Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AZZA H. HAMAD aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji katika Kijiji cha Ishilolo, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga?

Supplementary Question 1

MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini sasa naomba nimuulize Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Serikali ipo tayari sasa kuipa kipaumbele Skimu ya Umwagiliaji ya Ishololo ili iweze kuleta tija kwa wakulima wetu mara itakapokuwa imepata fedha?

Mhesimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini Serikali itachimba bwawa katika Skimu ya Umwagiliaji ya Nyida ambayo imekuwa ikitegemea maji ya mto ambao ni wa muda?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Azza Hillal Hamad, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Azza Hillal kwa kuonesha uongozi kwa mfano. Tunamfahamu ni mdau wetu mzuri katika sekta ya kilimo, ni mkulima mkubwa wa mpunga, anawaongoza watu wake wa Shinyanga yeye mwenyewe kwa kuwa mbele na wale wanaoongozwa kuwa nyuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza kujibu swali lake la nyongeza la kwanza, nimhakikishie kwamba Serikali ipo tayari kuipa kipaumbele hii Skimu ya Ishololo pale ambapo tutaanza kupata pesa. Kama nilivyosema kwenye majibu yetu ya awali, tumeshaanza mazungumzo na wadau wetu mbalimbali ikiwemo Serikali bya Japan kupitia Shirika lake la JICA.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili kuhusu suala la ujenzi wa bwawa katika hii Skimu ya Nyida, nimhakikishie Mheshimiwa Azza Hillal Serikali inafahamu na ipo katika mipango mikakati yetu kwa miradi yote ile inayotumia maji katika mito ambayo ni ya msimu kuijengea mabwawa ukiwemo huu wa Nyida ili tuweze kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuleta kilimo chenye tija, chenye manufaa kwa wakulima wetu.