Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Ujenzi wa Barabara ya Makofia-Mlandizi-Vikumburu kwa lami ni ahadi ya Ilani ya CCM tangu mwaka 2010, na kwa sababu upembuzi yakinifu na usanifu wa barabara hiyo umekamilika:- Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu haya mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kutambua kwamba hii ni ahadi ya chama chetu ya muda mrefu tangu Ilani ya mwaka 2010, huu ni mwaka wa tisa na sasa usanifu umekamilika, je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kwamba ni muafaka sasa kwa kipande kile cha Makofia hadi Mlandizi ambacho usanifu wake umekamilika kuanza taratibu za ujenzi mapema iwezekanavyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa sababu hivi sasa usanifu umekamilika na wananchi hawa walikuwa wanasubiri fidia ya maeneo yao tangu kipindi ambapo barabara hii ilitangazwa kujengwa kwa maana ya takribani imefika miaka tisa. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwalipa fidia wananchi hawa kutoka Makofia hadi Mlandizi mpaka Vikumburu ili waweze kupisha ujenzi wa muundombinu huu muhimu kwa furaha?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shukuru Jumanne Kawambwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Kawambwa kwa sababu nafahamu amekuwa akifuatilia sana barabara nyingi za Mji wa Bagamoyo, ikiwemo barabara hii ya Makofia-Mlandizi lakini pamoja na barabara nyingine ambazo zinaunganisha Mji wa Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la kwanza, ni kweli kwamba barabara hizi alizozitaja, ukiichukua kutoka Bagamoyo - Mlandizi - Kisarawe ziko kilometa 100, lakini kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi kwamba kazi kubwa imeshafanyika na sasa tunakamilisha kufanya mapitio ya compensation (fidia) kwa wananchi ambao watapisha mradi huu. Kama ilivyo kanuni, tukishawalipa wananchi hawa sasa tutakuwa na haki ya kuanza kuenga kipande hiki cha barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimtoe hofu tu Mheshimiwa Dkt. Kawambwa kwamba kipande cha barabara hiyo kutoka Makofia mpaka Mlandizi kilometa 36.7 sasa tunakamilisha. Tathmini ya awali ilionyesha kama fidia ya shilingi bilioni 11 au 12, hivi sasa Mtathmini anafanya review ili tuweze kuwa na uhakika wa kiasi gani wananchi hawa wanastahili ili tuwalipe tuanze kujenga kipande hiki.

Mheshimiwa Spika, lakini niseme tu kwamba kwa sababu barabara hii inaunganisha vipande viwili, kile cha kutoka Kisarawe - Mlandizi, kile kipande cha kutoka Kisarawe - Maneromango kama kilometa 10, hivi sasa ujenzi unaendelea. Kwa hiyo, niseme tu kwa ujumla wake kwa wananchi wa Bagamoyo na Pwani kwa ujumla kwamba barabara hii yote kwa ujumla wake ujenzi tumeshaanza na tukilipa fidia pia kipande cha kutoka Mlandizi - Bagamoyo tutaanza kukijenga ili wananchi waweze kunufaika na matokeo makubwa ya kazi nzuri ya Serikali yao.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Ujenzi wa Barabara ya Makofia-Mlandizi-Vikumburu kwa lami ni ahadi ya Ilani ya CCM tangu mwaka 2010, na kwa sababu upembuzi yakinifu na usanifu wa barabara hiyo umekamilika:- Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nangurukuru-Liwale ni muhimu sana kwa wakazi wa Liwale, lakini siyo hivyo tu ni barabara iliyoahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015-2020. Je, Serikali inawaambia nini wana Liwale juu ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimpongeze tu Mheshimiwa Kuchauka kwa sababu namfahamu amekuwa akiifuatilia sana barabara hii, ni kilometa 230 kutoka Nagurukuru - Liwale. Niwahakikishie tu wananchi wa Liwale kwa ujumla wake, maana walikuwa wanajiona kama wako Kisiwani. Mheshimiwa Kuchauka anafahamu tunatoka Nachingwea, kilometa 129 kuja Liwale na tuko kwenye hatua ya usanifu. Namwomba Mheshimiwa Mbunge asiharakishe tu shughuli, tutakuja na pendekezo kwenye bajeti yetu inayokuja kwa ajili ya kusanifu barabara hii ya kutoka Nangurukuru - Liwale.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niliombe tu Bunge lako tutakapokuja na pendekezo hilo watupitishie ili twende kusanifu barabara hii ya Mheshimiwa Mbunge Kuchauka na hatimaye tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ahsante.