Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Kahawa ni zao la biashara na la kimkakati ingawa kwa miaka kadhaa bei ya zao hilo imeendelea kuwa chini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuinua zao hilo Mkoani Kagera ikiwemo kupandisha bei ili kumnufaisha mkulima?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na mikakati mizuri na mingi ya Serikali, lakini bei ya kahawa ya mkulima Mkoani Kagera bado ni Sh.1,000 kitu ambacho kinamuumiza mkulima. Kwa kuwa soko la kahawa linategemea soko la dunia, linategemea mauzo nje ya nchi, mahali ambapo mkulima wa kawaida au Vyama vyetu vya Ushirika hivi vya Msingi hawana uwezo wa kuyafikia hayo masoko. Pia kwa kuwa msimu unaofuata wa kahawa unaanza hivi keshokutwa mwezi wa Tano, ili makosa yasijirudie mkulima akaendelea kulipwa 1,000, je, Taasisi za Serikali ambazo zinahusika na utafutaji wa masoko wana mipango gani ya kwenda kule nje ya nchi wakawatafutia Watanzania masoko ikiwezekana wakaingia na mikataba na nchi hizo ili Watanzania wauze kahawa zao na waweze kupata bei nzuri? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwenye baadhi ya super market huko China imeonekana kahawa ambayo inaonekana imetoka Uganda imekaangwa tu haijasindikwa zaidi ya hapo na ikawekwa kwenye kifungashio kizuri, robo kilo inauzwa kwa dola 40 ambayo ni zaidi ya Tanzanian Shillings 88,000 wakati sisi mkulima anapata 1,000 kwa kilo. Je, Wizara zinazohusika kama Wizara ya Kilimo, Wizara ya Viwanda na Biashara, wanawaandaaje Watanzania kwa maana ya wakulima na wafanya biashara wasindike kahawa badala tu ya wakulima kuuza zile zilizo ghafi kusudi Mtanzania aweze kupata bei nzuri na hasa hasa mkulima kutoka Mkoa wa Kagera?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mushashu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anataka kujua mikakati iliyopo kwa ajili ya kuongeza bei ya mkulima kutoka Sh.1,000 wanayolipwa sasa mpaka ile ambayo itaridhisha na kukidhi gharama za uzalishaji. Kwanza kwa niaba ya Serikali, Wizara ya Kilimo, baada ya kuona changamoto hiyo ya zao la kahawa, bei yake na mazao mengine, tumeanzisha Kitengo cha Utafiti wa Biashara na Masoko ambacho kimeanza kazi tangu tarehe Mosi Julai, 2018. Lengo la kitengo hiki ni kuratibu na kufuatilia mwenendo wa masoko duniani na kutoa taarifa sahihi kwa wakulima wetu wakishirikiana na wenzetu wa Wizara ya Viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa pili tunashirikiana kwa karibu sana na Balozi zetu zilizokuwa nje. Hapa nichukue nafasi kumpongeza sana Balozi wetu wa China, Ndugu Kairuki kwa kazi kubwa anayoifanya na ameweza kutupatia soko jipya la kahawa nchini China lakini pia na Mabalozi wa nchi nyingine kama za Japan, Ujerumani, wote hawa wamekuja na mikakati mizuri na kupanua soko la kahawa yetu inayotoka hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anataka kujua kwamba mikakati ya kuongeza thamani ya mazao yetu ikiwemo kahawa ili kahawa hii badala ya kuuzwa ghafi tuweze kuiuza wakati imechakatwa. Kwanza niendelee kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa muono huu, lakini nataka nimwambie kwamba Serikali tulishaanza muda mrefu mipango hii na ndiyo maana siyo kwa zao tu la kahawa, hata korosho umeona mwaka huu tumeanza kubangua na mwakani Insha Allah tutabangua zaidi ya asilimia 50 kwenda juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la msingi la kahawa; pia tulishaanza kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vyetu na kiwanda kimojawapo cha Amir Hamza kimeshaanza kuchakata kahawa ya Mkoani Kagera kwa ajili ya kuiuza kahawa iliyokuwa imeshachakatwa badala ya kuuza kahawa ghafi. Pia kwa wakulima hawa tunaendelea kuwasisitiza wajiunge kwenye vikundi vyao vya ushirika ili Serikali tuweze kuwasaidia kwa ukaribu kwenye umoja wao kuongeza mitaji na kununua mashine ndogo ndogo za kuchakata mazao yao, kuuza mazao ya kahawa iliyosagwa badala ya kuuza kahawa ghafi.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Kahawa ni zao la biashara na la kimkakati ingawa kwa miaka kadhaa bei ya zao hilo imeendelea kuwa chini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuinua zao hilo Mkoani Kagera ikiwemo kupandisha bei ili kumnufaisha mkulima?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mwaka jana kwenye msimu wa kahawa, Serikali ilitangaza bei elekezi Sh.1,400 lakini wakulima wamelipwa Sh.1,106. Ni kwa nini wamelipwa hiyo badala ya bei elekezi iliyoelekezwa na Serikali? (Makofi)

