Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Uwepo wa madini ya chokaa umedhihirika katika Kijiji cha Ausia, Kata ya Suruke, Jimbo la Kondoa Mjini, kwa muda mrefu sasa, katika jitihada za kujaribu kunufaika wananchi wamekuwa wakichimba madini haya kienyeji:- Je, ni lini Serikali itapeleka Wataalam kufanya utafiti kubaini kiwango cha uwepo na ubora wa madini hayo ya chokaa ili wananchi wa maeneo hayo waanze kunufaika sasa na rasilimali hiyo muhimu?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nipongeze majibu mazuri ya Serikali kutoka kwa Naibu Waziri. Pamoja na majibu mazuri hayo, basi nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, ripoti hii ya utafiti wa awali sisi kama watu wa Ausia na kule Kondoa hatuna, kwa hiyo hata kuweza kujua kuna kiwango cha chokaa kiasi gani imekuwa ni mtihani na ukizingatia kwamba madini haya ni muhimu sana katika kazi za ujenzi, sasa tunataka kujua, ni hatua gani na wao kama Serikali watatusaidia ili twende kwenye utafiti wa kina tuweze kujua madini kiasi gani yapo kule tuendelee na hatua ya pili ya kupata mwekezaji na hatimaye kuanza kunufaika na uwepo wa madini hayo? Hilo ni la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ili Mheshimiwa Naibu Waziri akajiridhishe na hali halisi iliyoko pale akifika site, je, anaonaje sasa mimi na yeye pamoja na wataalam wake wa Wizara tukaongozana tukaenda site tuweze kuharakisha mchakato huu wa wananchi wa Kondoa Mjini waweze kunufaika na madini haya ambayo yanaonekana yako kwa wingi.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Edwin , Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru sana Mheshimiwa Sannda kwa kazi nzuri anayoifanya kwa wananchi wa Kondoa, wananchi wa Kondoa nadhani watamtazama tena hapo mwakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu ni kwamba, alichokisema na majibu yangu ya msingi nilivyosema ni sawa, Wizara yetu kupitia GST tunafanya tafiti za kina kupitia zile QDS yaani Quarter degree sheets, tunafanya kitu wanaita Geophysical Survey ambayo inatambua uwepo wa madini katika maeneo hayo na kwa kweli kwa nchi nzima tuna ramani inayoonyesha uwepo wa madini na kila sehemu ni madini gani yako katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa utafiti wa kina ambayo ni geochemistry ambayo inafanywa mara nyingi na mwekezaji mwenyewe. Anakwenda anafanya utafiti wa kina kujua deposit iliyopo pale na kama deposit hiyo anaona yeye inaweza ikamlipa, ikawa economical, sasa hatua ya pili ya kuomba leseni ya uchimbaji, anakuja kuomba kwetu na tunampatia kwa ajili ya uchimbaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba utafiti wa kina umeshaonesha madini katika maeneo niliyoyataja na sasa hivi tunakaribisha wawekezaji wengi waje wawekeze kwa sababu utafiti wa kina unahitaji fedha nyingi.

Kwa hiyo sasa hivi tunaweka mahusiano mazuri na maeneo mbalimbali kwa mfano jana nimepokea ugeni kutoka China, wao wanataka kutusaidia kufanya tafiti za kina kuweza kutambua maeneo na deposit zilizopo katika maeneo mbalimbali ili kuweza kuwasaidia wachimbaji kuwapa taarifa za kijiolojia na waweze kwenda kuwekeza maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ameuliza kwamba niko tayari kwenda Kondoa na wataalam, mimi nimweleze tu ni kwamba niko tayari, tunaweza tukaenda Kondoa na niko tayari muda wote na wataalam wapo, lakini pale panapohitajika tutaweza kubeba timu ya wataalam kwenda nayo, lakini kwa kufika pale na kujionea niko tayari wakati wowote.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Uwepo wa madini ya chokaa umedhihirika katika Kijiji cha Ausia, Kata ya Suruke, Jimbo la Kondoa Mjini, kwa muda mrefu sasa, katika jitihada za kujaribu kunufaika wananchi wamekuwa wakichimba madini haya kienyeji:- Je, ni lini Serikali itapeleka Wataalam kufanya utafiti kubaini kiwango cha uwepo na ubora wa madini hayo ya chokaa ili wananchi wa maeneo hayo waanze kunufaika sasa na rasilimali hiyo muhimu?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba niishukuru Serikali sana kwa kazi nzuri inayofanya ya kufanya utafiti wa awali ili kuchora ramani za kijiolojia. Hata hivyo, napenda niikumbushe Serikali kwamba iliahidi kuwasaidia wachimbaji wadogo kwa kuwafanyia utafiti wa kina maana yake minor exploration kwa kupitia STAMICO. Ni lini basi Serikali itafanya kwa sababu wachimbaji wadogo hawana huo mtaji wa kufanya huo utafiti wa kina kwa ajili ya uchimbaji wakiwemo hao wachimbaji na wanaotafuta madini ya chokaa kule Kondoa. Ahsante sana.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kafumu, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa, Serikali ilitoa ahadi kuwasaidia wachimbaji wadogo kufanya tafiti mbalimbali na hasa tafiti za kina, kuweza kujua kuna kiasi gani cha madini katika maeneo mbalimbali na madini tofauti mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanza tu STAMICO tayari imekwishanunua mtambo wa ku-drill yaani drilling machine kwa ajili ya kuweza kufanya tafiti za kina. Mtambo huo kwa kweli tayari upo na tumekwishaanza kufanya tafiti mbalimbali maeneo mbalimbali na niwaase tu wale wachimbaji wadogo ambao wanahitaji huduma hiyo wanaweza sasa hivi wakaleta mahitaji yao au maombi yao katika Shirika letu la Taifa, yaani STAMICO kwa ajili ya kufanyiwa hizo exploration.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tutaendelea kununua mashine mbalimbali ambapo tunaweza sasa tukaendelea kufanya tafiti za kina na kuweza kuwasaidia wachimbaji wadogo kwa sababu tunatambua uchimbaji wao wa kubahatisha ambao unawatia hasara, wengine wanapoteza fedha nyingi kwa sababu ya kwenda kubahatisha. Uchimbaji wa kubahatisha unasababisha umaskini mkubwa. Ahsante sana.