Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Hakuna barabara ya kuunganisha Daraja la Nyubati na Kata ya Kisondelea hadi Nzunyuke umbali wa zaidi ya kilomita 30 kufika kijiji cha Nyubati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Kijiji cha Nyubati na Kata ya Kisondelea?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa matatizo ya wananchi wa Rungwe kuhusu barabara yanafanana kabisa na matatizo ya wananchi wa Chunya hasa hasa kwa barabara inayotoka Chunya – Kiwanja - Ifumbo - Mjele, ambayo sasa hivi inaunganisha Mikoa miwili ya Songwe na Mbeya; na kwa kuwa Mamlaka ya Wakala wa Barabara (TARURA) toka imeanzishwa Chunya hakuna barabara hata moja ambayo wameikarabati. Je, Mheshimiwa Waziri anatoa maagizo kwa TARURA ili waikarabati barabara hiyo iweze kupitika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri kijana mchakapa kazi yupo tayari kuongozana name kwenda Chunya ili akaangalie kazi ambazo wanafanya TARURA katika Halmshauri ya Chunya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kwa barabara ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja na mipango iliyopo na kwa sababu michakato hii inaanzia kwenye ngazi ya Halmashauri, inakuja kwenye Mkoa mpaka ngazi ya TAMISEMI, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane baadaye tupate taarifa sahihi ya eneo hili na tuweke mipango mahususi ambayo inaweza kutatua shida hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Mbunge anauliza kama nipo tayari. Mimi nipo tayari sana wakati wowote. Tupande ratiba twende tuone eneo hili, turudi kufanya mipango ya kukamilisha na kuondoa kero za wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Hakuna barabara ya kuunganisha Daraja la Nyubati na Kata ya Kisondelea hadi Nzunyuke umbali wa zaidi ya kilomita 30 kufika kijiji cha Nyubati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Kijiji cha Nyubati na Kata ya Kisondelea?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naipongeza Serikali kwa mradi wake wa kuleta mpango wa DNDP kwenye Mkoa wa Dar es Salaam. Jimbo la Ilala tumepata Kilometa mbili tofauti na maeneo mengine wamepata zaidi ya Kilometa 40.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuboresha barabara za kata zote 10 za Jimbo la Ilala ili ziweze kuonekana za kupitika kwa sababu ni katikati ya mji na zinasaidia kupunguza msongamano katikati ya mji kuelekea pembezoni mwa mji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M.WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna miradi inaendeshwa katika Mji wa Dar es Salaam, UNDP na sasa kilichobaki, baada ya kutengeneza barabara nzuri zaidi, ni vingumu zaidi barabara za pembezoni zikawa nzuri. Sasa kwa sababu Mheshimiwa Mbunge tupo wote Ilala na tunampongeza Meneja wa TARURA kwamba ni msikivu sana, tutawasiliana naye tuone mipango iliyopo na sisi tuishi kama Wabunge wa Dar es Salaam ili kuwezesha mipango ya kukamilisha barabara zetu na hasa wakati wa mafuriko watu wa Dar es Salaam wasiweze kupata shida zaidi.

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Hakuna barabara ya kuunganisha Daraja la Nyubati na Kata ya Kisondelea hadi Nzunyuke umbali wa zaidi ya kilomita 30 kufika kijiji cha Nyubati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Kijiji cha Nyubati na Kata ya Kisondelea?

Supplementary Question 3

MHE. ZAINABU AMIR MNDOLWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara itaokayo Korogwe kupitia Kwa Mndolwa - Mkaalie - Tamota hadi kuunganishwa na Kiwanda cha Chai Mponde ni takribani kilometa 40 lakini haijajengwa kwa kiwango cha lami. Hii ni barabara muhimu sana katika nchi kwa sababu mazao mengi kutoka Jimbo la Bumbuli ambayo yanasafirishwa kwenda Dar es Salaam hupita pale, lakini wakati wa mvua barabara hii haipitiki kabisa na kuna maporomoko ya mawe:-

Je, ni lini sasa Serikari itajenga hii kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza kuendelea kuwasema wananchi wa Korogwe, lakini namwomba sana kwa sababu tupo kwenye wakati wa bajeti hii aunge mkono bajeti ya TAMISEMI Jumatatu tutakapofika kwa majaliwa ya Mwenyenzi Mungu tupate fedha hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nilijibu swali hapa nikasema, tuliunda timu ya wataalam, inapitia sasa namna ya ku-identify hizi barabara ili tuangalie ule Mfuko wa TANROADS na TARURA. Nimesikia michango ya Waheshimiwa Wabunge kwamba TARURA inafanya kazi nzuri sana. Shida hapa ni fedha. Tukipata chanzo realible cha fedha na formula ambayo ipo sawaswa na wadau mbalimbali na bajeti ikaungwa mkono. Nia ya Serikali ni kukamilisha barabara zote ikiwezekana kwa kiwango cha lami ikiwepo hiyo ya Korogwe. Ahsante.