Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Serikali ilikuwa na mpango wa kupeleka maji katika Mji wa Kisesa - Bujora na Kata ya Bukandwe:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga na kupeleka maji katika miji hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nini sasa commitment ya Serikali? Financing agreement ni lini itasainiwa ili miji hii midogo iweze kupata maji?

Swali la pili, kwa kuwa kuna mradi ambao ulikuwa umeanza upembuzi yakinifu na umeshakamilika katika Ziwa Victoria ambao utanufaisha Wilaya ya Kwimba Jimbo la Sungwe na Wilaya ya Maswa Jimbo la Malampaka na Vijiji vya Magu takribani 40, ni lini mradi huo utaanza kutekelezwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Magu kwa kazi nzuri sana na kuweza kuwapigania wananchi wake mpaka ule mradi wa Euro milioni 104 kuweza kuanza katika Jimbo lake. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba safari moja huanzisha nyingine. Tunatekeleza mradi huu, lakini kwa kuwa ile ni kazi ya nyongeza, sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo, tutafanya mawasiliano haraka, pamoja na wenzetu wa Wizara ya Fedha ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika Wizara yetu; tutashirikiana kwa haraka ili mradi huu uweze kusainiwa na uweze kupeleka maji katika eneo lake.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala zima la eneo lake kwa vijiji alivyovitaja pamoja na suala la upatikanaji wa maji, maeneo mengi ya Magu pamoja na Sumve yamekuwa karibu sana na Ziwa Victoria. Siyo busara sana kuona tuna rasilimali hizi za kutosha halafu maji yale yasinufaishe wananchi. Sisi kama Wizara ya Maji, tuna Mhandisi Mshauri sasa hivi anayefanya kazi ya upembuzi katika kuhakikisha rasilimali ile ya Ziwa Victoria, maeneo ya miji yaliyoko karibu waweze kupata maji safi na salama yenye kutosheleza.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Sumve pamoja na Mheshimiwa wa Magu, sisi kama Wizara ya Maji, tumejipanga katika kuhakikisha mradi ule utakapokuwa umeshasanifiwa, utaanza kwa haraka ili wananchi waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Serikali ilikuwa na mpango wa kupeleka maji katika Mji wa Kisesa - Bujora na Kata ya Bukandwe:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga na kupeleka maji katika miji hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nami napenda kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mradi unaotegemewa kutekelezwa pale Magu unategemea sana chanzo kipya kitakachojengwa kwenye Jimbo la Nyamagana pale Butimba ambao utasaidia pia maji kule Buswelu kwenye Jimbo la Ilemela, ikiwemo Kata ya Buhongwa kama ilivyotajwa, Kishili, Rwanima pamoja na Igoma.

Mheshimiwa Spika, mradi huu tayari mkandarasi wa kusambaza bomba za maji ameshapatikana na mkandarasi wa kujenga chanzo hiki kipya ndio imekuwa inasuasua. Mheshimiwa Kiswaga ameomba commitment ya Serikali, sasa Mheshimiwa Waziri atuhakikishie kwamba hii financial agreement ni lini itakuwa tayari ili miradi hii iweze kutekelezeka kulingana na hali halisi ilivyo?

Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa maji na uwepo wa Ziwa Victoria haufurahishi leo watu wa Mwanza, Nyamagana pamoja na miji inayozunguka kuendelea kuchota maji kwenye visima.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nampongeza kaka yangu Mheshimiwa Mabula kwa kazi nzuri anayoifanya katika Jimbo lake la Nyamagana, lakini atambue kabisa eneo ambalo litapata maji kwa asilimia 100 ni eneo la Nyamagana. Sasa sisi kama Wizara kuna kazi kubwa sana inayofanyika, hiki kilichobaki ni kiasi kidogo sana.

Mheshimiwa Spika, kubwa, nataka nitengeneze commitment kwake kwamba sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji na siyo Wizara ya Ukame tutafanya mawasiliano ya haraka na Wizara ya Fedha kuona ule mkataba unasainiwa kwa haraka ili mwisho wa siku mkandarasi yule aweze kuhakikisha chanzo kile cha maji kinatekelezwa kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Serikali ilikuwa na mpango wa kupeleka maji katika Mji wa Kisesa - Bujora na Kata ya Bukandwe:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga na kupeleka maji katika miji hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa miradi mingi ya maji imesimama katika Wilaya ya Mpwapwa na Kongwa na hivi sasa wananchi wanakosa huduma ya maji; makandarasi hawajalipwa fedha:-

Je, Mheshimiwa Waziri anasemaje kuhusu hili? Ni lini makandarasi watalipwa miradi ikamilike na wananchi waweze kupata maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ukimwona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha. Kiukweli tulikuwa na madai ya makandarasi takribani zaidi ya shilingi bilioni 104.5. Tunashukuru sana Wizara ya Fedha, baada ya kufanya ukaguzi imeonekana makandarasi ambao wanatakiwa kulipwa, wanadai zaidi ya shilingi bilioni 88. Wameshatupa fedha zaidi ya shilingi bilioni 44 mwezi huu Machi na wametupa commitment ndani ya mwezi huu wa Nne watatupa tena shilingi bilioni 44 katika kuhakikisha makandarasi wote fedha zao zinalipwa.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama kuna certificate yake hajalipwa, tuwasiliane tumlipe. Nataka nimhakikishie, baada ya kumlipa, ataendelea kuwa juu juu kileleni katika Jimbo lake la Mpwapwa. Ahsante sana.