Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- Serikali ilianzisha Kanda Maalum ya Kipolisi Dar es Salaam na kufanya Wilaya ya Temeke kuwa Mkoa wa Kipolisi; tangu Temeke iwe Mkoa wa Kipolisi kumekuwa na ongezeko kubwa la uhalifu hasa maeneo ya Jimbo la Mbagala:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbala? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Vituo vya Polisi na kuviongezea askari, vitendea kazi na kujenga nyumba za askari katika maeneo ya Jimbo la Mbagala?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Swali lwa kwanza, kama ambavyo Serikali inakiri umuhimu wa kituo hiki lakini ni muda mrefu sasa majibu yamekuwa ni haya haya kwamba bajeti itakaporuhusu, bajeti itakaporuhusu. Juzi tumepitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani na ujenzi wa kituo hiki haupo kwenye bajeti hiyo. Sasa nataka kujua Mheshimiwa Naibu Waziri anavyotuambia tusubiri bajeti itakaporuhusu ni bajeti ipi anayoizungumzia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wamekuwa wakijitahidi kujenga vituo vya polisi lakini vingi havifanyi kazi kwa saa 24 yaani havipewi hadhi ya kufanya kazi saa 24. Kwa mfano, Kituo cha Polisi cha Buza ambacho wananchi wamekijenga kwa kiwango cha hali ya juu lakini mpaka leo ni miaka mitano bado kinafanya kazi kwa saa 12 tu. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari sasa kutoa amri kituo hicho kianze kufanya kazi kwa saa 24?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mtolea, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nikijibu swali lake la kwanza kwamba bajeti ya mwaka huu haikuhusisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbagala. Hata hivyo, si Kituo cha Polisi Mbagala tu, vituo vya polisi vingi havikuhusishwa sababu ni kama nilivyozungumza mwanzo kwamba hatuwezi tukategemea bajeti ya mwaka mmoja itatue changamoto ya vituo vyote au maeneo yote. Kwa hiyo, kazi hii itaenda kwa awamu na kituo hiki kama hakijaweza kupata fursa katika bajeti hii basi kinaweza kupata fursa katika bajeti zinazokuja. Cha muhimu atambue Serikali inathamini na inatambua juu ya umuhimu wa ujenzi wa kituo hiki hasa ukitilia maanani changamoto za usalama katika Mkoa wa Kipolisi Temeke na Wilaya ya Mbagala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la pili, kwanza niwapongeze yeye pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke kwa ujumla wao kwa jitihada zao kubwa ambazo wanachukua katika kusaidiana na Serikali kupunguza changamoto ya vituo vya polisi. Nami ni shahidi kwani nimeshiriki katika programu mbalimbali ikiwemo programu ya uchangishaji fedha wa kituo cha Chamanzi, ambapo sasa kipo katika hatua nzuri ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo, nimhakikishie kwamba tutakapomaliza kujenga vituo hivi madhumuni yake ni vitumike kama ilivyokusudiwa. Hoja ya kutumika saa 24 inategemea na aina ya kituo. Kwa mujibu wa PGO kuna Class A, B na C. Kuna vituo ambavyo vinapaswa vitumike kulingana na category ya class ya kituo hicho kwa muda wa saa 24 na viko ambavyo havipaswi kutumika kwa muda wa saa 24.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo ambacho amekizungumza ni Class C, kwa hiyo, hakiwezi kutumika kwa saa 24. Si kwa sababu labda hatuna askari wa kupeleka ama tumekitelekeza au hatuoni umuhimu huo lakini ni kwa sababu ya aina ya kituo na utaratibu ambao tumejiwekea kwa mujibu wa PGO.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- Serikali ilianzisha Kanda Maalum ya Kipolisi Dar es Salaam na kufanya Wilaya ya Temeke kuwa Mkoa wa Kipolisi; tangu Temeke iwe Mkoa wa Kipolisi kumekuwa na ongezeko kubwa la uhalifu hasa maeneo ya Jimbo la Mbagala:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbala? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Vituo vya Polisi na kuviongezea askari, vitendea kazi na kujenga nyumba za askari katika maeneo ya Jimbo la Mbagala?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Mbagala limekuwa na ongezeko kubwa la watu hali ambayo inachangia sana kuwa na ongezeko kubwa la uhalifu lakini mazingira ya Kituo cha Polisi Mbagala Kizuiani ni mabaya sana pamoja na makazi ya polisi. Pamoja na hayo, Serikali imeeleza wazi kwamba utaratibu wa kujenga kituo hiki kwa sasa haupo. Je, Serikali ina mkakati gani basi wa kuwaboreshea angalau makazi ya askari wale jamani, hali mbaya, nyumba zile haziendani na eneo lile? Mbagala sasa imekua, mabasi ya mwendokasi yanakuja, zile nyumba za Polisi pale zinatisha. Je, Serikali mna mkakati gani wa kufanya angalau maboresho ya eneo lile?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dar es Salaam, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya uchakavu wa nyumba za askari katika eneo la Mbagala Kizuiani tunaifahamu. Nichukue fursa hii kumpongeza kwa mara nyingine tena Mheshimiwa Rais kwa kuliona hilo na kutupatia fedha ambazo tunatarajia kujenga takriban nyumba 400 nchi nzima. Katika maeneo ambayo nyumba hizo zitajengwa ni Kanda Maalum ya Dar es Salaam ikiwemo Mkoa wa Kipolisi wa Temeke. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na nimpongeze kwa concern na huruma aliyokuwa nayo kwa askari wetu, Serikali inalitambua na tunaendelea kulitatua hatua kwa hatua.