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafsi hii. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bilakwate kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kupitia Bodi ya Kahawa, mwezi Julai mwaka jana ilitangaza bei elekezi ya Sh.1,400 ya kahawa. Bei elekezi ni bei ya chini anayotakiwa kulipa mkulima maana yake kama tungeruhusu wafanyabiashara binafsi kununua, lakini kahawa hii haikununuliwa na wafanyabiashara binafsi, ni wakulima wenyewe kupitia Vyama vyao vya Msingi na Vyama Vikuu vya Ushirika waliamua kwenda kuuza kahawa yao kule mnadani Moshi. Kwa hiyo kama wakulima wenyewe kupitia vyama vyao ndiyo waliamua kwenda kuuza kule baada ya kukusanya kahawa yao, kwa hiyo wanakwenda kulipwa kutokana na bei waliyouza kwenye mnada, siyo bei iliyotangazwa ile elekezi kwa sababu hakuna mfanyabiashara binafsi aliyenunua kwa wakulima kule Moshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hivi Vyama vya Ushirika siyo wafanyabiashara bali wanakusanya kwa niaba ya wanachama wenzao, kwa niaba ya wakulima wenzao baadaye wanakwenda kuuza kwa pamoja kule Moshi na ndiyo maana kwamba sasa hivi kutokana na myumbo wa bei mwaka jana, bei ilishuka kwenye soko la dunia na ikaathiri mnadani pale Moshi na ndiyo maana sasa bei hiyo wanakwenda kulipwa kwa kuzingatia bei iliyouzwa hiyo kahawa.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Kahawa ni zao la biashara na la kimkakati ingawa kwa miaka kadhaa bei ya zao hilo imeendelea kuwa chini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuinua zao hilo Mkoani Kagera ikiwemo kupandisha bei ili kumnufaisha mkulima?

Supplementary Question 3

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu na Naibu Waziri anayejibu maswali kule Kagera walifika na wakafanya mambo lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kutoa bei elekezi kama alivyouliza Mheshimiwa Bilakwate kahawa ikauzwa kwa Sh.1,000, huku Karagwe hamna shida lakini ukija Muleba, Bukoba Vijijini, Misenyi bei ya Sh.1,000 watu hawajalipwa mpaka leo, mnasubiri nini? Si muende kama milivyoenda kwenye korosho watu wapate haki zao? Kahawa ipo kwenye maghala lakini mpaka leo watu hawajalipwa na ninyi Wizara ya Kilimo mmenyamaza. Nataka nipate majibu, ukienda Muleba, Chama cha Msingi Magata, Misenyi, Katoro, Kaibanja, Kazinga watu wana shida na kahawa mmeshachukua na hela hawajalipwa, ni lini watalipwa hela zao?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Alhaj Abdallah Bulembo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, sisi Serikali hatujanunua kahawa ya wakulima wa Tanzania popote pale. Wakulima hawa kwa kupitia vyama vyao vya msingi na vyama vikuu waliamua kwa hiari yao kwenda kuuza kahawa wenyewe kule mnadani Moshi. Kilichotokea kwenye Wilaya hizi alizozitaja Muleba, Bukoba na Bukoba Vijijini na sehemu nyingine ni kwamba kahawa yao wameshakoboa, wamefika pale Kilimanjaro Moshi kama nilivyosema kutokana na kuyumba kwa bei kwenye soko la dunia na uzalishaji mkubwa uliotokea kwa nchi ya Brazil kuingiza sokoni zaidi ya magunia milioni saba mwaka jana ikaathiri bei nzima ya kahawa na kusababisha bei kushuka chini mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sababu walienda kuuza wenyewe maana yake ile bei imewakuta wao moja kwa moja. Kilicholewesha mpaka sasa kutolipwa fedha zao ni hiki Chama cha KCU hakijauza kahawa yote. Kwa hiyo, sehemu nyingine hawajalipwa kwa sababu wenyewe hawajauza kahawa hiyo. (Makofi)