Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 1

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naipongeza Serikali kwa hatua ambayo imechukua kuweza kuhakikisha kwamba kuna mradi wa maji wa kutoka Ziwa Victoria, Katoro, Buseresere. Wananchi wanahitaji kujua ni lini utekelezaji utaanza rasmi?

Swali la pili; kwa kuwa azma ya Serikali mpaka mwaka 2020 ni kuhakikisha kwamba mijini asilimia 95 ya maji, asilimia 85 vijijini, jambo ambalo nikiangalia hali halisi, kwa mfano katika Mkoa wa Geita Jimbo la Busanda, naona hali iko chini sana. Napenda kujua sasa kwamba nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunapata maji kwa asilimia 85 katika Jimbo Busanda na asilimia 95 Mji wa Geita ambapo sisi wananchi wote ni Makao Makuu ya Mkoa wetu wa Geita?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nampongeza sana Mheshimiwa Lolesia kwa kazi nzuri sana ya kuwapigia wananchi wake. Kubwa, tunatambua kabisa maji hayana mbadala. Ndiyo maana sisi kama Wizara ya Maji tumefanya jitihada ya kuwasilisha hili andiko kwa Wizara ya Fedha ili waweze kuwasilisha EIB. Wizara ya Maji itafanya ufatiliaji wa karibu katika kuhakikisha jambo hili linakamilika kwa wananchi wake ili mradi uweze kuanza kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha azma ya Mheshimiwa Rais ya kumtua mwanamama ndoo kichwani na kutimiza Ilani ya Chama cha Mapinduzi asilimia 85 ya upatikanaji wa maji vijijini na asilimia 95 ya upatikanaji mijini, tumeshakamilisha miradi zaidi ya mitatu katika Jimbo lake. Moja, Nyakagongo, Luhuha pamoja na Mharamba katika kuhakikisha wananchi wale wanapata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati uliokuwepo sasa hivi ni katika kuhakikisha tunakamilisha mradi wa zaidi ya shilingi bilioni nne wa Nachankorongo ili mradi ule ukamilike kwa wakati na umeshafikia zaidi ya asilimia 90 upo katika muda tu wa matazamio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa na la msingi kabisa, sasa hivi tunakamilisha mradi wa Lamugasa na tunajenga mradi wa maji Nkome, Nzela ambao ni wa zaidi ya shilingi bilioni 25 katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Wizara ya Maji katika miji 25 katika mpango wa kutatua tatizo la maji, Mkoa wa Geita tumeuangalia kwa ukaribu zaidi na tunafanya jitihada kubwa ya kutatua tatizo la maji.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 2

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Kwa kuwa Bwawa la Yongoma, katika Mto wa Yongoma lilikuwa-designed na Serikali ya Japan kupitia JICA tangu 2012; na kwa kuwa mwaka huu 2018/2019 liliwekwa kwenye bajeti kwamba lijengwe, Serikali inatoa tamko gani kuhusu ujenzi wa bwawa hili?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Kaboyoka. Kubwa ambalo nataka niseme ni utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha. Nia ya Serikali bado ipo pale pale, na sisi kama Wizara tunaendelea kuhakikisha fedha hizi zinapatikana ili bwawa lile liweze kujengwa na wananchi waweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Liwale ni Mji unaokua kwa haraka sana na una chanzo kimoja tu cha maji; na kutokana na mabadiliko ya tabianchi, chanzo kile hakitoshelezi tena. Je, ule mradi wa kutafuta chanzo mbadala cha maji kwa Mji wa Liwale, umefikia wapi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, lakini na pili nimepata nafasi ya kufika katika Jimbo lake la Liwale. Pamoja na jitihada kubwa za Serikali zinazofanyika lakini kiukweli, Liwale kuna changamoto. Sasa sisi kama Wizara tulishawaagiza watu wetu wa rasilimali za maji katika kuhakikisha wanafanya utafiti wa kina ili tuweze kupata chanzo cha uhakika, tuweze kubuni mradi mkubwa ambao kwa ajili ya kutatua kabisa tatizo la maji Liwale. Nataka nimhakikishie sisi tutalifanya jambo hili kwa haraka ili wananchi wake wa Liwale waweze kupata maji ya uhakika.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 4

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Miradi ya maji katika Vijiji vya Matala, Kansay, Buger, Endonyawet na Getamock Wilayani Karatu chini ya mpango wa WSDP imejengwa chini ya kiwango na hivyo haifanyi kazi, karibu shilingi bilioni nne zimetumika na haziwanufaishi wananchi. Tulimwomba Mheshimiwa Waziri mara nyingi aje Karatu ili aje atatue tatizo hilo…

MWENYEKITI: Uliza swali sasa.

