Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando?

Supplementary Question 1

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali, nimpongeze Rais wangu Mungu azidi kumjaza hekima na maisha marefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, pamoja kwamba tumepata fedha zote hizo kama nilivyosema nashukuru lakini bado sekondari nyingi katika Jimbo la Lushoto hazina hosteli na hii imepelekea watoto wengi kufeli na watoto wengi wa kike kupata ujauzito. Je, Serikali ina mkakati gani sasa tena wa haraka kuhakikisha kwamba wanajenga hosteli katika sekondari ambazo hazina hosteli?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa Jimbo la Lushoto kwa nguvu zao wamejenga majengo ya maabara tena yote matatu lakini mpaka sasa majengo yale hayajamalizika. Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu sasa wa kumalizia maboma yale ili watoto wetu waweze kusoma elimu kwa vitendo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Shekilindi maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nampongeza Mheshimiwa Mbunge nimefika kwenye Jimbo lake la Lushoto, wananchi wa eneo lile na yeye mwenyewe wamefanya kazi kubwa kuongeza miundombinu ya elimu lakini pia afya na maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anaomba kujua mpango wa Serikali kuongeza hosteli. Katika bajeti ambayo inaendelea kujadiliwa sasa kila mtu akipitia kwenye kitabu cha bajeti cha Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, utaona kuna maeneo mbalimbali fedha zimetengwa kwa kazi hiyo lakini iko miradi mingine ya elimu itakayoimarisha hosteli mbalimbali. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge avumilie mwaka huu wa fedha tumetenga fedha na kadri zitakavyopatikana tutaweza kumaliza hiyo shida kwa watoto wa kike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kuhusu maboma ya maabara, tumeanza kupeleka vifaa na kukamilisha maboma katika shule nyingi kadri itakavyowezekana. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane huenda shule au maeneo yake anayotaja tutapeleka vifaa vya maabara lakini pia tutamalizia maboma ya maabara hizo. Lengo ni ili tupate wataalamu wa sayansi ili tutakapoanza issue ya viwanda tuwe na wataalam wa kutosha.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa misingi ya elimu bora, sawa, shirikishi kwa wote, elimu ya msingi inaanzia darasa la ngapi mpaka la ngapi na elimu ya sekondari inaanzia darasa la ngapi mpaka la ngapi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa James Mbatia, Mbunge wa Jimbo la Vunjo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utaratibu tunaotumia tuna darasa la awali, darasa la kwanza mpaka la saba, form one mpaka form four na kidato cha tano na cha sita baadaye elimu ya juu. Ahsante.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba hivi karibuni Serikali imefanya ukarabati mkubwa wa shule za sekondari kongwe ikiwemo Shule ya sekondari ya Mpwapwa lakini mimi nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri mnafanya ukarabati wa shule tu lakini nyumba za walimu zimechakaa kweli kweli. Je, mna mpango gani wa kukarabati shule na nyumba ya walimu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa George Malima Lubeleje (Senator), kama lifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, si kweli kwamba tunakarabati shule tu ukweli ni kwamba tumekarabati shule nyingi zaidi kuliko nyumba za walimu. Hata kwenye kitabu cha bajeti tunachojadili sasa ambapo Mungu akipenda tutahitimisha Jumatatu tarehe 15 akipitia kwenye majimbo mbalimbali ataona fedha zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa nyumba za walimu. Uwezo wa Serikali siyo mkubwa sana, tunaomba Mheshimiwa Mbunge na wadau mbalimbali tushirikiane katika jambo hili kupunguza shida ya walimu katika nchi hii. Ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa tumeona shule nyingi kongwe zilizotoa viongozi mbalimbali zimekuwa zikikarabatiwa. Kwa Mkoa wangu wa Arusha, kuna Shule ya Arusha Sekondari ambapo miundombinu yake ni mibovu na chakavu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutenga pesa kwa ajili ya kukarabati shule hii kongwe ya Arusha Sekondari?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, msemaji mzuri sana wa Mkoa wa Arusha na Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nia ya Serikali kukarabati shule zote kwa wakati mmoja kama ingewezekana lakini kwa sababu ya ufinyu wa bajeti jambo hilo halijawezekana, tutakarabati kulingana na uwezo lakini pia kuna vigezo mbalimbali. Kwa hiyo, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge, tufanye tathmini, tumeshamaliza awamu ya kwanza tupo kwenye mpango wa awamu ya pili, huenda kwenye awamu ya tatu Shule ya Arusha Sekondari ikaingizwa kwenye mpango huu wa Serikali wa kukarabati shule hizi.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za msingi na sekondari nchini:- Je, ni lini Serikali itazifanyia ukarabati Shule za Msingi Kwemashai, Bandi, Milungui, Kilole na Shule za Sekondari za Ntambwe, Ngulwi - Mazashai na Mdando?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri sambamba na matatizo ya Lushoto, Wilaya ya Busega haikupata mgao wa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma. Je Mheshimiwa Naibu Waziri, unaweza ukatoa maelekezo katika mgao huu na Wilaya ya Busega tupate mgao huo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge wa Busega swali lake la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natambua kazi nzuri ambayo anaifanya katika Jimbo lake la Busega kuwasemea wananchi wake lakini sina hakika kwa sababu fedha zile zilisambazwa kwenye wilaya zote kwa maana ya Halmashauri inawezekana kwenye Jimbo hilo kuna bahati mbaya. Naomba tuwasiliane baada ya kipindi cha maswali na majibu tuone njia bora ya kumaliza shida hiyo. Ni nia ya Serikali kila Jimbo lipate mgao wa kupunguza shida ya maboma na kuchangia nguvu za wananchi ili wasilalamike.