Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Kituo cha Forodha katika Bandari ya Manda, Ludewa ili kurahisisha huduma kwa wananchi wanaoenda nchi jirani hasa kwa shughuli za biashara?

Supplementary Question 1

MHE. DEORATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Eneo la Manda ni bandari nzuri ambayo ingeweza kutumika ku-tap soko la nchi ya Malawi. Eneo la Malawi au nchi ya Malawi ina tatizo kubwa sana la bidhaa au vyakula kama mahindi na kadhalika ambako Ludewa mahindi yanalimwa kwa wingi kiasi ambacho mengine yanaoza kwenye maghala. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kujenga hicho Kituo cha Forodha? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili. Utaratibu wa kupata forodha ni kama ulivyoelezwa na Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha. Je, baada ya kuandika proposal hiyo inachukua muda gani mpaka kukamilika kwake? Ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Ngalawa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza alivyoanza kuipongeza Serikali kwa kufungua miundombinu kuwafikia wananchi ambao walikuwa hawajafikiwa nami naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya katika Taifa hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, naomba niwapongeze sana wananchi wa Manda kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya ya shughuli za kiuchumi zinazowaondoa katika mzunguko wa umaskini kama ambavyo wenzetu wanaendelea kutangaza sifa za Taifa hili ambazo si sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambe Watanzania kwamba Taifa hili, alisema Mheshimiwa Waziri wa Fedha siku mbili zilizopita, kwamba kiwango cha umaskini kimepungua kwa kiwango kikubwa na sasa tunasubiri utafiti huu watakapotoa matokeo yao rasmi (household based survey) Watanzania wataona na wapuuze haya yote yanayoendelea kuenezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili nalisema kwa sababu sisi kama Serikali tunaitambua Manda kama eneo la kimkakati na ndiyo maana Bunge lililopita nilipojibu swali la 73 la Mheshimiwa Mbene kuhusu ujenzi wa Kituo cha Forodha Ileje na swali la nyongeza la Mheshimiwa Ngalawa nilimwambia tayari Serikali na namhakikishia tumeshaanza kufanya utafiti, tunachosubiri ni maombi hayo rasmi kutoka kwenye mkoa ili nasi tuifanyie kazi haraka iwezekanavyo.

Mheshimwa Naibu Spika, swali lake la pili, kwamba kwa muda gani unachukuliwa; kwa sababu tumeshaanza utafiti kama Serikali, namhakikishia, tutakapopata maombi hayo, tutayawasilisha rasmi Wizara ya Afrika Mashariki ili waweze kuwasilisha katika Sekretarieti ya Afrika Mashariki na haitachukua muda kwa sababu Manda ni eneo la kimkakati kwa Taifa hili.