Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza-:- Je, Serikali itakamilisha lini ujenzi wa barabara ya kutoka Kibaoni kupitia Majimoto mpaka Inyonga kwa kiwango cha lami ukizingatia kuwa daraja la Kavuu limekwishakamilika ili barabara hiyo ianze kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake yenye matumaini kwa sababu barabara ya kutoka majimoto Inyonga zabuni imeshatangazwa. Swali langu ni kwamba kwa kuwa barabara hii iko chini ya TANROADS na TANROADS wamesema kwamba wanatangaza zabuni ya kumpata mpembuzi na msanifu ili waweze kuianza barabara hiyo na kwa kuwa zoezi la kutangaza zabuni na mpaka kumpata mkandarasi ni la muda mrefu. Je, ni lini sasa katika maombi yangu maalum ya kilomita 2.0 katika Mji wa Usevya yatapatiwa majibu na barabara hiyo ianze kutengenezwa kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa mkandarasi alipatikana ambaye ameweza kujenga kilomita
1.7 katika Mji wa Inyonga, lakini katika mwaka wa fedha 2018/2019 mkandarasi wa kujenga kilomita 2.5 amepatikana na yupo katika eneo la mradi. Je, ni eneo gani la mradi ambapo mkandarasi huyo yupo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, kwanza nazipokea shukurani alizozitoa, nazipokea kwa dhati, lakini pia kwa furaha nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi ya usanifu kama nilivyojibu katika jibu la msingi tarehe 11 ambayo ni Jumatatu ijayo zabuni itafunguliwa na hii hakuna namna kwa sababu, harakati za ujenzi zinazingatia pia Kanuni na Sheria za Manunuzi. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge tupo kwenye hatua nzuri, mzabuni atakapokuwa amepatikana na sisi tutasimamia kwa umahiri ili hii kazi hii iweze kukamilika kwa wakati. Kwa hiyo, nimtoe hofu pamoja na wananchi wa Kavuu kwa ujumla kwamba sasa ujenzi wa barabara hii utakuwa umeanza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu eneo la kilomita 2.0; eneo hili ni mwendelezo katika Mji wa Inyonga, lakini Mheshimiwa Mbunge nafahamu kwamba iko haja ya kuweka msukumo wa kujenga kipande cha barabara kutoka Kibaoni kuja kwenye Mji wa Usevya ambao ni Makao Makuu ya Halmashauri. Kwa hiyo nimtoe hofu tu kwamba, usanifu utakapokamilika na sisi tutaweka kipaumbele ili wananchi hawa wanaokwenda makao makuu waweze kuunganika vizuri na barabara ambayo sasa ukitoka Kizi kuja Kibaoni, hatimaye tuunganishe kipande hiki cha kuja Makao Makuu ya Wilaya, lakini pia sehemu ya Majimoto ambayo ina wafanyabiashara wengi na kuna sehemu kubwa ya uchumi. Kwa hiyo, asiwe na wasiwasi, tutazingatia haya maeneo ambayo ni muhimu kuhakikisha wananchi wanaunganishwa vizuri.