Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- (a) Je, barabara ya Kilwa imeshakabidhiwa kwa Serikali kutoka kwa mkandarasi aliyejenga barabara hiyo (KAJIMA)? (b) Je, barabara hiyo ipo katika kiwango kinachotakiwa? (c) Je, ni nani anagharamia ukarabati usiokwisha wa barabara hiyo kati ya Serikali na mkandarasi?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze sana Serikali kwa usimamizi makini wa barabara ambao ndiyo ulibaini kwamba barabara hii ilijengwa chini kiwango na kumtaka mkandarasi airudie kwa gharama zake hata hivyo nina maswali mawili madogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, baadhi ya mitaro iliyojengwa katika barabara hii inapeleka maji kwenye majumba ya watu hasa maeneo ya Mtoni kwa Azizi Ally na Mtoni Mtongani. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kuwapeleka wataalam kwenda kuiangalia upya mifereji hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini sasa Serikali itamalizia kipande cha kutoka Mbagala Rangi Tatu mpaka Kongowe kwa ujenzi wa barabara mbili?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza pongezi alizozitoa nazipokea. Pili, kuhusu mitaro kupeleka maji majumbani, sisi kama Serikali tutashirikiana na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili kuhakikisha kwamba tunayatazama vizuri maeneo ambayo yana matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuendelea na ujenzi wa barabara kutoka Mbagala Rangi Tatu kwenda Kongowe, niseme tu kwamba Serikali inayo mipango ya muda mrefu kuboresha barabara hii.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- (a) Je, barabara ya Kilwa imeshakabidhiwa kwa Serikali kutoka kwa mkandarasi aliyejenga barabara hiyo (KAJIMA)? (b) Je, barabara hiyo ipo katika kiwango kinachotakiwa? (c) Je, ni nani anagharamia ukarabati usiokwisha wa barabara hiyo kati ya Serikali na mkandarasi?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na juhudi za Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kufanya maboresho ya barabara mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam jambo ambalo tunaipongeza sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi, kwa kuwa barabara ya Kilwa maeneo ya Mbagala Rangi Tatu - Kokoto kuelekea Kongowe Mwisho kumekuwa na ufinyu wa barabara na kusababisha foleni kubwa ya magari muda wa asubuhi na jioni. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza upana wa barabara na kuweka vituo vya mabasi maeneo ya Mzinga na Kongowe mwisho ili kuondoa kero kwa wananchi wanaokwenda Kongowe, Tuwangoma, Kigamboni na wale waendao Mkuranga?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza pongezi nyingi alizozitoa nazipokea lakini niseme tu kwamba nampongeza kwa kufuatilia barabara hii na barabara zingine katika Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu mwanzo kwamba tunao mpango wa kuitazama kwa upana barabara hii na mmeshuhudia tunaendelea kuweka maboresho mbalimbali ili kuweza kumudu foleni katika Jiji la Dar es Salaam, kwa hiyo, uvute subira tunalifanyia kazi.

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- (a) Je, barabara ya Kilwa imeshakabidhiwa kwa Serikali kutoka kwa mkandarasi aliyejenga barabara hiyo (KAJIMA)? (b) Je, barabara hiyo ipo katika kiwango kinachotakiwa? (c) Je, ni nani anagharamia ukarabati usiokwisha wa barabara hiyo kati ya Serikali na mkandarasi?

Supplementary Question 3

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwa nini ujenzi wa barabara ya Ifakara-Kidatu unasuasua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia naomba nifahamu ni lini yupo tayari twende wote kwenye hii barabara tukakague tuone shida?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kama ulivyoelekeza tutaongea na Mheshimiwa Mbunge ili baada ya Bunge tutembelee eneo hili.