Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Amina Saleh Athuman Mollel
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Kuna miradi mikubwa ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo hadi sasa haijakamilika. Miradi hiyo ipo Kijiji cha Mperamumbi Kata ya Kwala, Kijiji cha Boki Mnemera Kata ya Bokomnemera, Kijiji cha Vukunti Kata ya Mlandizi na Kijiji cha Dutumi Kata ya Dutumi:- Je, ni lini miradi hiyo itakamilika ili kuwaletea matumaini wananchi wa maeneo hayo, hususan akinamama?
Supplementary Question 1
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Kijiji cha Kipangege, Kata ya Soga mradi wa maji tayari umeshakamilika lakini hadi hivi sasa wananchi hawajaanza kutumia maji hayo. Je, lini sasa mradi huu utakamilika na kuanza kutoa maji ili wananchi wa Kata ya Soga waanze kufurahia huduma ya maji safi na salama?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tatizo hili pia linafanana na tatizo la Wilaya ya Arumeru katika Jimbo la Arumeru Magharibi, Kata ya Bwawani ambapo mradi wa maji tangu enzi za aliyekuwa Mbunge Elisa Mollel na Ole- Medeye ulianza kujengwa mpaka leo hii bado haujakamilika na Serikali imekwishatoa fedha mkandarasi hayupo. Napenda tu kufahamu majibu kutoka kwa Serikali, nisikie kauli yao juu ya mradi huu ili wananchi wa Kata ya Bwawani nao waweze kupata maji na kuondokana na changamoto kubwa iliyopo hivi sasa. Ahsante.
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma kwa kazi nzuri anayoifanya katika Mkoa wa Pwani. Kikubwa sisi kama Wizara ya maji jukumu letu ni kuhakikisha Wanapwani, kwa maana ya Soga, waweze kupata maji safi na yenye kuwatosheleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, amesema katika Kijiji kile cha Kipagenge katika Kata ya Soga kuna mradi lakini wananchi hawapati maji. Nataka nimhakikishie baada ya Bunge nitafanya ziara katika eneo hilo la Soga, niangalie ili mwisho wa siku mradi ule uweze kukamilika na wananchi waweze kupata maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia dada yangu Amina Mollel amezungumza kwamba sasa mradi umekuwa wa muda mrefu sana, kwamba Serikali imekwishatoa fedha lakini mkandarasi hayupo site. Nimhakikishie katika maeneo nitakayotembelea basi na Arumeru Mashariki nitafika na kuhakikisha tunaongeza nguvu katika mradi ule ili wananchi waweze kupata maji safi na salama na yenye kutosheleza.
Name
Kiswaga Boniventura Destery
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Magu
Primary Question
MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Kuna miradi mikubwa ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo hadi sasa haijakamilika. Miradi hiyo ipo Kijiji cha Mperamumbi Kata ya Kwala, Kijiji cha Boki Mnemera Kata ya Bokomnemera, Kijiji cha Vukunti Kata ya Mlandizi na Kijiji cha Dutumi Kata ya Dutumi:- Je, ni lini miradi hiyo itakamilika ili kuwaletea matumaini wananchi wa maeneo hayo, hususan akinamama?
Supplementary Question 2
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Tatizo la Pwani linafanana kabisa na tatizo lilipo Wilaya ya Magu katika miradi inayoendelea Sola, Kisamba, Bubinza, Matelamuda, pamoja na Kabila Ndagalu na Kitongo Sima, miradi hii imesimama sasa kwa sababu wakandarasi wamesha-raise certificate na Wizara tayari inazo taarifa hizo. Je, ni lini Wizara italipa fedha kwa wakandarasi ili miradi hiyo iweze kuendelea?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Kiswaga kwa kazi nzuri sana anayoifanya katika Jimbo lake la Magu. Tunatambua kwamba utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha. Sasa sisi kama viongozi wa Wizara hatutakuwa kikwazo katika kuwapatia wakandarasi wake fedha. Nimwombe baada ya Bunge tukutane ili tupate zile certificate tuangalie namna bora ya kuwapatia fedha ili wakandarasi waendelee na kazi.
Name
Joseph Roman Selasini
Sex
Male
Party
CHADEMA
Constituent
Rombo
Primary Question
MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Kuna miradi mikubwa ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo hadi sasa haijakamilika. Miradi hiyo ipo Kijiji cha Mperamumbi Kata ya Kwala, Kijiji cha Boki Mnemera Kata ya Bokomnemera, Kijiji cha Vukunti Kata ya Mlandizi na Kijiji cha Dutumi Kata ya Dutumi:- Je, ni lini miradi hiyo itakamilika ili kuwaletea matumaini wananchi wa maeneo hayo, hususan akinamama?
