Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. SUSAN L. KIWANGA) aliuliza:- Mji Mdogo wa Mlimba unazungukwa na Kata za Chisano, Kalengakelo na Kamwene na zina jumla ya wakazi wasioupungua elfu hamsini na nane ambapo hawana maji kwa matumizi ya nyumbani na kunywa; na kwa kuwa kuna chanzo kikubwa cha maji na Mhandisi wa Halmashauri ameshaleta andiko la mradi wa maji:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za mradi huo ili wananchi hao wapate maji ya kunywa safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nimesikiliza majibu ya Naibu Waziri na kwa kuwa Serikali imepokea andiko hilo, naamini kwamba italichukulia kwa uzito ili kunusuru wananchi hususan akina mama katika Kata za Mlimba na kata za jirani na Jimbo la Mlimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, mkandarasi aliyemaliza Mradi wa Maji Msolwa - Kilombero ambaye hajalipwa fedha zake na Serikali lakini amekubali kuendelea kufanya ujenzi katika Mradi wa Mbingu. Je, Serikali ipo tayari kumlipa fedha zake za awali alizozilimbikiza na anaidai Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kulikuwepo na mpango wa kuongeza kina katika bwawa la Mindu Manispaa ya Morogoro kutokana na maji yaliyopo kutotosheleza wananchi wa Manispaa ya Morogoro. Kwa miaka mitatu sasa Serikali imesambaza mabomba katika Kata za Kiega A na B, Kihonda, Mkundi, je, ni lini itapeleka maji kwa wananchi hao?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge. Mimi nilipata nafasi ya kufika katika jimbo lake lakini kubwa ambalo tumeona tuna changamoto kubwa pale Mlimba lakini tumefanya jitihada ya uchimbaji wa visima lakini bado kumekuwa na changamoto. Tumeona haja sasa ya kutafuta chanzo cha kutosheleza kuhakikisha wananchi wa Mlimba wanapata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu fedha anazodai mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji, tunashukuru sana Wizara ya Fedha ilitupatia kiasi cha shilingi bilioni 44 kwa ajili ya malipo ya wakandarasi. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Wizara ya Maji hatutokuwa kikwazo kumlipa fedha zake kwa wakati ili aendelee kutekeleza mradi na wananchi waweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la maji Manispaa ya Morogoro, kiukweli Morogoro Mjini kuna changamoto ya maji na hii yote imetokana na sababu tu ya ongezeko la watu na hata shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Sisi kama Wizara ya Maji tumefanya jitihada kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha kufanya mazungumzo na Serikali ya Ufaransa kwa ajili ya uwekezaji wa fedha kwa maana ya utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha. Zaidi ya Euro milioni 70 zitakazopatikana zitawekezwa katika Mji ule wa Morogoro ili kuhakikisha tunaongeza kina cha Bwawa la Mindu ili wananchi wa Morogoro waweze kupata maji safi, salama na yenye kutosheleza. Sisi kama Wizara ya Maji tutafanya jitihada za haraka ili jambo hili liweze kutekelezeka na wananchi wa Morogoro waweze kunufaika na huduma hii muhimu. Ahsante sana.

Name

Mboni Mohamed Mhita

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. SUSAN L. KIWANGA) aliuliza:- Mji Mdogo wa Mlimba unazungukwa na Kata za Chisano, Kalengakelo na Kamwene na zina jumla ya wakazi wasioupungua elfu hamsini na nane ambapo hawana maji kwa matumizi ya nyumbani na kunywa; na kwa kuwa kuna chanzo kikubwa cha maji na Mhandisi wa Halmashauri ameshaleta andiko la mradi wa maji:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za mradi huo ili wananchi hao wapate maji ya kunywa safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mradi wa Maji Handeni pamoja Korogwe yaani Handeni Trank Main ambao tuliahidiwa kuwemo katika miradi ya miji 28 ambayo inategemea fedha kutoka Serikali ya India na naamini kwamba fedha hizo tayari zimepatikana. Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi huu ili wananchi wa Jimbo la Handeni Vijijini waweze kupata maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, dada yangu Mboni amekuwa mpiganaji mkubwa sana hususani katika suala zima la maji katika Jimbo lake la Handeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tulipata nafasi ya kutembelea katika jimbo lake na tumeona kabisa hii changamoto. Ndiyo maana Wizara yetu ya Maji tukaona katika miji hiyo 28 ambayo inatakiwa ipatiwe maji haraka ni mmojawapo ni Jimbo lake la Handeni. Nataka nimhakikishie sasa hivi tupo katika hatua ya kumpata Mhandishi Mshauri na mkadarasi ndani ya mwezi Septemba atakuwa amekwishapatikana na miradi hii itatekelezwa katika maeneo yote ili kuhakikisha tunamtua mwanamama ndoo kichwani.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. SUSAN L. KIWANGA) aliuliza:- Mji Mdogo wa Mlimba unazungukwa na Kata za Chisano, Kalengakelo na Kamwene na zina jumla ya wakazi wasioupungua elfu hamsini na nane ambapo hawana maji kwa matumizi ya nyumbani na kunywa; na kwa kuwa kuna chanzo kikubwa cha maji na Mhandisi wa Halmashauri ameshaleta andiko la mradi wa maji:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za mradi huo ili wananchi hao wapate maji ya kunywa safi na salama?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyikiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri amefika Jimbo la Mbuli Vijijini na ameona changamoto iliyopo hapo inayofanana na Jimbo la Mlimba. Mheshimiwa Naibu Waziri aliahidi kisima kichimbwe Hyadom na tumeomba shilingi milioni 80 na akaahidi itatumwa. Je, ni lini sasa atatupatia fedha za kuchimba kisima pale Hyadom?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri sana anayofanya katika jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilifika pale Hyadom tumeona kuna mradi mkubwa lakini katika kuhakikisha tunawaongezea chanzo kwa maana ya uzalishaji tukaona kuna haja ya uchimbaji wa kisima. Sisi tuna Wakala wa Uchimbaji Visima (DDCA), kwa hiyo, niwaagize wachimbe kisima kile haraka ili wananchi wa Hyadom waweze kupata ongezeko la maji na waweze kupata huduma hii muhimu.