Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuelekeza taasisi zote nchini kuwa sifa mojawapo ya kuajiriwa iwe ni umri wa miaka 21- 35 ili kuwezesha Vijana wengi wanaotoka vyuoni kupata ajira?

Supplementary Question 1

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Spika, pamoja na sheria kuelekeza umri wa kuajiriwa kazini, bado ajira nyingi zinapotangazwa hapa nchini hutoa sharti la kuwa na uzoefu wa kazi, kuanzia umri wa miaka mitano na kuendelea, na hivyo hii huwaondolea fursa vijana wengi wanaotoka vyuoni kutokupata ajira.

Mheshimiwa Spika, hivyo, naomba Serikali itoe majibu hapa kwamba ni lini itatoa tamko kwa waajiriwa kuondoa sharti la vigezo ili kuwapa fursa vijana wanaotoka vyuoni, isipokuwa tu kwa zile ajira ambazo zinahusu nafasi za juu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Spika, kwa kutambua kwamba kumekuwepo na changamoto kubwa sana kwa vijana wahitimu wa vyuo vikuu na vyuo vya elimu ya juu kupata kazi kwa kikwazo cha uzoefu. Ofisi ya Waziri Mkuu katika utekelezaji wa programu ya ukuzaji ujuzi nchini, imeanzisha program maalum kabisa ambayo Mheshimiwa Waziri Mkuu alizindua miongozo yake ya mafunzo ya Uanagenzi na mafunzo ya Vitendo Kazini (Internship). Ambayo hivi sasa kwa mujibu wa utaratibu tuliouweka, tunawachukua vijana kutoka vyuo vikuu, kutokana na fani walizonazo na makubaliano ambao.

Mheshimiwa Spika, sisi Serikali tumeingia na chama cha waajiri na sekta binafsi, tunawapeleka katika kampuni husika kwenda kufanya kazi kivitendo, ambako wanakaa miezi sita mpaka miezi 12 na baadaye mwajiri katika eneo husika, anampatia cheti cha kumtambua kama ni mwanachuo ambaye amekaa kwake katika fani husika kwa miezi 12 ili baadaye ikitangazwa nafasi ya ajira ya kazi ambayo ameifanyia kwa vitendo, iwe pia ni sehemu ya yeye kumsaidia kupata ajira, kwa maana ya kutumia ule utambulisho wa kwamba tayari ameshafanya kazi katika mwajiri husika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama Serikali na sisi tumeliona jambo hilo, na ndiyo maana tumeweka nguvu kubwa sasa hivi katika kuhakiksiha kuwa tunawajengea ujuzi vijana wetu ili waweze kuwa na sifa za kuajirika na baadaye kuwasaidia kupata ajira pasipo kikwazo cha uzoefu.