Supplementary Question 3
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Waziri siku za karibuni alitembelea Rombo na walimtembeza kwenye miradi ya Leto, Ngareni na Shimbi Mashariki. Hii ni miradi ambayo ilikuwa katika ile miradi ya World Bank ya visima 10 na ni ya siku nyingi na imeshakamilika; na kila Waziri anapokuja Rombo hapelekwi kwenye miradi mingine ni hiyo mitatu tu. Je, Mheshimiwa Waziri sasa yuko tayari kuiagiza halmashauri, maji ambayo yameshapatikana wagawiwe wananchi badala ya kufanya siasa?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipende kumjibu mzee wangu hapa; kwamba sisi kama viongozi wa Wizara tunapotoa huduma ya maji tunalinda uhai wa Watanzania na tunapeleka huduma hii kwa wana-CCM na hata Wana- UKAWA. Nataka nimuhakikishie kwa kutibitisha hilo, kwamba hata katika certificate tulizozilipa mwaka huu katika mwezi huu zaidi ya milioni 20 tumepeleka katika jimbo lake. Sasa nataka niwaambie wataalam wetu wa Wizara ya Maji, wahakikishe wanapeleka huduma hii muhimu kwa Wanarombo. Ahsante sana.
Name
Nape Moses Nnauye
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtama
Primary Question
MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Kuna miradi mikubwa ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo hadi sasa haijakamilika. Miradi hiyo ipo Kijiji cha Mperamumbi Kata ya Kwala, Kijiji cha Boki Mnemera Kata ya Bokomnemera, Kijiji cha Vukunti Kata ya Mlandizi na Kijiji cha Dutumi Kata ya Dutumi:- Je, ni lini miradi hiyo itakamilika ili kuwaletea matumaini wananchi wa maeneo hayo, hususan akinamama?
Supplementary Question 4
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Halmashauri ya Lindi Vijijini na hasa Jimbo la Mtama tulipanga mwaka huu wa fedha kuchimba visima virefu 25 na fedha zipo, tumeomba kibali toka kibali toka mwezi wa Nane mwaka jana, tukaandika barua kukumbusha mwezi wa Kumi na Mbili lakini mpaka sasa hatujibiwi chochote, tatizo la vibali hivi ni nini?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mbunge, Mheshimiwa Nape, nimefanya ziara katika Jimbo la Mtama, ni mmoja kati ya Waheshimiwa Wabunge wanaofanya kazi nzuri sana katika majimbo yao. Sisi kama Wizara ya Maji hatuko tayari kukwamisha jitihada anazozifanya. Nimwombe tu baada ya Bunge tuweze kukutana na Katibu Mkuu ili tuweze kupata vibali hivyo ili wananchi wake waweze kupata huduma ya msingi.
Name
Amina Nassoro Makilagi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:- Kuna miradi mikubwa ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo hadi sasa haijakamilika. Miradi hiyo ipo Kijiji cha Mperamumbi Kata ya Kwala, Kijiji cha Boki Mnemera Kata ya Bokomnemera, Kijiji cha Vukunti Kata ya Mlandizi na Kijiji cha Dutumi Kata ya Dutumi:- Je, ni lini miradi hiyo itakamilika ili kuwaletea matumaini wananchi wa maeneo hayo, hususan akinamama?
Supplementary Question 5
MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyonge. Pamoja na kuishukuru Serikali kwa kazi nzuri sana iliyofanya ya kujenga miundombinu katika Mji wa Musoma kiasi kwamba maji sasa hivi yanapasua mpaka mabomba na maji yanayozalishwa kwa saa ni takribani lita elfu 12, lakini maji yale yanaweza kupelekwa mpaka Wilaya ya Butiama, Kata za Bukaga, Mkanga, Makatende mpaka Bisuma. Vile vile maji haya yanaweza kufika mpaka Jimbo la Musoma Vijijini katika Kata za Etalo, Nyakatende, Nyigima pamoja na Nyamimange. Ningependa kujua, je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo ambako chanzo cha maji yaliyoleta maji ya Musoma wanaweza kupata na wenyewe huduma ya maji safi na salama kutokana na chanzo hicho cha maji? Ahsante sana.
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Makilagi kwa kazi nzuri ya kuwatetea Wanamara, lakini kikubwa Serikali imefanya kazi kubwa sana ya kuwekeza mradi zaidi ya bilioni 45 pale Musoma. Kwa hiyo changamoto kubwa ni suala zima la usambazaji, sisi hilo tumeliona na tutahakikisha tunawekeza fedha ili tusambaze maji ili maeneo hayo aliyoyataja yaweze kupata maji safi salama na yenye kutosheleza.