Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI alliuliza:- Kata ya Mmale haina mawasiliano kabisa ya simu:- Je ni lini Serikali itawapatia wananchi hao mawasiliano kwa kuweka minara ya mawasiliano katika kata hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya kutia matumaini ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kama nakumbuka Wizara iliahidi kutoa orodha ya vijiji vyote vitakavyotagazwa na kufunga minara katika majimbo yetu nchi nzima. Swali langu ni lini orodha hii tutapatiwa Waheshimiwa Wabunge ili tuwe na nafasi ya kushauri yale maeneo ambayo tunadhani ni muhimu zaidi kupata mawasiliano? Hapo ikiwemo na Bariadi katika Jimbo unalotoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, maeneo mengi service provider hawa wanapenda kujazana katika maeneo ya centers tu, wanakimbia kupeleka minara katika maeneo ya vijiji vyetu ambako ndiyo kuna shida kubwa ya mawasiliano na population ni kubwa sana. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalazimisha service providers kwenda kuweka minara katika maeneo yetu ya vijijini ili wananchi wetu waweze kupata mawasiliano?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Musa Rashid Ntimizi, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyoshughulika kuhakikisha jimbo lake wananchi wanapata huduma ya mawasiliano. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine wote kwamba Serikali inahakikisha kwamba mawasiliano yanapatikana kwa uhakika katika majimbo yote nchi nzima. Hivi navyozungumza nimekwishazungumza tena mara nyingine kwamba tumefikia asilimia 94 ya wananchi kuwasiliana na tutahakikisha kabla ya mwaka ujao kuisha asilimia 100 ya wananchi wa Tanzania wanapata mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la kwanza, Mheshimiwa Mbunge orodha ya mwanzo nitaitoa kesho ya vijiji zaidi ya 600 ambavyo tunategemea kupeleka minara ya mawasialiano kwa ajili ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anataka kujua kwa nini watoa huduma wanarundikana sehemu moja. Kama nilivyowahi kuzungumza hapo awali hawa watoa huduma za mawasiliano ni wafanyabiashara na mfanyabiashara kawaida anatafuta sehemu ambako atapata biashara nzuri, hawawezi kupeleka sehemu ambako hakuna mvuto au ambako wakiwekeza pesa yao haitarudi. Ndiyo maana Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imekuwa ikitoa ruzuku kwa haya makampuni waweze kupeleka mawasiliano mpaka vijijini ambako kabisa wananchi hawawezi kununua huduma za mawasiliano kwa jinsi ambavyo watoa huduma wanataka. Ndiyo maana sasa tumeanzisha Mfuko wa Wawasiliano kwa Wote ili uweze kuziba hilo gap na kufanya wananchi waweze kuwasiliana nchi nzima.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI alliuliza:- Kata ya Mmale haina mawasiliano kabisa ya simu:- Je ni lini Serikali itawapatia wananchi hao mawasiliano kwa kuweka minara ya mawasiliano katika kata hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kama ilivyo Igalula kumekuwa na changamoto kubwa ya mawasiliano kwenye Jimbo la Korogwe Vijijini hususan kwenye Kata za Kizara, Makumba, Kalalani, Mkalamo, Elewa na Lutindi na Mheshimiwa Naibu Waziri anafahamu changamoto hizi. Ni lini Serikali itatoa utatuzi wa changamoto hizi zinazowakabili watu wa Korogwe Vijijini?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikiri kwamba nilishatembelea Korogwe Vijijini na hilo eneo alilolitaja Mheshimiwa Mbunge nililiona, ni kweli kwamba kuna mnara wa mawasiliano lakini hauna nguvu ya kutosha. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba nitatuma wataalam kwanza wakaongeze nguvu kwenye hicho kijiji cha kwanza alichokitaja halafu na nitatoa orodha nyingine kesho aangalie vijiji vingine ambavyo tumeviorodhesha kwa ajili ya kuimarisha mawasiliano maeneo hayo.

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI alliuliza:- Kata ya Mmale haina mawasiliano kabisa ya simu:- Je ni lini Serikali itawapatia wananchi hao mawasiliano kwa kuweka minara ya mawasiliano katika kata hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo Igalula, Jimbo la Ludewa lina eneo kubwa sana ambalo halina mawasiliano ya simu. Hivi karibuni imejengwa minara katika Tarafa ya Mwambao lakini minara ile toka ilipowashwa imeongea kwa siku tatu tu. Sasa nimuulize Mheshimiwa Waziri kuna tatizo gani minara imejengwa imewashwa siku mbili na baada ya hapo mawasiliano hakuna pamoja na ujenzi wa Kijiji cha Ibumi?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Ngalawa, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekwishatembelea Kata ya Mwambao ambayo iko mwambao wa Ziwa Nyasa na nimekwishavitembelea vijiji mbalimbali kuanzia Lupingu, Higa, Makonde ambako kweli kabisa kulikuwa kuna tatizo kubwa sana la mawasiliano. Mheshimiwa Deo ambaye ni mfuatiliaji mkubwa sana wa suala la mawasiliano ni shahidi kwamba ndani ya miezi mitano toka nimetembelea eneo hilo tumekwishaweka minara tisa (9) ya mawasiliano kwa ajili ya wananchi wa eneo la Mwambao. Minara mitatu (3) ambayo sasa hivi haifanyi kazi ilipata hitilafu kidogo na hivi sasa tunapozungumza tumetuma wataalam kutoka Halotel wanakwenda kurekebisha hitilafu hiyo ili wananchi waweze kuendelea kupata mawasiliano.

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI alliuliza:- Kata ya Mmale haina mawasiliano kabisa ya simu:- Je ni lini Serikali itawapatia wananchi hao mawasiliano kwa kuweka minara ya mawasiliano katika kata hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba niulize swali kwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Rombo limekuwa na tatizo kubwa sana la mawasiliano hasa katika kata zilizoko mpakani na ukanda wa juu na Mbunge wa Jimbo hili amekuwa akiuliza maswali mara kwa mara. Je, ni lini tatizo hili litamalizika katika Jimbo hilo la Rombo?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Kiwelu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba siyo Jimbo la Rombo tu maeneo ya mpakani ni karibu majimbo yote ambayo yako mipakani Tanzania kuna tatizo la mwingiliano wa mawasiliano ya simu kutoka nchi jirani. Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekwishawaagiza watoa huduma kwanza kwenda kuongea na majirani zao watoa huduma wa nchi jirani kurekebisha changamoto iliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kulikuwa na utaratibu ambao wenzetu nchi jirani walikuwa wameukiuka ambapo tunaendelea kuufanyia kazi. Sasa hivi eneo la Rombo wako Vodacom na Halotel kwa ajili ya kurekebisha tatizo hil. Eneo la Musoma (Tarime) tumewapeleka Airtel na Tigo kwa ajili ya kurekebisha tatizo hilo. Maeneo ya Bukoba na Kigoma tumewapeleka tena watoa huduma wengine kwa ajili ya kurekebisha tatizo hilo.