwamba mbegu hizo ni ghari na pia siyo rahisi kumfikia mkulima. Ni lini sasa mbegu hizo zitagaiwa kwa wanawake hao kupitia katika Kata zao?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, nashukuru. Swali la kwanza la Mheshimiwa Shally Rymond anataka kujua kwamba kwa sababu benki ya Maendeleo ya Kilimo haipo kila Mkoa na kwamba hizi benki nyingine ni za kibiashara, anataka kujua mikakati ya Serikali kama iko tayari kudhamini mikopo hii.

Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali tupo tayari na tulishaanza na ndiyo maana kama alivyosema Benki ya Maendeleo ya Kilimo haipo kila Mkoa, ni kwa sababu hii ni Benki ya Maendeleo, ni benki ya kimkakati na lengo lake ni kuwasaidia wakulima kupitia madirisha mbalimbali ya Taasisi za Fedha. Moja, tulichokifanya, Serikali kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo tumedhamini mikopo yote ambayo inayotolewa na Benki ya NMB ili kwenda kwenye Sekta ya Kilimo hususan pamoja na akina mama.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwamba ni lini Serikali itatengeneza mazingira ya mbegu hizi zikapatikana katika ngazi za Kata ili wanawake wazipate kiurahisi?

Mheshimiwa Spika na Mheshimiwa Mbunge, ni kwamba Serikali siku zote kwamba tuko tayari. Mbegu hizi kupitia Shirika letu la Mbegu (ASA) na Taasisi nyingine binafsi na mawakala mbalimbali, tumeweka mazingira mazuri kwamba mbegu hizi zinapatikana Tanzania kote, siyo kwa kwenye Kata tu, mpaka ngazi za vijiji kwa kuzingatia mahitaji. Kama kuna mahitaji maalum katika eneo unalotoka, baada ya Bunge hili tuone ili tuwaelekeze wenzetu wa ASA ili waweze kupeleka mbegu haraka iwezekanavyo ziwafikie wakulima.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Changamoto kubwa inayowafanya wanawake wa Tanzania wasishiriki kwenye Sekta ya Kilimo na ufinyu wa Bajeti na mitaji kutoka kwenye Taasisi za Kifedha:- Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya ushiriki wa wanawake kwenye Sekta ya Kilimo ukizingatia changamoto hizo?

Supplementary Question 2

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ukiacha Taasisi nyingi kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake lakini Benki ya Kilimo ndiyo yenye dhamana ya kutoa mikopo. Benki ya Kilimo imekuwa na tabia ya ubaguzi, inatoa mikopo kwa wale wanawake ambao wana uwezo au wake za vigogo, lakini wale wanawake ambao wana uwezo mdogo na wamejiunga kwenye vikundi wamekuwa wakipewa masharti magumu.

