Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA (K.n.y. MHE. RUKIA AHMED KASSIM) aliuliza:- Kuna baadhi ya wanawake wameathirika sana na matumizi ya dawa za kuongeza makalio pamoja na matumizi ya kope na kucha bandia:- Je, Serikali ipo tayari kufungia saloon zote pamoja na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaotoa huduma hii?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza imeelezwa kwamba TFDA ndiyo Mamlaka ambayo inashughulikia chakula na dawa, lakini kwa hali ya uhalisia TFDA yenyewe capacity yake ni ndogo sana ya kuweza kupima vinasaba vyote Tanzania nzima kwa sababu Ofisi yao Kuu iko pale Dar es Salaam na wana vifaa vichache sana.

MWENYEKITI: Uliza swali.

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, je, ni lini Serikali itaiongezea vifaa TFDA iweze kufanya kazi yake sawasawa nchi nzima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna dawa pia ambazo inasemekana na wataalam wa afya, kwamba zinapelekea kuharibu miili ya binadamu na hasa zile dawa za kufanya rangi ya watu weusi iweze kuwa nyeupe, je, Serikali imechukua hatua gani mpaka hivi sasa ili kuwafanya Watanzania wengi wanaotumia dawa hizi wasiweze kupata madhara?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA (K.n.y. WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maftaha kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimhakikishie kwamba uwezo wa TFDA sio mdogo kama anavyodhani, Taasisi hii ni kubwa, ina Maabara ya kisasa sana pale Dar es Salaam lakini pia imeanza kujenga uwezo Kikanda na sio kwamba wanafanya kazi Dar es Salaam peke yake, wako katika Kanda mbalimbali katika nchi yetu, na wana maabara inayotembea, (mobile lab) kwa maana hiyo nadhani uwezo wao ni mzuri na wataendelea kuuboresha ili kuweza kufika nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili la dawa ambazo zinasababisha au tunaziita hizi dawa za kujichubua, ili watu wabadilike rangi zao, hili napenda nimwarifu Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, kwamba TFDA imekuwa ikichukua hatua mara nyingi sana. Dawa nyingi sana zimeshaondolewa kwenye soko zenye madhara haya na hizi mara nyingi ni dawa ambazo zina maada inayoitwa steroid ambazo kwa kweli zinaharibu ngozi na zinaweza kusababisha madhara makubwa, zimekuwa zikiondolewa na wahusika wamekuwa wakipigwa faini na kwa maana hiyo sasa hivi kuna udhibiti mzuri sana wa dawa zinazosababisha madhara haya.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA (K.n.y. MHE. RUKIA AHMED KASSIM) aliuliza:- Kuna baadhi ya wanawake wameathirika sana na matumizi ya dawa za kuongeza makalio pamoja na matumizi ya kope na kucha bandia:- Je, Serikali ipo tayari kufungia saloon zote pamoja na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaotoa huduma hii?

Supplementary Question 2

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la matumizi ya dawa za nguvu za kiume, enzi zenu nakumbuka kulikuwa na mkuyati, lakini sasa hivi, kuna super moringe, mundende, super gafina, gasosi mix, super shafti, sado power, amsha mzuka, Kongo dust na hii Kongo dust imeonesha kuwa mafanikio makubwa. Je, Serikali imeshafanya utafiti nini kinasababisha tatizo hili la watu kutokuwa na nguvu za kiume kupelekea kutumia sana hizi dawa?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA (K.n.y. WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mlinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu zinazopelekea kupungua kwa nguvu za kiume ni nyingi, ikiwemo magonjwa mbalimbali kama vile kisukari, msongo wa mawazo na kadhalika, kwa hiyo kuna sababu nyingi zinazopelekea matatizo haya na ndio maana watu wengi wamekuwa wakitafuta ufumbuzi wa tatizo hilo. Ninachoweza kusema hapa ni kwamba ziko dawa zenye maada ambazo sio za kikemikali, ambazo ni bora zaidi zitumike kuliko kemikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili kama nilivyosema awali TFDA wanao uwezo wa kubaini ni dawa gani ambazo zinasababisha madhara na zile ambazo zinasababisha hakuna budi kutolewa taarifa mapema ili ziweze kuondolewa kwenye soko, lakini tunatambua kwamba sasa hivi kuna dawa zilizopitishwa na Mamlaka za Udhibiti ambazo zinauzwa kihalali kabisa za kuweza kuongeza nguvu za kiume na ambazo hazijaripotiwa kuwa kuna matatizo kama ya athari zinazopelekea kutokana na matumizi ya dawa hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wetu ni kwamba wanaotaka kutumia dawa hizi waendelee kutumia zile ambazo zimethibitishwa kitaalam na wasitumie zile ambazo hazina uthibitisho ili wasiweze kupata madhara.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA (K.n.y. MHE. RUKIA AHMED KASSIM) aliuliza:- Kuna baadhi ya wanawake wameathirika sana na matumizi ya dawa za kuongeza makalio pamoja na matumizi ya kope na kucha bandia:- Je, Serikali ipo tayari kufungia saloon zote pamoja na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaotoa huduma hii?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na wimbi kubwa la wanaume na vijana kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume, sasa hivi kuna baadhi wanatumia dawa za kukuza maumbile ya kiume, nataka kujua nini madhara yake na ni kwa nini wanafanya hivi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA (K.n.y. WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Susan Lyimo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na taarifa nyingi za dawa zinazoweza kukuza maumbile na wito wangu ni kwamba, watu waendelee kuhakikisha kwamba hawatumii dawa yoyote ambayo haijasajiliwa, haijathibitishwa kitaalamu kwa sababu inaweza ikasababisha madhara na wale ambao wanatoa taarifa hizi bila ya uthibitisho kwa kweli wanafanya kosa na wanatakiwa wachukuliwe hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa nilizokuwa nazo ni kwamba hakuna dawa yoyote ambayo kitaalam imethibitishwa na imepewa kibali kwa ajili ya matumizi kama hayo. Kwa hivyo nawaomba Watanzania wawe makini wanapotaka kununua dawa kama hizi kwa sababu zinaweza zikawa zina madhara. Tungependa wananchi watoe taarifa endapo wamewahi kutumia na wamepata madhara yoyote ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.