Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Kuna uhaba wa watumishi na vitendea kazi katika Idara ya Ardhi na Maliasili – Wilaya ya Muheza kunakosababisha kuazima watumishi na vifaa kutoka Halmashauri nyingine:- (a) Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi na kununua vitendea kazi katika Idara hiyo? (b) Je, Serikali iko tayari kuwawekea wananchi Wanasheria ili kusaidia kutatua migogoro ya ardhi?

Supplementary Question 1

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikiliza Waziri wakati anajibu, nafahamu Wilaya ya Muheza ni moja kati ya wilaya ambayo iliyofutiwa hati mashamba zaidi ya sita toka wawekezaji ambao mengi yao yalikuwa mashamba ya mikonge. Kutokana na hilo kumekuwa na tatizo kubwa sana la migogoro, sasa naomba niulize kuhusu kwanza watumishi, Serikali imejiandaaje hasa kwa mwaka huu inatuambia nini wananchi wa Muheza kwenye suala la watumishi, tutawaongezea watumishi wangapi ukizingatia tatizo la watumishi linatuathiri sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Rais alipokuwa anaenda kuzindua bomba la mafuta kule Tanga alipopita Muheza aliahidi na aliwaambia wananchi watagawiwa maeneo bure walime na kuyaendeleza, lakini wananchi wa Muheza hawakuamini hivyo, wamekuwa wanalipishwa gharama za upimaji na wamekubali. Hata hivyo, kuna migogoro mikubwa sanasana, wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wanaohusika na ardhi wamekuwa wanauza maeneo ya wananchi kwa watu tofauti ambao siyo wakazi wa Muheza. Nataka nipate kauli ya Serikali, je, wapo tayari kutuma timu maalum iende Muheza ikasimamie masuala ya ugawaji wamashamba na viwanja hasa katika maeneo haya sita ambayo yamefutiwa hati?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri katika swali lake la msingi, lakini naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Yosepher kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la watumishi nadhani hata kipindi kilichopita Bunge lililopita tulilizungumzia kwamba baada ya watumishi sasa kuelekezwa kwenye Wizara ya Ardhi, tayari tulikuwa tunafanya utaratibu wa kupata ikama yao na kujua wanataaluma tulionao ni kiasi gani ili waweze kusambazwa katika Halmashauri kulingana na uhitaji na kazi hiyo inafanywa na Ofisi ya Rais, TAMISEMIkwa sababu suala la uhamisho litasimamiwa na Wizara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile katika suala zima la ugawaji wa mashamba na wakati tumeenda kwenye ziara ya Kamati ya Ardhi suala hilo tulilikuta, lakini tayari Ofisi ya Halmashauri pale Muheza walikuwa wameshaanza kugawa hekari tatu tatu kwa wananchi katika yale mashamba yaliyorejeshwa na suala la kulipishwa katika suala la upimaji ni makubaliano ya Halmashauri yenyewe ambayo walikaa wakakubaliana na kiasi cha wao kuchangia na ndicho hicho kilichofanyika. Kwa hiyo suala linalofanyika linafanyika kutegemeana na mamlaka zenyewe za upangaji na matumizi bora ya ardhi. Kwahiyo hilo ni suala ambalo lipo chini ya halmashauri na Serikali inalisimamia kulingana na makubaliano ambayo yanakuwa yamefikiwa, hakuna migogoro ambayo itaendelea kwa sababu kila kitu kinasimamiwa.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Kuna uhaba wa watumishi na vitendea kazi katika Idara ya Ardhi na Maliasili – Wilaya ya Muheza kunakosababisha kuazima watumishi na vifaa kutoka Halmashauri nyingine:- (a) Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi na kununua vitendea kazi katika Idara hiyo? (b) Je, Serikali iko tayari kuwawekea wananchi Wanasheria ili kusaidia kutatua migogoro ya ardhi?

