Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELSTER A. BURA aliuliza:- Mkoa wa Dodoma una upungufu wa Walimu 527wa Sayansi:- Je, ni lini Serikali italeta Walimu wa kutosha wa sayansi?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, kama uhitaji wa Walimu wa Sayansi kwa Mkoa wa Dodoma ni 916. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba uhitaji wa Walimu wa Sayansi ambao ndio Madaktari na Wahandisi na Wauguzi unakamilika kwa kuwaajiri Walimu wanaotesheleza mahitaji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, pamoja na uhitaji mkubwa wa Walimu wa Sayansi kwa shule za sekondari, kuna uhitaji mkubwa wa Walimu wa shule za msingi. Kwa mfano, Wilaya ya Kongwa kuna uhitaji wa Walimu 1,088; Chemba, Walimu 786; Kondoa, Walimu 618; Dodoma Jiji, Walimu 656, hapo ni Wilaya nne tu nimezitolea mfano. Je, ni lini sasa Serikali itaamua sasa kuwaajiri Walimu wa shule ya msingi kwa sababu elimu ya msingi ni kujenga msingi wa mwanafunzi, Je, Serikali iko tayari kuwaaajiri Walimu wa kutosha pamoja na halmashauri zetu kujenga miundombinu, Jiji wamepanga bilioni 8.3 kwa ajili ya kujenga miundombinu kwa ajili ya shule za msingi na sekondari. Je, serikali iko tayari sasa kuwaajiri na Walimu wa shule za msingi ili kukidhi mahitaji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Felister Bura, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli swali lake la kwanza anauliza upungufu mkubwa Walimu na naomba nikiri kwamba ni kweli kwamba tuna uhitaji mkubwa sana wa Walimu wa Hesabu na Sayansi, takribani nchi nzima na Wilaya zote na Wahesimiwa Wabunge wote hawa ukiona wanapiga makofi wanazungumza hilo. Hii ni ajira ya awamu ya kwanza, bado tathimini ile ya Walimu hewa na wengine, hii tumeomba kibali kupata Walimu 8,500 kama nilivyosema, lakini tunatarajia kupa kibali kingine mwezi wa Tano au wa Sita ambao watakuwa wengi zaidi ya hawa. Kwa kweli makusudi yetu ni kulenga kuajiri Walimu wengi wa Hesabu na Sayansi, lakini kama nilivyosema pale ambapo wana mahitaji makubwa sana, kwa mfano, unakuta kuna shule haina Mwalimu wa Hesabu, haina Mwalimu wa fizikia na kemia tutazingatia maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi wakati tunapeleka Walimu hawa katika shule zetu za sekondari.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ameuliza ajira ya Walimu wa shule za msingi. Katika hao niliowataja Walimu 4,500 nimesema 1,300 ni masomo ya sayansi na hisabati, maana yake Walimu 3,200 wanaobaki wote hawa ni Walimu wa shule ya msingi pamoja na Walimu wa watoto wenye mahitaji maalum. Kwa hiyo, tutazingatia kupeleka pia na Walimu wa shule za msingi katika maeneo mbalimbali ambayo yana upungufu mkubwa. Tumefanya mawasiliano na Waheshimiwa Wabunge, wanafahamu, tutalizingatia, lakini tukipata kibali mwezi wa Tano kama nilivyosema au wa Sita tutazingatia maeneo gani ya kwenda.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna upungufu mkubwa, lakini tuna maelekezo mengine ambayo kama kutakuwa kwa mfano kwenye vibali vya muda, tukianza kutangaza nafasi unakuta pia inakuwa ni pungufu. Tumetoa vibali vya muda, Walimu ambao wamesoma masomo ya sayansi na hesabu lakini sio Walimu wanapata mafunzo ya muda mfupi ili waweze kuziba gape hili la Walimu wa Sayansi na Hisabati. Ahsante.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. FELSTER A. BURA aliuliza:- Mkoa wa Dodoma una upungufu wa Walimu 527wa Sayansi:- Je, ni lini Serikali italeta Walimu wa kutosha wa sayansi?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nasema tu kwamba Wilaya ya Kilombero na hasa kutokana na miundombinu yake ina upungufu wa Walimu 1,018 na sio wa sayansi tu, wa kada zote. Kwa mfano, Jimbo la Mrimba unakuta shule ina Walimu watatu lakini ina wanafunzi 800 au 1,000. Je ni lini sasa Serikali katika hawa Walimu wanaosema wanawaajiri sasa hivi watatupelekea Walimu kwenye Wilaya ya Kilombero, ikiwemo na wanawake kwa sababu kuna shule haina Mwalimu mwanamke hata mmoja. Sasa wale watoto wanaokuwa wakamuone nani? Kwa hiyo, ni lini sasa mtapeleka walimu hususan Jimbo la Mrimba ili watoto wale waendelee kukua wakiwa na chakula cha akili? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Suzan Kiwanga, Mbunge wa Mrimba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tumeshatoa maelekezo zile shule ambazo zina Walimu wa kike peke yake au wa kiume peke yake ni lazima wachanganywe. Hii kwa kweli ni kazi ambayo inafanywa ndani ya Wilaya na Mkurugenzi mwenyewe kwani ana uwezo kupata taarifa na Mheshimiwa Mbunge anawasiliana naye halafu wanawabadilisha ndani, kama ni Mwalimu kutoka nje ya mkoa mwingine hilo ndio unakuja ngazi ya TAMISEMI. Kwa hiyo, nadhani hilo lifanyike na ningepeda kueleza kwa kweli itakuwa sio sawasawa kama kuna shule ina Walimu wa kiume tu na shule ile ni mchanganyiko. Kwa hiyo, naomba nitoe maelekezo kwa Wakurugenzi wote na Maafisa Elimu wa Mikoa na Makatibu Tawala, hili jambo walifanyie kazi sio zaidi wiki mbili kwa sababu inawezekana na ndani ya mazingira yao.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyozungumza, ajira hizi ambazo tumetangaza tutazingatia maeneo ambayo yana upungufu mkubwa na tuliomba Mheshimiwa Mbunge anajua kuna shule ambayo, shule za msingi inawezekana kwamba unaweza ukawa na Walimu wachache kwa sababu wanafundisha masomo mengi kwa wakati mmoja, lakini sekondari lazima kila mtu ana somo lake au masomo mawili ambayo anafundisha, haya maeneo ambayo yana changamoto kubwa na tutahakikisha kwamba tunapeleka Walimu katika maeneo haya. Ndiyo maana tumezuia pia na uhamisho, labda niliseme hili, kwa maana kwamba kuna maeneo ya halmashauri kwa sababu yana mazingira magumu, watu wamekuwa na sababu nyingi sana za kuwahamisha na kuomba uhamisho.

Mheshimiwa Spika, maelekezo yametoka kwa Serikali kwamba tusimamishe uhamisho kwanza wa Walimu nchi nzima ili tutengeneze mifumo ambayo, anapoomba uhamisho kwa sababu yoyote ile hata kama ni mgonjwa, kumfuata mume wake au mke wake au vyovyote itakavyokuwa tujue je, anapotoka kule Kaliua, Mrimba, Kilosa anapooenda kule balance ikoje kule ya Walimu, kwa maana ya kuangalia ikama hiyo. Kwa hiyo, tumelichukua hatua hiyo baada ya kugundua kwamba kuna maeneo wanakimbia mazingira magumu ya kazi, wanaenda sehemu ambayo kuna unafuu, anapaswa kufundisha mahali popote kulingana na mkataba wake wa kazi. Ahsante.