Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Barabara ya kutoka Kinyanambo A – Isalavamu – Igombavanu – Sadani hadi Madibira ilikuwepo kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2005 – 2010 na 2010 – 2015 lakini hadi sasa haijajengwa kwa kiwango cha lami:- (a) Je, ni sababu zipi zilizofanya Serikali kutoanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa uchumi wa Wilaya za Mbarali na Mufindi? (b) Je, ni lini sasa ujenzi wa barabara hiyo utaanza? (c) Je, ni lini Serikali itaanza uthamini kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi wanaopisha ujenzi wa barabara hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, alipokuwa kwenye ziara yake Wilaya ya Mufindi alisema ahadi ni deni na hii barabara ni ya muda mrefu. Akaahidi kwamba hii barabara itajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa Wilaya ya Mufindi na Rujewa na ni short-cut kwa wasafiri wanaotoka Mbeya. Nini commitment ya Serikali, lini wataanza kujenga barabara hii hata kwa kilometa mbili-mbili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuja Wilaya ya Mufindi kukutana na wananchi wote waliopo kandokando ya barabara hii kusudi uweze kuwaambia hatma ya tathmini na malipo yao?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mgimwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mgimwa kwa sababu anafuatilia kweli siyo barabara hii tu peke yake lakini pia barabara inayoenda kumuunga kule Kihansi na kila wakati yuko Wizarani kufuatilia barabara hii. Kwa hiyo, nampongeza sana naamini kwamba wananchi wa Mafinga hawakukosea kumpa nafasi ya Ubunge.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba ahadi ni deni ni kweli na ndiyo maana tumeendelea kuiwekea kipaumbele barabara hii ili tuweze kujenga kwa lami. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mgimwa nakubaliana na wewe lakini tatizo ni fedha, tukipata fedha tutaendelea kupunguza kwa maana ya kujenga kwa awamu kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kwamba kadiri tunavyopata fedha tutaendelea kujenga barabara hii muhimu kwa sababu inapita maeneo ya uzalishaji mkubwa wa mpunga kule Mbarali.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kutembelea eneo hili, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge mara baada ya Bunge hili nitatembelea eneo hili ili kuweza pia kuwahakikishia wananchi wa Tarafa hii ya Sadani na maeneo mengine kwamba tumejipanga kuwaletea barabara ya lami lakini pia kuwalipa fidia ili kupisha mradi huu muhimu. Ahsante.

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Barabara ya kutoka Kinyanambo A – Isalavamu – Igombavanu – Sadani hadi Madibira ilikuwepo kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2005 – 2010 na 2010 – 2015 lakini hadi sasa haijajengwa kwa kiwango cha lami:- (a) Je, ni sababu zipi zilizofanya Serikali kutoanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa uchumi wa Wilaya za Mbarali na Mufindi? (b) Je, ni lini sasa ujenzi wa barabara hiyo utaanza? (c) Je, ni lini Serikali itaanza uthamini kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi wanaopisha ujenzi wa barabara hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami napenda niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nimekuwa nikisimama mara kwa mara nikimuomba Waziri atujibu ni lini wataleta pesa na kujenga barabara ya kilometa 142 kutoka Dumila – Kilosa mpaka Mikumi ambayo kwa sasa imejengwa kuanzia Dumila mpaka Ludewa na bado kilometa 21 Ludewa – Kilosa? Kila siku nimekuwa nikijibiwa kwamba tuko kwenye upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na vitu kama hivyo. Wananchi wa Kilosa wanataka kujua ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii muhimu kwa uchumi wao?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Haule, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara hii muhimu inayotoka Dumila - Kilosa, inapita maeneo ya Ulaya mpaka Mikumi, niseme tu kimsingi barabara hii imeanza kujengwa lakini tunaenda kwa awamu. Mheshimiwa Mbunge unafahamu eneo hili la Ludewa – Kilosa ambalo sasa tuna mpango wa kujenga kwa kiwango cha lami na katika bajeti inayokuja kipande hiki tutaanza kujenga ili tupunguze uelekeo wa kwenda Mikumi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikuombe tu Mheshimiwa uvute subira, tumejipanga na tunaendelea kujenga kama unavyofahamu ili kuweza kuwaunganisha wananchi hawa wa Mikumi. Hii njia kwa kweli ni fupi, itapunguza gharama na muda lakini pia inapita maeneo muhimu ya uzalishaji na utalii kwenye maeneo yetu ya Mikumi. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Barabara ya kutoka Kinyanambo A – Isalavamu – Igombavanu – Sadani hadi Madibira ilikuwepo kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2005 – 2010 na 2010 – 2015 lakini hadi sasa haijajengwa kwa kiwango cha lami:- (a) Je, ni sababu zipi zilizofanya Serikali kutoanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa uchumi wa Wilaya za Mbarali na Mufindi? (b) Je, ni lini sasa ujenzi wa barabara hiyo utaanza? (c) Je, ni lini Serikali itaanza uthamini kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi wanaopisha ujenzi wa barabara hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri tuliambatana naye mpaka Kipiri Port. Sasa namuuliza lini usanifu wa barabara ya Namanyere – Kipiri Port utaanza?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Keissy, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli nimetembelea eneo la Kipili, Mheshimiwa Mbunge anafahamu yapo mambo mengi, nimpongeze tu kwa kweli kwa ufuatiliaji wake kwa sababu hata hii Bandari ya Kipili kule iko vizuri, tumeona maendeleo mazuri lakini uko umuhimu sasa wa kuunganisha kwamba tunakuwa na bandari nzuri lakini tunahitaji pia tuwe na barabara nzuri ya kuwapeleka wananchi katika maeneo hayo. Tumeona pia kuna uchumi mzuri, kuna samaki wanavuliwa maeneo yale wananchi hawa wanahitaji hii barabara.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Keissy, kama tulivyojipanga katika mwaka huu wa fedha tuliitengea fedha kwa ajili ya usanifu, harakati za awali zinaendelea, lakini katika mwaka unaokuja pia tutaweka mapendekezo ya fedha,ili tukamilishe usanifu na tuweze kuanza kujenga kipande hiki cha barabara kilometa kama 72 hivi kwa kiwango cha lami. Ahsante.