Supplementary Question 2

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Migogoro ya ardhi katika nchi hii ipo katika kila wilaya na kila mkoa, lakini katika Mkoa wetu wa Songwe mpaka sasa hivi hatujapata Baraza la Ardhi la Wilaya na Wilaya zetu za Ileje Momba na maeneo mengine zinakwenda Mbeya Mjini. Je,ni lini Serikali sasa itaanzisha Baraza la Ardhi la Wilaya katika Mkoa wetu wa Songwe?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Meshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakajoka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ambayo Serikali inatakiwa kufanya kazi kila wilaya inapaswa kuwa na Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya na tayari tulishasema na kutoa majibu tuna mabaraza 97 ambayo tayari yalikwishaanzishwa na sasa hivi yote yatakwenda kufanya kazi kwa maana ya kwamba tumepata baadhi ya watumishi ambao wanakwenda. Hata hivyo, kufungua Baraza la Ardhi katika eneo inategemeana pia na idadi ya kesi na namna ambavyo wilaya yenyewe imejiandaa katika kutupa ofisi, kwa sababu katika maeneo ambayo tunafanyia kazi hiyo, Wizara haijengi ofisi bali Halmashauri na mkoa husika wanatupa majengo, sisi tunapeleka watumishi pamoja na vitendea kazi, kwa maana ya thamani. Kwahiyo kama watakuwa tayari, basi tunaweza tukafika katika eneo hilo, lakini pia tunazingatia takwimu na migogoro iliyopo. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Kuna uhaba wa watumishi na vitendea kazi katika Idara ya Ardhi na Maliasili – Wilaya ya Muheza kunakosababisha kuazima watumishi na vifaa kutoka Halmashauri nyingine:- (a) Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi na kununua vitendea kazi katika Idara hiyo? (b) Je, Serikali iko tayari kuwawekea wananchi Wanasheria ili kusaidia kutatua migogoro ya ardhi?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi. Naipongeza Serikali kwa upande wa Morogoro kwa kuanza upimaji wa ardhi hasa kwa upande wa Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga, lakini upimaji unakuta migogoro bado inaendelea kwenye Wilaya nyingine, lakini ni matatizo kweli kwa vifaa vya upimaji kwa sababu vinanunuliwa kwa bei ghali na halmashauri zingine hazina uwezo wa kununua hivyo vifaa. Je, Serikali inasemaje kwa kusaidia hizo Halmashauri ambazo haziwezi kununua hivyo vifaa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipokee shukrani zake kwa Serikali kwa kazi inayofanya katika Wilaya ya Malinyi, Ulanga na Kilombelo, kwa kupima ardhi yote katika maeneo yale na niwashukuru wananchi wa maeneo hayo kwa sababu wamekuwa wakitoa ushirikiano mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumaliza migogoro hiyo kama ambavyo tumeanza ile ni kama pilot area, lakini tayari tutakuwa na resource persons wengi kutokana na wananchi wenyewe kwa sababu pia watakuwa wamepata ujuzi mzuri wa kuweza kufanya scale up kwenye maeneo mengine na lengo la Wizara ni kuhakikisha maeneo yote yanapimwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vifaa vya upimaji, napenda nitoe rai kwa halmashauri zetu zote, Wizara ilikwishatoa vifaa katika maeneo yote ya kanda zetu nane, lakini halmashauri haziendi kuomba vifaa vile. Bahati nzuri kwa kuwa ameuliza hili swali, basi nitatayarisha takwimu niletehapa baada ya kuwa tumeshapata vifaa, ni halmashauri ngapi zimeomba. Halmashauri nyingi hawaendi kuchukua vifaa, lakini wana-opt kutafuta vifaa vya kukodi wakati kuna vifaa vya bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa halmashauri zetu, watumie vifaa hivyo ambavyo Wizara ilishafundisha watumishi wawili, wawili kutoka kila halmashauri kwa nchi nzima ambao wana Wapima kwa ajili ya kuweza kutumia vile vifaa. Matokeo yake wamefundishwa, hawaleti maombi na vifaa vimekaa idle,halafu Wabunge wanalalamikia suala la upimaji. Naomba usimamizi katika halmashauri, watumie vifaa ambavyo tayari Wizara imegharamia.Ahsante.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Kuna uhaba wa watumishi na vitendea kazi katika Idara ya Ardhi na Maliasili – Wilaya ya Muheza kunakosababisha kuazima watumishi na vifaa kutoka Halmashauri nyingine:- (a) Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi na kununua vitendea kazi katika Idara hiyo? (b) Je, Serikali iko tayari kuwawekea wananchi Wanasheria ili kusaidia kutatua migogoro ya ardhi?

Supplementary Question 4

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sanakwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Lupembe katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe haina Afisa Ardhi Mteule na tuna mpango wa kupima ardhi katika maeneo yetu.

Je, ni lini Serikali italeta mtaalam kwa maana ya Afisa Ardhi Mteule ili kuweza kusaidia kupima ardhi lakini pia kutatua migogoro iliyopo? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hongoli kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani wakati najibu swali nyongeza la Mheshimiwa Yosepher, nimesema utaratibu unafanyika sasa tutaweza kuwatawanya wataalam wetu kama walivyo, lakini kwa sasa naomba tu waendelee kumtumia huyo Afisa Ardhi Mteule ambaye alikuwa kazi yote kutoka kwenye halmashauri jirani ya jimbo lake ili tuweze kuendelea. Hii kazi itakamilika muda si mrefu, naomba tu Waheshimiwa Wabunge tuvumiliane kwa sababu kazi ya kuwapanga itachukua muda kwa sababu yakutaka kujua taaluma zao na uhitaji wa kila halmashauri.