Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Miradi ya maji katika vijiji vya Lupunga, Ruvu Dosa na Kipandege Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha bado inasuasua mpaka sasa. Je, ni lini miradi hiyo itapatiwa fedha ili iweze kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA MCHAFU CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushuru pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri sasa ningependa nimuulize maswali wadogo wawili yangongeza. Tunaishukuru sana Serikali kwa kuikabidhi miradi ya serikali kwa DAWASA ikiwemo mradi wa Bokomnemela Vikuruti na Ngeta.

(i) Ni lini sasa DAWASA itakamilisha zoezi la ufangaji maji majumbani ikizingatiwa wananchi wanauhitaji mkubwa wa maji na hivi tunavyozungumza ni nyumba 30 tu zilizofungwa kati ya wananchi wote walojaza fomu?

(ii) Nataka kujua ni kwanini DAWASA wanafanya ucheleweshaji wa kijiji cha kipangege Kata Soga. Kijiji hakipati maji ya kuridhisha presha yake ni ndogo na wakati mwingine hakuna kabisa maji nataka kusikia kauli ya Serikali inasema nini juu ya uchelewashi huu unaofanywa na DAWASA?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma ni miongoni mwa Wabunge makini katika ufuatiliaji na kupigania maendeleo ya watu wake katika Mkoa wa Pwani. Lakini kikubwa maji hanaya mbadala sasa niagize Mkurugenzi wa Mamlaka wa Majisafi na Usafi wa Mazingira DAWASA Eng. Luhemeja katika kuhakikisha suala la ufungaji mita kwa wananchi lakini pia mradi huu wa Soga uwezi kukamilika kwa wakati ahsante sana.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Miradi ya maji katika vijiji vya Lupunga, Ruvu Dosa na Kipandege Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha bado inasuasua mpaka sasa. Je, ni lini miradi hiyo itapatiwa fedha ili iweze kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na niweze kuuliza wali la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yanayowapata watu Kibaha yanafanana na watu wa kigamboni

Je Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi wa visima vya Kimbiji na Mpera ili wananchi wa Kigamboni, Tuangoma, Chamazi na Mbagala waweze kupata maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nimpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya lakini kikubwa katika kuhakisha tunatatua tatizo la maji katika Mkoa wa Dar es Salaam. Wizara yetu ya maji kupitia Wizara ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira DAWASA imechimba visima zaidi ya 20 Mpera na Kimbiji. Sasa agizo la Mheshimiwa Waziri nikuhakisha visima vitano wanatangaza tenda mkandarasi ampatikane ili wananchi wa maeneo ya Kigamboni na Mbagala waweze kupata maji safi, salama na ya kutosheleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tupo katika hatua hiyo tunataka mkandarasi akapopatikana kazi ianze mara moja na wananchi hawa waweze kupata maji.