Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Uwanja wa Ndege wa Njombe umekuwa kero kwa wananchi, kwani upo katikati ya Mji na haujakarabatiwa kwa muda mrefu matokeo yake uwanja huo umejaa barabara hizo. Aidha, watu wanaopita katika barabara hizo zisizo rasmi hukamatwa na kutozwa faini:- Je, ni lini mkakati wa Serikali juu ya uwanja huo ili kupunguza kero kwa wananchi hao?

Supplementary Question 1

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba kiwanja hicho kilijengwa kabla ya uhuru; na kwa kuwa kiwanja hicho kilijengwa kabla ya makazi ya watu hayajasogea maeneo yale na sasa hivi maeneo yale yamejaa makazi ya watu; na kwa kuwa Liganga na Mchuchuma ndiyo mradi ambao unakaribia sasa kuingia katika Mji wetu wa Njombe. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kukihamisha kiwanja hicho na kupeleka sehemu za Tanwati au Mgodeti, ama Ilembula? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS JOHN KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mlowe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Serikali tunatambua umuhimu wa kujenga kiwanja hiki. Pia nafahamu Njombe ina fursa nyingi za kiuchumi, mojawapo Mheshimiwa Mbunge ametaja, tunafahamu pia uhitaji wa huduma hii ya usafiri, hususan wa ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu, suala la ujenzi wa uwanja huu pia mimi mwenyewe nimetembea Njombe, nimefanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa, lakini mara nyingi nimefanya mazungumzo na Mbunge wa Jimbo Mheshimiwa Mwalongo. Kwa hiyo, tulijaribu kuona namna bora ya kuweza kuendeleza uwanja huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mahitaji ya kuendeleza uwanja huu bado yapo, kwa sababu kwenye taarifa ile ya usanifu kama ingeonesha kutokuwa na mahitaji ya kuendeleza kiwanja hiki katika eneo hili, basi ningeshauri namna tofauti. Hata hivyo, jambo hili kama wana Njombe mtaona kwa kushirikiana na Uongozi wa Mkoa mnaweza, mkalizungumze mlilete.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakutahadharisha tu kwamba kwa sababu kulikuwa kuna hatua ambayo imefikiwa na kuna gharama ambazo kama Serikali tumetumia kwamba kuhamisha uwanja huu kupeleka maeneo mengine kunaweza kupoteza fursa ambayo ilikuwa iko tayari imeshapatika kwa sababu inaweza ikatahitaji muda mrefu kufanya usanifu mpya na wananchi hawa wanahitaji huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri tu kwamba uwanja huu tuujenge na kama mtahitaji kuwa uwanja mkubwa, mzungumze katika level ya Mkoa halafu ushauri wenu muulete, sisi kama Serikali tutauzingatia.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Uwanja wa Ndege wa Njombe umekuwa kero kwa wananchi, kwani upo katikati ya Mji na haujakarabatiwa kwa muda mrefu matokeo yake uwanja huo umejaa barabara hizo. Aidha, watu wanaopita katika barabara hizo zisizo rasmi hukamatwa na kutozwa faini:- Je, ni lini mkakati wa Serikali juu ya uwanja huo ili kupunguza kero kwa wananchi hao?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi nami niulize swali moja dogo la nyongeza. Dodoma sasa ni Makao Makuu ya nchi, kiwanja cha ndege kilichopo hakikidhi haja ya kutua kwa ndege kubwa. Je, ule mkakati wa Serikali kukamilisha uwanja wa ndege wa Msalato umefikia wapi?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS JOHN KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nkamia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme tu kwamba ni kweli Serikali imefanya Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi na niseme tu kwamba uhimu wa kuwa na kiwanja kikubwa cha Kimataifa upo. Hatua ambazo zimefikia Mheshimiwa Nkamia anafahamu, liko eneo la kutosha kabisa kuweza kujenga huo uwanja.

Mheshimiwa Naibu Spika, anafahamu na kwa kauli ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa kwamba ule ufadhili kwa ajili ya kujenga uwanja huu kulikuwa kuna hatua nzuri kwamba tutapata fedha za kutosha kujenga uwanja huu. Ili huduma iweze kuanza, Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo kwamba badala ya kuanza na kujenga majengo makubwa ili huduma ianze, tutaanza kutengeneza runway ili ndege zianze kushuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Nkamia juhudi za kuujenga uwanja huo ziko katika kasi ambayo siyo ya kawaida. Kwa hiyo, nimtoe hofu yeye na Waheshimiwa Wabunge na wananchi wote ambao wanakuja kupata huduma katika Makao Makuu kwamba tumejipanga vizuri kuweza kujenga huu uwanja. Kwa hiyo asiwe na wasiwasi. Avute subira, muda siyo mrefu ataona mambo yanavyoendelea. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Uwanja wa Ndege wa Njombe umekuwa kero kwa wananchi, kwani upo katikati ya Mji na haujakarabatiwa kwa muda mrefu matokeo yake uwanja huo umejaa barabara hizo. Aidha, watu wanaopita katika barabara hizo zisizo rasmi hukamatwa na kutozwa faini:- Je, ni lini mkakati wa Serikali juu ya uwanja huo ili kupunguza kero kwa wananchi hao?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Changamoto iliyopo Njombe inafanana kabisa na changamoto iliyopo uwanja wa ndege wa Bukoba kwamba ni mfupi na kupelekea ndege kutua kwa shida au kuruka kwa shida mfano kama Bombadier. Je, ni lini Serikali itaongeza urefu wa uwanja huo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS JOHN KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, nianzie uwanja wa ndege wa Bukoba, yako maboresho muhimu yamefanyika na huduma inaendelea vizuri na ndege zinashuka vizuri na miruko imeongezeka. Pia ule mpango wa kuuboresha uwanja huu tunaendelea na hatua ya kutathmini maeneo ambayo tutahamisha wananchi, Mheshimiwa Mbunge anafahamu ili sasa ule urefu wa sehemu ya kurukia na kutoa ndege iweze kuongezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kwamba zile hatua za kufanya maboresho ya viwanja mbalimbali nchini ziko kwenye mpango na Waheshimiwa Wabunge wanafahamu, mara kadhaa tumezungumza namna ya viwanja, hata leo nimerejea kuzungumza viwanja vingi ambavyo tunaendelea kujenga.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaendelea kuimarisha ili kuhakikisha kwamba tuna viwanja wa ndege ambavyo vitamudu kutoa huduma katika maeneo ya Mikoa yote. Tutaendelea kutoa maeneo mengine ambayo ni maalumu kama ilivyoonekana kwamba uwanja wa ndege wa Mafia, kama nilivyozungumza jana, tunaupeleka katika hatua uwe na hadhi ya kimkoa ili huduma ziongezeke.

Mheshimiwa Naibu Spika, viko viwanja vingine ambavyo tunaendelea kuvipanua. Kwa mfano, tunaendela kupanua uwanja wa ndege wa Kigoma, Tabora, Shinyanga na Bariadi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge waamini tumejipanga kuhakikisha kwamba pamoja na Serikali kuendelea kuliboresha shirika letu kwa kununua ndege, italeta maana pale ambapo Serikali inanunua ndege na ndege zinaenda kuwahudumia Watanzania kwa ujumla. (Makofi)