Je, Serikali inatoa kauli gani hususan kwa wanawake wa Ulanga, Kilimanjaro na juzi nilikuwa Mbeya kule, hamna hata mmoja aliyepata mkopo?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, nashukuru. Napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mlinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza siyo kweli kama Serikali kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo tunatoa mikopo kwa kibaguzi. Hii kama nilivyosema ni benki ya maendeleo, ni benki ya kimakakati na tumeianzisha maalum kwa ajili ya kuendeleza sekta ya kilimo hapa nchini. Kwa hiyo hizi ni pesa za umma, kama pesa za umma lazima zina taratibu zake na zina masharti. Labda hao wanaoona wanapata maana yake ni wanawake waliotimiza vigezo vinavyohitajika na benki ili waweze kupata mikopo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo niendelee kumshauri kama nilivyosema kwenye jibu letu la msingi, tumewaelekeza wanawake hao hususani wale wa vijijini wajiunge kwenye vikundi, vile vikundi vyao ndiyo vitatumika kama dhamana na benki hii itaendelea kutoa mikopo. Hivi ninavyozungumza, pamoja na maelekezo ya Serikali tuliwaambia kwamba mikopo wanayotoa asilimia 20 watoe kwa akinamama, lakini benki hii imeweza kutoa mpaka leo tunavyozungumzia zaidi ya asilimia 33 ya mikopo yote waliyotoa imekwenda kwa akinamama.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Changamoto kubwa inayowafanya wanawake wa Tanzania wasishiriki kwenye Sekta ya Kilimo na ufinyu wa Bajeti na mitaji kutoka kwenye Taasisi za Kifedha:- Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya ushiriki wa wanawake kwenye Sekta ya Kilimo ukizingatia changamoto hizo?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara ya Kilimo. Serikali kupitia Wizara ya Kilimo mwaka juzi walianzisha utaratibu wa kwamba zao la korosho lilimwe katika kila mkoa hapa Tanzania kwenye mikoa 17. Wakati wa uhamasishaji huo, wakawahamasisha pia akinamama wengi sana kwenye Wilaya ya Masasi, Wilaya ya Tandahimba ikiwemo pamoja na Newala, Lulindi pamoja na Ruangwa wakope pesa kwenye mabenki lakini pia walikopeshwa pesa pamoja na Halmashauri. Sasa bahati mbya sana mpaka sasa hivi Serikali haijalipa pesa hizo za hao akinamama na wameanza kutaifishwa, kufilisiwa na wanashindwa kufanya shughuli zao na hapa tunasema tunataka tuwawezeshe akinamama. Sasa nataka tusikie kauli ya Serikali, je, ni lini watawalipa akinamama hao waliozalisha miche iliyopelekwa mikoa mingine 17 pesa zao?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, nashukuru. Napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mwambe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli Serikali miaka yote tuna mradi wa kuongeza uzalishaji wa korosho hapa nchini kutoka tani 300,000 za sasa kwenda tani milioni moja ndani ya miaka mitano ijayo. Kwa hiyo miongoni mwa miradi hiyo lazima tulikuwa tuongeze eneo la uzalishaji na moja ya mikakati ilikuwa kwamba kuzalisha miche zaidi ya milioni 10 kwa kila mwaka kwa muda wa miaka hiyo mitatu. Pia ni kweli kwamba miche hii ilizalishwa kwa vikundi mbalimbali vya akinamama na vijana, lakini baada ya kupitia yale madeni, tumegundua kwamba kuna kasoro nyingi katika yale madeni.

Mheshimiwa Spika, kama ninavyosema siku zote kwamba hizi ni pesa za umma, kama Serikali tuliona ni busara kwamba tufanye uhakiki wa kina ili tujue, tubainishe na kutambua yapi madai halali na yapi madai yaliyopikwa ili wale halali waweze kulipwa. Niendelee kumsihi tu Mheshimiwa Mwambe na wengine wote waendelee kuvuta subira, jambo hili karibu linafika mwisho, timu ya uchunguzi iko katika hatua za mwisho kumaliza, tukimaliza hela zipo na tutawalipa wote waliozalisha miche hii.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND (K.n.y. MHE. ESTER M. MMASI) aliuliza:- Changamoto kubwa inayowafanya wanawake wa Tanzania wasishiriki kwenye Sekta ya Kilimo na ufinyu wa Bajeti na mitaji kutoka kwenye Taasisi za Kifedha:- Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya ushiriki wa wanawake kwenye Sekta ya Kilimo ukizingatia changamoto hizo?

Supplementary Question 4

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja ya changamoto wanayoipata wakulima wakiwemo Wanawake hasa wanaolima tumbaku ni upatikanaji wa pembejeo kwa wakati hususan mbolea aina ya NPK.

Je, Serikali inawahakikishiaje wakulima wa tumbaku kwamba watapata mbolea ya NPK kabla ya mwezi wa Nane mwaka huu?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Spika, nashukuru. Napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Sitta kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli yaani mwaka jana mbolea zilichelewa kufika kwa wakulima na sababu ndiyo mwaka wa kwanza ambao tulikuwa tunatekeleza ule mfumo wa bulk procurement (uagizaji wa mbolea kwa pamoja) na kitu chochote kikiwa cha kwanza lazima kina changamoto zake. Tumeona hizo changamoto, lakini mwaka huu ambao mchakato wa kufahamu kiwango cha uzalishaji na mahitaji ya mbolea tumeshakifanya mapema na tayari sasa hivi watu tuko kwenye mchakato wa kupata Mawakala wa kuagiza hizo mbolea na vyama vyenyewe tumevipa ruhusa ya kuagiza. Kwa hiyo, hilo tatizo mwaka huu halitakuwepo na mbolea zitafika kwa wakati kwa wakulima wa tumbaku na hasa akinamama wa Tabora.