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba awaambie wananchi wa vijiji hivyo ni lini atakwenda ili kutatua changamoto za miradi hiyo? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, binafsi nilishapata taarifa za Karatu na nimefika, lakini kubwa kuna miradi ambayo imefanyiwa ubadhirifu. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Viongozi wa Wizara tumesha-note na tumekubaliana tutakwenda katika maeneo yale yote na wale walioshiriki katika ubadhirifu ule, lazima fedha watazitapika na hatua kubwa kali tutazichukua.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 5

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Mradi wa bomba la Ziwa Victoria umeshafika katika Halmashauri ya Mji wa Kahama, lakini usambazaji katika Kata nyingi bado haujafanyika, Kata ya Mwenda kulima, Kagongwa, Iyenze, Isagee maji hayajafika. Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza maji ya Ziwa Victoria ili wananchi waweze kunufaika? Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza tutambue jitahada kubwa zilizofanywa na Serikali, tunatambua kabisa tulikuwa na changamoto kubwa sana, katika Mji wa Kahama na Shinyanga na Serikali ikaona haja sasa ya kuyatoa maji Ziwa Victoria kwa ajili ya kutatua matatizo haya ya maji, kikubwa maji yale yamekwishafika lakini imebaki changamoto tu ya usambazaji. Hivyo, nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge, wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani, sisi tumekwishawaita Wakurugenzi wote na tumekwishawaagiza katika mapato yao wanayoyakusanya watenge asilimia katika kuhakikisha wanasambaza maji kwa wananchi ili waweze kupata maji safi salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 6

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba anijibu swali langu la nyongeza. Mheshimiwa Waziri alifika katika Kata ya Ruaha Mbuyuni na akaona jinsi matatizo ya maji yanavyosumbua. Wananchi wamekuwa wakipata kipindupindu kila mwaka na yeye aliahidi mambo makubwa. Sasa je, ni lini wananchi wa Ruaha Mbuyuni ambao wanategemea kupata kituo cha afya watapata maji pale?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze Mbunge wa Kilolo, Mzee wangu, kwa kazi kubwa sana anayoifanya, lakini tulipata nafasi ya kufika Ruaha Mbuyuni. Changamoto kubwa tuliyoiona kwa Wahandisi wetu walitengeneza tenki la maji lakini hawakuwa na chanzo cha maji. Kwa hiyo tuliwaagiza watu wa rasilimali za maji wa bonde lile waende na wameshafanya tafiti kikubwa tunawaagiza watu wa DDCA waende kuchimba kisima haraka katika kuhakikisha mradi ule unafanya kazi kwa wakati.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 7

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa ongezeko la watu na hasa Jiji la Dodoma limekuwa kubwa baada ya Makao Makuu kuhamia Dodoma, je, Serikali ina mpango kabambe au mkakati gani wa kuhakikisha kwamba maji ya Ziwa Victoria yaliyofika Tabora yanafika Dodoma kuwasaidia wananchi wa Dodoma kutokana na upungufu wa maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Bura kwa swali lake zuri sana, sisi kama Wizara ya Maji tunatambua kabisa sasa hivi kumekuwa na ongezeko kubwa sana katika Mkoa huu wa Dodoma, lakini jitihada kubwa ambazo tulizozifanya sasa hivi, uzalishaji wetu zaidi ya lita milioni 55, lakini mahitaji lita kama milioni 44. Kwa hiyo, tuna maji kwa kiasi kikubwa, kubwa ambalo tunaloliona hapa ni suala zima la usambazaji, lakini itakapobidi tutafanya kila jitihada katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji na wananchi wa Dodoma wasipate tatizo hilo.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kutokana na shida kubwa ya maji hapa nchini, Bunge hili lilitengeneza, liliunda Wakala wa Maji, sasa ningependa kujua, je, tayari, Serikali imeshatengeneza kanuni za huo Wakala na kama zitagawiwa kwa Wabunge?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilipongeze sana Bunge lako Tukufu kutokana na jitihada kubwa walizofanya kupitisha Muswada wetu, pia kwa namna ya kipekee tumshukuru sana Mheshimiwa Rais. Baada ya Bunge kupitisha Muswada ule, Mheshimiwa Rais ameshasaini na imeshakuwa Sheria, sisi kama Wizara ya Maji, tutazileta kwa haraka kanuni zile ili tuanze utekelezaji kwa haraka sana. Ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Katoro- Buseresere unaokusudia kutoa maji Ziwa Victoria?

Supplementary Question 9

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda nimuulize Waziri, kwa kuwa kuna mradi mkubwa wa maji kutoka Nyamtukuza katika Wilaya ya Nyang’hwale, kupita Kakora, Kitongo, Ikangala, Kharumwa, Izunya hadi Bukwimba ambao umekuwa ukisuasua kwa muda mrefu, lakini Serikali ikiwa ikitoa pesa. Je, ni lini sasa mradi huu utakamilika na namwomba Mheshimiwa Waziri baada ya Bunge hili aende akauone mradi huo kwa nini unaendelea kusuasua?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge. Kubwa pamoja na mradi huo, lakini tumeshalipa zaidi ya bilioni moja na milioni mia saba certificate yake kwa Mkandarasi anayedai, ili mradi usikwame.

Kuhusu kusuasua kwa mradi, sisi kama Wizara ya Maji, Wahandisi ama Wakandarasi wababaishaji tutawaweka pembeni, nataka nimhakikishie kabla ya Bunge tutakwenda Nyang’hwale katika kuhakikisha tunaenda kuukagua mradi ule na ikibidi kama Mkandarasi hana uwezo wa kutekeleza mradi huo tutamwondoa mara moja. Ahsante sana.