Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Wakazi wa Kitongoji cha Mafulungu kilichopo katika Kijiji cha Ilangali, Kata ya Manda wanajishuhgulisha na uchimbaji wa madini. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wakazi hao ili shughuli zao za uchimbaji ziwe za ufanisi na zenye tija?

Supplementary Question 1

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza nawapongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri pamoja na Waziri wake kwa namna ambavyo wanafanya kazi kwenye Wizara hii. Hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa eneo lile na Tarafa nzima ya Mkwayungu limegundulika kuwa na madini mengi sana ya gypsum na dhahabu kwa upande


wa Mafulungu na ninyi Serikali mlikuwa mmeona kabisa watu wanachimba na wanapata fedha na nyie mnapata kodi lakini baadaye mlisimamisha uchimbaji wa madini ya gypsum. Je, ni lini Serikali itawafungulia wale wachimbaji wengine ili waendelee kuchimba na nyie muendelee kupata mapato na wananchi waendelee kufanya kazi zao?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuongozana nami ili twende tukajionee hali halisi ya watu wanaochimba dhahabu Mafulungu na wale wanaopata tabu ya kuchimba madini ya gypsum pale Manda ili tukaone na tukatatue matatizo yao kwa macho huku akishuhudia? Ahsante. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtera, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijajibu nimpongeza Mheshimiwa Livingstone Lusinde kwa kuweza kufuatilia mambo ya wapiga kura wake na hasa wachimbaji wa maeneo ya pale Manda. Kwa kweli Mheshimiwa Mbunge anafanya kazi kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba wachimbaji wa gypsum eneo la Manda na Mafulungu ni kweli walikuwa wamesimamishwa kwa sababu hawakufuata taratibu ambazo zilikuwa zimewekwa na Tume ya Madini katika uchimbaji huo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakwenda na watafunguliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niwataarifu wachimbaji wote wa gypsum na wachimbaji wengine wote Tanzania, madini ya gypsum tuliyazuia kwa maana ya madini ghafi kuyapeleka nje ya nchi, naomba wapitie GN Na.60 ambayo tumeitoa siku ya tarehe 25 Januari, waangalie ile GN ambayo imetoa mwongozo wa madini yote,
wanachenjua katika kiwango gani na kiwango kipi ambacho kinaruhusiwa kutoa nje ya nchi. Wakishapitia mwongozo huo wachimbaji watakuwa hawapati shida tena katika kufanya biashara hii ya madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Mheshimiwa Mbunge ameomba niongozane naye kwenda katika eneo la Manda kuangalia changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo. Nimhakikishie baada ya Bunge hili niko tayari kuongozana naye twende tukaangalie changamoto zinazowakabili wachimbaji wa Manda tuangalie namna ya kutatua changamoto hizo vilevile tuwawezeshe wachimbaji hawa waweze kuchimba wapate faida na waweze kufanya biashara hiyo ya madini. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Wakazi wa Kitongoji cha Mafulungu kilichopo katika Kijiji cha Ilangali, Kata ya Manda wanajishuhgulisha na uchimbaji wa madini. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wakazi hao ili shughuli zao za uchimbaji ziwe za ufanisi na zenye tija?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Kijiji cha Kwahemu, Kata ya Haneti, kuna vikundi 16 ambavyo vina wachimbaji zaidi ya 200 lakini havina maeneo ya kuchimba madini licha ya kupeleka maombi Tume ya Madini. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu kuwapa maeneo wachimbaji hawa wadogo ili waweze kujikimu? Ahsante. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maeneo ya Kwahemu (Haneti), kuna uchimbaji mdogo mdogo wa madini ya vito. Katika eneo lile kuna leseni moja inamilikiwa na Bwana Dimitri, raia mmoja wa kigeni lakini kuna maeneo mengine ambayo yako katika utafiti kwa maana ya PL. Kama nilivyosema siku zilizopita ni kwamba tunafuatilia zile PL zote ambazo hazifanyiwi kazi tutazichukua na tutazifuta na tutawapa wachimbaji wadogo wadogo waweze kuchimba na waweze kujipatia riziki kama tulivyojipangia katika Serikali yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge watu wa Kwahemu maeneo ya Haneti tuna mpango kabambe wa kuwapa maeneo ya kuchimba. Wale wachimbaji walioko pale nilishafika na wakatoa kero zao na mimi kwa kweli naendelea kuzifuatilia kwa maana ya kuzitatua na tunahakikisha kwamba hawa watu wa Kwahemu watapata leseni na wataweza kupata nafasi ya kuchimba.