Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Mji wa Itigi unakua kwa kasi na umeme umeenda vijiji vya Lulanga, Itagata, Ukimbu, Chabutwa, Mtakuja, Makale na Mitundu ambapo ni kilomita 71; kwenda Itigi hadi Mwamagembe ni zaidi ya kilomita 130:- (a) Je, Serikali haioni ni vema sasa kuipa TANESCO hadhi ya Kiwilaya katika Wilaya ya Itigi? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi wa Shirika la Umeme katika Jimbo la Manyoni Magharibi?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati, ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, dhamira ya wananchi lakini dhamira ya Serikali ya kupeleka umeme vijijini kwa maana ya REA utekelezaji wake umekuwa mdogo na unasuasua sana. Katika Jimbo langu kuna vijiji vya Kashangu, Jeje, Idodyandole, Ipangamasasi, Mbugani, Agondi, Mabondeni, Kitopeni, Ipande, Muhanga, Damwelu, Kitalaka, Kaskazi Station, Kintanula na Rungwa havina umeme. Je, nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa vijiji hivi wategemee lini kupelekewa umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa umeme wa Mkoa wa Singida unakwenda hadi katika Wilaya ya Manyoni pamoja na Itigi lakini hatuna substation ipo station moja tu kubwa kule Singida. Je, Serikali iko tayari sasa kuweka substation Itigi kwa ajili ya kuboresha miundombinu hii ya umeme? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Massare, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi. Kwanza, nimpe pole kwa ajili ambayo aliipata na namwombea kwa Mwenyezi Mungu ampe afya njema. Pamoja na changamoto hiyo ya afya Mheshimiwa Massare ameendelea kulitumikia Jimbo lake hususani katika sekta ya nishati.

Mheshimiwa Naibu Spika, maswali yake mawili ya nyongeza, la kwanza lilijielekeza katika utekelezaji wa mradi huu wa REA III. Katika Wilaya ya Manyoni REA III, mzunguko wa kwanza kuna vijiji 30 na Jimbo lake lina vijiji 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge mkandarasi yupo anaendele na kazi katika maeneo ya Manyoni Mashariki katika Vijiji vya Majengo, Selia, lakini kwa kuwa, yeye Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake la Manyoni Magharibi ameuliza utekelezaji, nataka nimtaarifu hata asubuhi hii nimeongea na mkandarasi, ameshaanza kupeleka vifaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka pia, nilitaarifu Bunge lako Tukufu kutokana na utatuzi wa changamoto ambazo zilikuwa zinaukabili mradi. Mradi vizuri, sasa hivi unaendelea vizuri kwa sababu, mpaka sasa tunavyozungumza mpaka Januari vijiji takribani 5766 vimeshapata umeme kutokana na utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameulizia juu ya ujenzi wa substation katika eneo la Itigi Manyoni:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba, Singida tuna substation. Kutokana na mipango ya Serikali na ujenzi ulioanza wa line ya Kv 400 kutoka Singida mpaka Namanga, Serikali ina mpango wa ku-upgrade Kituo cha Singida. Kwa hiyo, nataka nimtaarifu kwamba, kutokana na matengenezo yatakayoendelea tutakipandisha hadhi Kituo cha Singida, ili kuhimili umeme mkubwa utakaosafirishwa mpaka Namanga, hivyo ni wazi kwamba, Mkoa mzima wa Singida kuhusu changamoto ya labda pengine usafirishaji wa umeme haitakuwpo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namwomba tu Mheshimiwa Mbunge aendelee tu kuiunga mkono Serikali, mipango ya kupandisha hadhi substation ya Singida inaendelea. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Mji wa Itigi unakua kwa kasi na umeme umeenda vijiji vya Lulanga, Itagata, Ukimbu, Chabutwa, Mtakuja, Makale na Mitundu ambapo ni kilomita 71; kwenda Itigi hadi Mwamagembe ni zaidi ya kilomita 130:- (a) Je, Serikali haioni ni vema sasa kuipa TANESCO hadhi ya Kiwilaya katika Wilaya ya Itigi? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi wa Shirika la Umeme katika Jimbo la Manyoni Magharibi?

Supplementary Question 2

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kujua mara nyingi nimekuwa naongea Vijiji vya Manispaa ya Mtwara Mjini nimekuwa nikivitaja vijiji hivi katika Bunge hili miaka yote mitatu na Serikali ikiwa inaahidi kwamba, inatekeleza suala la kupeleka umeme. Vijiji hivi ni Mkangara ambako Naibu Waziri alishaenda kule na akaona hali halisi, Naulongo, Mkunjanguo, Namayanga na maeneo…

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Maftah, uliza swali.

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujua kwa nini Serikali haitaki kutenga bajeti ili kupeleka umeme katika vijiji hivi au mitaa hii?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maftaha kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo yeye mwenyewe amekiri kwenye swali lake la nyongeza kwamba, mimi hata pamoja na Waziri wa Nishati tumeshafanya ziara zaidi ya mara mbili katika Mkoa wa Mtwara. Maeneo ambayo ameyataja ikiwemo Mkangara, Chipuputa na Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi hata TANESCO Mkoa wa Mtwara imekuwa ikijitahidi kufanya miradi. Nilipofanya ziara mwaka jana zaidi ya mitaa saba TANESCO imefanya miradi, lakini kwa eneo maalum ambalo ni maeneo aliyoyataja yameshaingia kwenye mpango wa utekelezaji wa mradi wa ujazilizi unaoanza Machi, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, hata alipofanya ziara Mheshimiwa Waziri wa Nishati pia ametoa maelekezo yale ambayo tuliyaelekeza siku za nyuma na kwa kuwa Mtwara imepitiwa na bomba la gesi na Serikali ilitoa punguzo kwa ajili ya kuwasambazia umeme wananchi wa maeneo ya gesi na mitaa mingi ipo katika Mtwara Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge ambaye amekuwa akifuatilia mara kwa mara kwamba, vijiji, mitaa aliyoitaja na vijiji katika Manispaa ya Mtwara Mikindani na maeneo ya Mtwara vitapatiwa umeme na kazi zinaendelea na mradi wa ujazilizi utaanza mwezi Machi, 2019. Ahsante sana.