Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya utafiti wa gharama za uzalishaji wa kahawa Wilayani Mbinga kwa mara ya mwisho? (b) Je, utafiti huo ulibaini kilo moja ya kahawa kavu inazalishwa kwa gharama gani?

Supplementary Question 1

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, hata hivyo ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni kwa kiasi gani Serikali imesambaza tafiti hizo za gharama za uzalishaji kwa wakulima wa kahawa ili kuwawezesha kufahamu msimu hadi msimu kama wanauza kwa faida ama hasara?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; wakulima wengi wamekuwa wakilalamika juu ya bei duni ya mazao yao mwaka hadi mwaka; je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya tafiti za gharama za uzalishaji kwenye mazao mengine ya kipaumbele kama pamba, tumbaku, chai, korosho yakiwemo mahindi ili kuwawezesha wakulima hao kufahamu gharama zao za uzalishaji na hivyo kufahamu kama wanauza kwa hasara au kwa faida mwaka hadi mwaka? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Msuha kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anataka kujua matokeo ya tafiti hizi zimewafikia namna gani wakulima wa Tanzania; nataka nimueleze Mheshimiwa Mbunge, matokeo yote ya tafiti hizi tumeyifikisha kwa wakulima kwa njia mbalimbali; kwa njia ya mawasiliano ya television, radio na magazeti na vipeperushi vingine, lakini pia kwa kushiriki Taasisi zetu za TACRI na zingine zinazofanya utafiti wa kahawa na mazao mengine kwenye Maonyesho kama Nane Nane na maonyesho mengine ili wakulima na watu wengine wapate elimu ile pale. Pia zaidi, tuna mpango ambao ni endelevu ulioanza tangu SDP I wa kujenga kila kata vituo vya elimu kwa wakulima ili kutoa elimu kwa wakulima muda wote.


Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, anataka kujua kwamba, je, tafiti hizi za kujua gharama ya mazao mengine hasa mazao yale ya kimkakati na mazao ya mahindi ikoje. Kwanza nataka nimpe uelewa vizuri Mheshimiwa Mbunge na nimpongeze kwa kazi kubwa anayoifanya. Zao la mahindi ni moja ya zao la kimkakati. Labda Waheshimiwa wengi hapa wanashindwa kutambua kwamba kipaumbele cha kwanza cha Taifa ni mazao yale zamani tulikuwa tunaita mazao ya chakula. Kwa sasa hivi hatujaweka hiyo demarcation kwamba kuna mazao ya chakula na mazao yote ya biashara. Sasa hivi mazao yote ni ya biashara ila kipaumbele tumeyapa haya mazao nane ya mwanzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kujua tumefanya tafiti ngapi; tumefanya kila zao na kila mwaka kupitia ikutano yetu yote ya wadau. Kwa mfano, nimpe kwenye zao la korosho, kilo moja ya kuzalisha korosho ni Sh.1,350 na kwenye kilo moja ya kuzalisha mahindi, heka moja inatumia Sh.740,000. Kwa hiyo, kila mwaka tunafanya na kupeleka elimu hii kwa wakulima.

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya utafiti wa gharama za uzalishaji wa kahawa Wilayani Mbinga kwa mara ya mwisho? (b) Je, utafiti huo ulibaini kilo moja ya kahawa kavu inazalishwa kwa gharama gani?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini tunakubaliana kwamba masuala ya utafiti kwa ujumla nchini yamedorora sana. Hii ni kwa sababu vituo vya utafiti kikiwemo Kituo cha Utafiti Uyole - Mbeya viko hoi. Uyole iko hoi kimiundombinu na hata kibajeti. Sasa ni lini Serikali itatambua umuhimu wa vituo hivi kama zamani ili kuvipelekea bajeti stahiki tupate kuboresha kilimo nchini na hasa kituo cha Uyole Jijini Mbeya . Miundombinu iko hovyo, hata hali za wafanyakazi ziko hovyo. Before wakati tuko…

NAIBU SPIKA: Umeshauliza swali Mheshimiwa. Mheshimiwa Naibu Waziri wa Kilimo, majibu kwa swali hilo.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbilinyi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze kwa ajili ya kuviona vituo hivyo, lakini nataka nimhakikishie kwamba, kama Serikali hatujawahi kuviacha nyuma vituo hivi kama anavyodai na ndiyo maana mwaka juzi 2017, tulileta Muswada wa Sheria na Bunge hili likaridhia. Kwa ajili ya kuviboresha vituo vile, tuliweza kuunda Sheria maalum ile Sheria hatari na kuunda vituo vyetu nane vikuu na nane vidogo, jumla vituo 16 na kuvipangia majukumu mahususi kwa kila kituo mazao mawili mawili ili kuyapunguzia mzigo.

Mheshimiwa Naibu Spika, yote haya ni katika kuweka juhudi za msingi ili vituo hivi viwe na mazao machache ya ku-focus badala ya kubeba mazao yote na sasa hivi tuko kwenye mchakato wa bajeti na miongoni mwa vipaumbele tulivyovipa na katika hivi vituo vya utafiti kwenda kuviongezea uwezo pia kuviboresha miundombinu yake ili viweze kukidhi matarajio ya wakulima wa nchi hii.