Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:- Je, ni fedha kiasi gani zilitumika kujenga mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yajulikanayo kama H.E Magufuli Hostel?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu. Mabweni haya yana ghorofa nne nne na ni majengo 20. Bei hii ilileta maneno mengi sana na tukaomba CAG afanyie special audit. Nataka kujua ni jengo gani la ghorofa nne yenye kuchukua wanafunzi takriban 3,840 kwa majengo yote inaweza ghorofa moja kugharimu shilingi milioni 500 tu?

Mheshimiwa Spika, la pili, nataka kujua baada ya TBA kuyajenga majengo yale ndani ya miezi minne yalikuwa na nyufa nyingi, maarufu kama expansion joint ambazo sisi tunavyojua ni lazima jengo liwe nalo, lakini expansion joint
hizo zilienda mpaka kwenye floor na mpaka kwenye madirisha. Nataka kujua ni kwa sababu gani mabweni hayo yalimomonyoka na ni je ni gharama kiasi gani imetumika sasa kuweza kurekebisha hasa ikizingatiwa kwamba TBA hivi majuzi tu Mheshimiwa Rais aliwafukuza kwenye kazi mbalimbali. Je hili jengo ambalo sasa hivi limetengewa bilioni moja ni hao hao TBA pale kwenye hayo Magufuli Hostel watajenga au wamepata mkandarasi mwingine?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:

Mheshimiwa Spika, kuhusu hitilafu alizosema zimetokea na hususan zile zinazohusishwa na expansion joint naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba expansion joint sio hitilafu, expansion joint imekusudiwa kuwekwa kwenye maghorofa yale ili kuweza kuhimili changamoto ambazo zinaweza zikatokea, ni kazi ya kitaalamu na wala sio upungufu na tayari tulishatoa maelezo marefu sana kuhusu hili.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na upungufu mwingine mdogo mdogo uliotokea, hii ni kawaida ambayo inatokea katika ujenzi na tayari ilisharekebishwa na kwa sababu tayari mkandarasi aliyepewa kazi bado alikuwa katika kipindi cha liability alirekebisha yeye mwenyewe na tayari ilishakwisha na hakukuwa na fedha za ziada ambazo zilitumika kurekebisha changamoto hiyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu gharama naomba nimhakikishie Mheshimiwa Susan Lyimo kwamba jengo hilo limegharimu shilingi bilioni 10. Sasa kama yeye anatilia shaka kuhusu ukweli huo ambao namweleza labda yeye atuletee mahesabu yake ya kuonesha kwamba imegharimu zaidi, lakini hizi ni fedha za umma, zimelipwa kwa mujibu wa taratibu, taarifa rasmi ambayo naileta Bungeni ni kwamba imetumia shilingi bilioni 10 na hakuna fedha nyingine yoyote iliyotumika ukiacha fedha ambazo zimetumika kwa ajili ya kufanya masuala mengine ambayo ni nje ya scope ya kazi ile ambayo walipewa TBA.