Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nassor Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Ziwani

Primary Question

MHE. NASSOR SULEIMAN OMAR aliuliza:- Kilimo cha mazao ya viungo vya chakula ni biashara yenye tija kubwa duniani kwa sasa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha kilimo hicho hapa nchini?

Supplementary Question 1

MHE. NASSOR SULEIMAN OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa wakulima wa zao hilo hapa nchini kwetu wamekuwa wengi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatafutia soko la uhakika wa bidhaa hizo?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

NAIBU WAZIRI KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwa kuna ongezeko la uzalishaji wa spices hapa nchini na sisi kama Serikali, kama nilivyoeleza kwenye majibu ya swali la msingi, tunayo mikakati ya kusaidia wakulima wetu wa spices kuongeza uzalishaji; sanjari na hilo kuwasaidia kupata masoko ya uhakika. Azma ya Serikali ni kuhakikisha mazao yote ambayo yanatuingia fedha za kigeni tunawasaidia wakulima kuongeza uzalishaji na kuwasaidia masoko ili waweze kusaidia kwenye pato la Taifa na kuingizia Taifa fedha za kigeni.

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASSOR SULEIMAN OMAR aliuliza:- Kilimo cha mazao ya viungo vya chakula ni biashara yenye tija kubwa duniani kwa sasa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha kilimo hicho hapa nchini?

Supplementary Question 2

MHE. NAJMA M. GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa vile spices yaani viungo vya vyakula mbalimbali ni vinaonesha kwamba vina afya zaidi katika miili ya binadamu. Sasa kwa nini Serikali haitumi wataalam wake wakaja Zanzibar kujifunza faida za viungo hizo ili Watanzania wengine walioko Bara ambao hawajui kama vile Wasukuma, Wamasai na makabila mengine waweze kujua na kutumia na kupata afya njema? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

NAIBU WAZIRI KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wake tumeupokea, ni kweli hizi spices zina faida nyingi ikiwemo faida kwa upande afya kwa akinababa na akinamama. Ni ushauri mzuri kwa sababu tunatafuta masoko ya nje, lakini pia masoko ya ndani lazima nayo tuyatumie.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe wito kwa wanaume wenzangu, ukiangalia spices kuna faida nyingi sana kwa upande wa wanaume na ni namna mzuri ya kukuza soko la ndani. Kwa hiyo, ushauri wa Mheshimiwa Najma tumeuchukua.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. NASSOR SULEIMAN OMAR aliuliza:- Kilimo cha mazao ya viungo vya chakula ni biashara yenye tija kubwa duniani kwa sasa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha kilimo hicho hapa nchini?

Supplementary Question 3

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. Wilaya ya Mkinga, Muheza, Korogwe na Lushoto ni maeneo ambayo yanalima kwa wingi mazao ya spices, lakini kwa muda mrefu maeneo haya yamekabiliwa na changamoto ya ukosefu wa huduma za Ugani, masoko duni ya bidhaa hizi na vilevile mazao haya kuuzwa kwa bei ya chini sana. Je, Waziri yuko tayari na wataalam wake kuja kwenye maeneo haya kujionea hali halisi ili kuweza kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima wetu? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

NAIBU WAZIRI KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Dunstan Kitandula kwa namna anavyofuatilia masuala ya spices kwa niaba ya wakulima hapa nchini ikiwemo Jimboni kwake. Nimeshamhakikishia kwamba Serikali kwa kutambua kwamba spices hizi zina potential kubwa ya kutuingia fedha za kigeni, niko tayari kwenda Mkoa wa Tanga na kufika maeneo ambayo ameyataja kuhakikisha wakulima hawa tunawasaidia kwenye upande wa kuzalisha kwa tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo tunawasaidia kwenye mambo ya branding na mikakati ya kimasoko ili kilimo chao kiweze kuwasaidia kuwakwamua kutoka kwenye umaskini, lakini uzalishaji wao usaidie kuchangia kwenye fedha za kigeni za nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)