Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Flatei Gregory Massay
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Vijijini
Primary Question
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 wananchi wa Korogwe waliahidiwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Korogwe - Dindira – Bumbuli. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?
Supplementary Question 1
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika swali la msingi la Korogwe Vijijini na hali ya pale inafanana kabisa na Mbulu Vijijini. Barabara ya kutoka Sibiti-Hyadom-Mbulu kuelekea Karatu imeahidiwa kwenye Ilani. Je, ni lini sasa barabara ile itawekewa fedha hasa ukizingatia kwamba huu mwaka unaelekea kuwa wa mwisho?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Flatei kwa sababu ameifuatilia sana barabara hii lakini anafahamu pia kwamba barabara hii muhimu ziko hatua muhimu sana ambazo zinaendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na kuanza kukamilika kwa ujenzi wa daraja katika Mto Sibiti. Ziko hatua nzuri zinaendelea ili kuweza kujenga kwa kiwango cha lami sehemu ambayo ilikuwa korofi katika eneo hili. Mheshimiwa Mbunge anafahamu pia harakati za usanifu kutambua gharama za barabara hii ambayo anaizungumzia kwamba tunaendelea kukamilisha zoezi la usanifu ili tuweze kujua gharama za ujenzi wa barabara hii. Baada ya kupatikana kwa gharama za ujenzi wa barabara hii, Serikali itaendelea kutenga fedha kuweza kuiboresha.
Name
Timotheo Paul Mnzava
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Korogwe Vijijini
Primary Question
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 wananchi wa Korogwe waliahidiwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Korogwe - Dindira – Bumbuli. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?
Supplementary Question 2
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na naishukuru Serikali kwa kazi waliyoifanya. Pamoja na majibu hayo nina maswali madogo mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa barabara hii kwa mara ya kwanza kabisa iliwekwa kwenye Ilani mwaka 2010 na mwaka 2015 na kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hii Serikali haioni iko haja sasa ya kutenga fedha zaidi na kuongeza kasi ya utekelezaji ili tujenge barabara hii isivukwe na muda wa Ilani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wananchi wa Korogwe Vijijini wamekuwa wakisubiri utengenezaji wa barabara hii kwa hamu na kwa muda mrefu, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili kuongozana nami kwenda Korogwe akaone hali ya barabara hii na kutoa neno la matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Korogwe Vijijini?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Timotheo, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza uniruhusu nimpongeze sana Mheshimiwa Timotheo kwa sababu amekuwa anafuatilia sana mambo mbalimbali kuhusu eneo lake, nampongeza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maswali yake, kwa ufupi nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kama ilivyo kawaida kwamba Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kufanya maboresho ya barabara katika eneo lake. Kwa hiyo, nimuahidi tu tutaendelea kutenga fedha kadri tunavyopata bajeti ili tuendelee kuboresha barabara katika eneo hili. Niliwahi kutembelea katika eneo hili lakini nakubalia nitakuja kwa sababu zipo changamoto nyingi ili nije kuona pia na maeneo mengine. Ahsante sana.
Name
Hussein Nassor Amar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyang'hwale
Primary Question
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 wananchi wa Korogwe waliahidiwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Korogwe - Dindira – Bumbuli. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?
Supplementary Question 3
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Nataka nipate majibu kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kahama – Nyangolongo - Bukwimba, Kalumwa - Busolwa – Busisi, ni lini ujenzi huo utaanza kwa kiwango cha lami?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein, Mbunge wa Nyang’wale, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ziko barabara nyingi nchini ambazo ziliahidiwa na Mheshimiwa Rais na viongozi wengine wakuu. Ni kweli pia katika eneo hili la Nyang’wale kuna ahadi hii ya barabara kutoka Kahama kwenda hadi Busisi. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge labda baadaye tuonane ili angalau tuzungumze kwa upana ili apate details.
Name
Joseph Leonard Haule
Sex
Male
Party
CHADEMA
Constituent
Mikumi
Primary Question
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 wananchi wa Korogwe waliahidiwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Korogwe - Dindira – Bumbuli. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?
Supplementary Question 4
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ni juzi tu hapa tuliona kwamba barabara ya Dodoma-Morogoro ilipata tatizo pale Dumila na watu walipata tabu sana na kuzunguka kule Kilosa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na barabara mbadala na kutengeneza barabara ya lami ya kutoka Dumila-Kilosa mpaka Mikumi?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbilinyi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu upo na barabara hii iko kwenye mpango wa kuboreshwa.