Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. SAADA SALUM MKUYA aliuliza:- Kumekuwa na changamoto mbalimbali katika Muungano ambazo zinaendelea kutatuliwa mojawapo ikiwa ni ajira za Muungano ziwe asilimia 21 kwa upande wa Zanzibar. (a) Je, ni kwa kiasi gani makubaliano hayo yametekelezwa hadi sasa? (b) Je, ni ajira ngapi zimepatikana kwa utaratibu huu?

Supplementary Question 1

MHE. SAADA MKUYA SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante lakini nachuka fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake ambayo yametoa mchanganuo mzuri na unaleta matumaini na tunatarajia kwamba hizo changamoto zitatatuka karibuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwongozo huo haufuatwi katika mashirika ya Muungano, je, Serikali lini itatoa utaratibu huo wa mwongozo katika mashirika ya Muungano kuona na yenyewe yanafuata utaratibu huu katika ajira?

Swali langu la pili ni kwamba utaratibu huu umekuwa ukifuatwa kama ambavyo umeelezea, lakini bado umekumbwa na changamoto, kuna mfumo gani ambao unafuatwa ili kufanya assessment kuona kwamba huu utaratibu liowekwa unafuatwa katika taasisi zote za Muungano?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Saada Mkuya, lakini pia na mimi nichukue fursa ya kumpongeza kwamba mara nyingi tumekuwa tukishirikiana kwa namna ambavyo tunaweza kutatua changamoto za Muungano, lakini kama nimeeleza kwenye majibu yangu ya swali la msingi kwamba tayari mashirika haya tumeyapa mwongozo na suala kubwa sasa ni ufuatiliaji kwa namna gani wanatekeleza mwongozo ule.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia suala la pili juu ya assessment, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira tunawajibika moja kwa moja kupata taarifa kutoka kwa wenzetu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utaratibu wa kufuatilia assessment huu tumeuweka vizuri na tumeweka bayana, tutakavyo kutana nitamuelekeza vizuri namna ambavyo tumetekeleza. Ahsante.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongezee katika majibu mazuri aliyotoa Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni jambo muhimu sana ambalo linatusaidia kuimarisha Muungano wetu. Lazima nikiri kwamba katika maeneo ambayo hatufanyi vizuri ni hili la uwiano wa watumishi katika Taasis za Muungano na Wizara za Muungano, lazima tukiri ukweli huo. Bahati nzuri maamuzi yalishatoka na sisi kama Ofisi ya Makamu wa Rais na kama Serikali katika kuhakiksha kwamba maamuzi hayo yanatekelezwa kwa haraka tumeshirikiana na wenzetu wa Ofisi ya Rais, Utumishi kuhakikisha kwamba wanafungua Ofisi Zanzibar na kuajiri na kutangaza na kufanya interviews kwa Zanzibar vilevile.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutampa jedwari la kuonesha kila taasisi ya Muungano iwe Benki Kuu iwe TCRA na watu ilionao, Wazanzibari na Wabara ili kuwe na uwazi na tusaidiane katika usukumaji wa jambo hili, hilo la pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa rai vilevile kwa vijana wa Zanzibar ambao wanaomba nafasi katika taasisi za Muungano kuandika address sahihi, kwa sababu msingi wa taarifa tunazopata ni anuani kwenye maombi. Kwa hiyo, wengine ni Wazanzibar lakini wanaandika anuani za Bara; kwa hiyo, hatupati taarifa sahihi kuhusu hasa idadi ya Wazanzibar na watu wa Bara katika nafasi hizi. Kwa hiyo, wito wangu ni kwamba ukiandika anuani sahihi inasaidia kupata takwimu sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingi Wazanzibar wapo wengi zaidi kuliko inavyoonekana kutokana kwamba walioomba kazi hiyo kutokea Bara na waliandika anwani za Bara.