Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Wanawake Mkoani Kigoma wameitikia wito wa kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali kama vile vikundi vya kilimo cha muhogo, kurina na kuchakata asali na VICOBA:- Je, Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Kigoma zimechangia kiasi gani kwa vikundi hivyo kama sheria inavyotamka?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu maswali mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, kabla ya kuuliza swali langu, naomba nichukue nafasi hii kupongeza Halmashauri ya Kusulu TC kwa kuweza kufanya vizuri kwa kutoa pesa hizo kila baada ya miezi mitatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, kwa kuwa wanawake wengi, vijana pamoja na walemavu wameweza kuhamasika kufungua vikundi lakini zipo Halmashauri ambazo zinasuasua na nyingine kutokupeleka pesa hizo kama sheria inavyotaka. Je, Wizara iko tayari sasa kutoa agizo ili Halmashauri hizo ziweze kutoa pesa kwa wakati?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, zipo Halmashauri ambazo bado ni changa mfano Halmashauri ya Kakonko pamoja na Buhigwe, makusanyo yao sio mazuri sana, ni kidogo. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa kuzisaidia Halmashauri hizo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephine, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kwa kujali wanawake na kuwasemea ili waweze kupata mikopo na kujikwamua kiuchumi. Hii kazi inafanywa na Wabunge wote wa Viti Maalum kama nilivyosema jana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wakati wa bajeti bahati nzuri nimehudhuria kikao cha Kamati ya Utawala wa TAMISEMI, naomba niwapongeze wajumbe wakiongozwa na Mwenyekiti, Mheshimiwa Rweikiza kwa kazi nzuri waliyofanya katika mjadala ule. Kila Mkoa, Halmashauri, Mkurugenzi, Katibu Tawala alihojiwa na kutoa maelezo namna ambavyo amesimamia ukusanyaji wa fedha na kupeleka kwenye vikundi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii hoja ya kusuasua kutokupeleka fedha ni jambo la kisheria na maagizo yametoka naomba nirudie, Wakurugenzi, Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala kwa maelekezo ya Kamati ya Utawala na TAMISEMI kwa mwaka wa fedha ujao kama kuna mtu atakuwa hajapeleka fedha hizi kikamilifu na kusimamia marejesho hali yake itakuwa mbaya sana. Haya ni maagizo ya Kamati na sisi kama Wizara tumeyachukua.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, maelekezo ni kwamba hakuna Halmashauri changa katika jambo hili, kama umekusanya Sh.100 umetoa makato yale ambayo ni ya msingi na makato mbalimbali ambapo yametolewa kwenye Halmashauri inayobaki 10% yake peleka kwenye vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Kwa hiyo, hata kama utakuwa umekusanya Sh.5, ondoa makato yote ya msingi ambayo yameelekezwa na Serikali inayobaki 10% peleka, usipopeleka sheria itachukua mkondo wake.